Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia Mpango huu wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2016/2017-2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa suala la Benki ya Wanawake Tanzania (TWB). Benki hii ilipoanzishwa mwaka 2009 lengo kuu ilikuwa kuwakomboa wanawake kiuchumi kupitia mikopo nafuu, kinyume na matarajio ya wanawake wote nchini, benki hii imekuwa ikitoa mikopo kwa riba kubwa sana, ya asilima kumi na tisa, riba hii imewafanya wanawake kushindwa kufanya biashara zao vizuri, kwa kuwa wanafanya biashara kwa kuhudumia mikopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeupitia vema Mpango huu wa Miaka Mitano, sijaona mwanamke akipewa kipaumbele, ukizingatia mwanamke hata katika jamii amekuwa mtu wa mwisho kuthaminiwa katika kipaumbele. Hivyo basi, naishauri Serikali, imwangalie mwanamke kwa jicho la tatu, hasa katika Mpango huu wa Maendeleo ya Taifa, ili kumwezesha kukabiliana na changamoto anazokutana nazo kama mwanamke katika jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali katika kipaumbele cha fedha katika Mpango huu, basi iongeze mtaji katika Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), kwa kiwango cha shilingi bilioni thelathini, ili ifanye jumla ya mtaji wa benki hiyo, kuwa bilioni hamsini, kwani kwa sasa benki hiyo ina mtaji wa karibu bilioni ishirini.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, katika Mpango huu, katika suala la afya, Serikali imeweka mkakati wa kujenga blood bank mikoani. Mkoa wa Mwanza unayo blood bank katika hospitali teule ya Bugando, lakini wanawake wengi hupoteza maisha wakati wa kujifungua kwa kupungukiwa na damu. Hivyo basi, naishauri Serikali badala ya kujenga blood banks bora inunue majokofu ya kutunzia damu, katika kila Kata na kila Wilaya. Ili kusudi kila kituo cha afya na hospitali ya wilaya, iweze kujitunzia damu, kwa kuwa watu wengi Watanzania hupenda kujitolea damu. Hii itasaidia kupunguza vifo vya akinamama.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naishauri Serikali katika Mpango huu wa Maendelo ya Taifa, kwa kushirikiana na Wizara ya afya itenge fedha za kununulia CT scan katika kila hospitali ya Mkoa, ikiwemo hospitali ya Mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure kwani wananchi hufa kwa magonjwa mbalimbali, ambayo kama kipimo cha CT scan kingekuwepo, mgonjwa angeweza kubainika ugonjwa unaomsumbua ili apatiwe matibabu sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja baada ya kuwasilisha ushauri wangu kwa njia hii ya maandishi.