Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Waziri, Naibu Waziri wa Fedha pamoja na Watendaji wote wa Wizara ya Fedha kwa kuandaa Mipango ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka Mitano, 2016/2017- 2020/2011. Naunga mkono hoja kwa sababu Mpango huu wanaonesha kusaidia kupunguza umaskini kwa wananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa ushauri kwa Serikali kufanya utafiti kwa viwanda ambavyo havifanyi kazi ili kuangalia uwezekano wa kufufua, lakini kwa gharama ndogo, pia kuweka mfumo ambao utawezesha viwanda hivyo kuzalisha kwa faida. Viwanda vizalishe bidhaa ambayo inatakiwa kwa matumizi ya binadamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ili kuhakikisha uzalishaji wa bidhaa za viwanda unakamilika lazima viwanda vitumie gesi kwa bei nafuu ili kupunguza gharama za uzalishaji. Pia kusimamia bei ya mafuta; petroli, diseli na mafuta mengine ya kuendeshea mitambo katika viwanda. Bei ya mafuta ikiwa ndogo au ya chini itasaidia kuendesha viwanda kwa gharama ndogo na kupata faida kubwa ya uzalishaji wa bidhaa. Kuboresha huduma za jamii kama vile, kuboresha miundombinu ya barabara, umeme, maji na Vituo vya Afya itasaidia sana kukuza uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mufindi Kusini ni Jimbo pekee katika nchi yetu lenye viwanda vikubwa na vidogo. Tatizo kubwa tunaomba barabara ya Nyololo - Mtwango hadi Mgololo ambayo imepita katika Viwanda vya Chai, Mbao na Kiwanda cha Karatasi, Mgololo. Barabara hii ni muhimu sana kwa kukuza uchumi wa nchi, naomba ijengwe kwa kiwango cha lami. Serikali ilishafanya upembuzi yakinifu na Mheshimiwa Rais wa Tanzania aliahidi kujenga kiwango cha lami. Pia iko kwenye Ilani ya Chama cha mapinduzi kuwa barabara ya Nyololo – Mtwango kilomita 40, Madinga – Mgololo Kilomita 82 zitajengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naomba ahadi zote za Mheshimiwa Rais ziingizwe kwenye Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2016/2017 - 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.