Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Natambua umuhimu wa Mpango kwamba, ndiyo dira ya maendeleo ya nchi kwa maana ya kujua tunatoka wapi, tuko wapi na tunataka kwenda wapi, tunakwendaje na kwa sababu gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri kwa Mpango huu. Naomba nichangie kwa kuzingatia kwamba mimi ni Mbunge wa Jimbo la Chilonwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, miundombinu; barabara zinazounganisha Wilaya, (maeneo mbalimbali na Makao Makuu ya Wilaya), ni mbaya sana na hazipitiki vizuri. Hii inafanya uchumi wa Wilaya inayotegemea sana ushuru wa mazao inakuwa mbaya sana. Kwa kuwa wanunuzi wengi wanafika kwa tabu na hivyo wananunua mazao kwa bei ya chini sana jambo linalodidimiza pia uchumi wa wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kuangalia kwa makini na kuzisaidia Halmashauri na hasa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kwa kujenga madaraja muhimu strategic kama haya yafuatayo:-
(a) Daraja linalounganisha Kijiji cha Msanga na Kijiji cha Kawawa.
(b) Daraja linalounganisha Kijiji cha Chilonwa na Kijiji cha Nzali.
(c) Daraja linalounganisha Kijiji cha Dabalo na Kijiji cha Igamba (Dabalo B)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, viwanda; Wilaya ya Chamwino na Jimbo la Chilonwa kwa jumla hakuna kiwanda chochote. Tunahitaji Agro-Based Industry/Factory na hasa cha ku-process zabibu. Jambo hili litainua uchumi wa mtu mmoja mmoja, lakini pia kukuza uchumi wa Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na kuunga mkono mpango mzima na kuomba hayo niliyoyaainisha hapo juu yafanyiwe kazi.