Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia katika Wizara hii nyeti. Awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniweka salama na kunipa nguvu za kuweza kuchangia siku hii ya leo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya hapo, napenda kutoa pongezi zangu kwa Mawaziri wote wawili ambao wameweza kutoa hotuba zao ambazo zimeonekana zina mashiko. Pia napenda kuchukua nafasi hii kuipongeza Serikali yangu kwa miradi ambayo inaendelea kuzinduliwa katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo, sasa naomba nianze mchango wangu kwa huduma za afya na ustawi wa jamii.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wizara hii ndiyo inayosimamia na kuratibu utoaji wa huduma za afya katika nchi yetu na ni Sera ya ya Wizara ya Afya kwamba kila Kata itakuwa na kituo cha afya. Pamoja na Jimbo la Segerea kuwa mjini na mpaka sasa lina watu 700,000 lakini Jimbo hili bado halina kituo cha afya.
Mheshimiwa Spika, miezi mitatu iliyopita tulifanya ziara na Naibu Waziri wa Afya na kugundua kwamba tuna zahanati ambazo zingeweza kupandishwa kutoka level ya zahanati kwenda kituo cha afya, lakini mpaka sasa hivi hazijapandishwa kuwa kituo cha afya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kumalizia kusoma hotuba yake kwenye ku-wind up aweze kutuambia je, atatumia njia gani kutujengea kituo cha afya au atupandishie vituo vya afya ambavyo tunavyo viwili; kimoja kipo Tabata ‘A’ na kingine
kipo Mnyamani ambacho ni Plan International? Hizi zahanati zote zina vigezo vya kuitwa vituo vya afya, lakini mpaka sasa hivi ni vitu vidogo vidogo tu ambavyo havijafanyika ili waweze kupandisha na kuwa vituo vya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa namwomba Mheshimiwa Waziri, atakapokuja kumalizia kwenye hotuba yake aangalie ni jinsi gani kama wanaweza kutujengea kituo cha afya au waweze kutupandishia kituo cha afya au waweze kupandisha hivi ambavyo vipo na vyenye upungufu
mchache. Kwa hiyo, nilikua naomba hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kitu kingine ambacho nachopenda kuongelea ni kuhusu miundombinu ya elimu hususan Mkoa wa Dar es Salaam lakini katika Jimbo langu la Segerea. Mkoa wa Dar es Salaam, naomba kwa niaba ya wananchi wa Segerea, unakuta mtoto amefaulu anakaa
Kata ya Ilala, lakini yule mtoto anapelekwa kwenda kusoma Msongola. Msongola ni mbali; na hakuna mzazi ambaye anaweza kumlipia mtoto wake nauli kila siku ya kutoka Ilala kwenda Msongola. Kwanza mazingira yenyewe ni magumu na ukiangalia kwa watoto wetu wa kike wanakutana na changamoto nyingi sana wanapokuwa wanakwenda huko mashuleni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa sababu kutoka Kata ya Ilala kwenda Msongola kwanza ukifika Msongola kwenyewe hakuna tena basi ambalo linaenda huko kwenye hiyo shule.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mtoto inabidi atumie pikipiki. Pikipiki kutoka kituo ambacho anatoka kwenda kwenye shule ni shilingi 10,000. Ina maana ni shilingi 20,000 kwa siku. Hakuna mzazi ambaye anaweza kutoa shilingi 20,000 aweze kumlipia mtoto wake kila siku.
Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu watoto wetu wa Dar es Salaam wanafeli kwa sababu hiyo na tuligundua taarifa ilipokuja kwamba Mkoa wa Dar es Salaam umekuwa wa mwisho na Wilaya ya Ilala ndiyo imekuwa ya mwisho kieliemu. Watoto wengine wameamua kupanga vyumba
huko karibu na shule. Unakuta mtoto wa kike amepanga chumba, lakini kile chumba ana-share na mvulana. Kwa hiyo, unaweza ukajua kabisa kwamba hapa hakuna kitu chochote ambacho kinaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba kupitia Wizara hii ambayo najua inashughulikia mambo ya elimu, watoto waweze kupangiwa sehemu waliyofaulu. Mtoto kama anakaa Ilala, amefaulu Ilala, apelikwe shule ya Kata ya Ilala. Kama anakaa Kipawa, basi apelekwe shule hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba sana kwa sababu siyo kwamba nafasi hazipo; nafasi zipo lakini sijui wanatumia utaratibu gani. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lingine nilikuwa nataka kuongelea…
SPIKA: Mheshimiwa Bonnah, Maafisa Elimu wako ndio wanahusika na hilo, nakushauri tu. Endelea tu Mheshimiwa Bonnah.
MHE. BONNAH M. KALUWA: Sawa.
Mheshimiwa Spika, lingine nililotaka kuongelea ni kuhusu fao la kujitoa. Linasema kwamba mtu anatakiwa afikishe miaka 55 ndiyo aweze kupewa yale mafao yake. Sasa hivi kuna watu wanaajiriwa kwa mkataba, anapewa kazi ya mkataba wa mwaka mmoja au miwili. Ina maana
amepata mkataba wa kazi wa miaka miwili, halafu amalize hapo asubiri mpaka miaka 55! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, licha ya hayo, kutokana na maisha magumu ya sasa hivi yanayoendelea, kwanza mtu unakuwa hauko sure kama utaishi kwa muda wa miaka 55. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri aangalie tena upya kuhusu hili fao la kujitoa ili watu waweze kupewa mafao yao wanapomaliza kazi na kazi zenyewe kama nilivyosema ni kazi za mkataba. Kwa hiyo, naomba sana Mheshimiwa Waziri aliangalie hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kitu kingine nilichokuwa nataka kuongelea ni Mfuko wa Barabara. Pamoja na kwamba kuna miradi mingi inaendelea katika Mkoa wa Dar es Salaam lakini pia pamoja na Jimbo la Segerea, lakini tunajua kuna barabara zetu nyingi ambazo ndiyo barabara za mitaa
ambapo Waziri wa TAMISEMI ndio anahusika nazo. Katika Kata ya Kiwalani pamoja na Kata ya Minazi Mirefu kuna mradi mmoja wa DMDP. Huo mradi umekuwa ukipangiwa kila mwaka, sasa hivi mfululizo ni miaka mitano kwamba barabara za mitaani zitatengenezwa, lakini mpaka sasa hivi hatujajua. Tukiuliza Manispaa, bado wanasema kwamba wanasubiri TAMISEMI ili waweze kuwaletea taarifa rasmi ni lini wataanza kutengeneza hizo barabara.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Waziri atakapomaliza, atueleze ili hawa wakazi ambao wanasubiri barabara zao kutengenezwa na kuna wengine tayari wanasubiri kulipwa kwa sababu kuna nyumba ambazo inabidi zibomolewe, wapate muda specific
ni lini barabara zinaanza kutengenezwa ili wajue na sisi tujue kwamba ni muda gani barabara hizo zitaanza kutengenezwa na mimi Mbunge maswali yapungue.
Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja.