Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Umeniomba niongee kwa muda mfupi sana nitajitahidi kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo machache ambayo yamejitokeza yanahitaji niyatolee majibu. Nianze na la kwanza ambalo ni suala la uelewa tu ambalo Mheshimiwa Nkamia alionesha mshangao hapa kuniona mimi niko pamoja na huyu msanii kwa jina la Roma Mkatoliki
anayedaiwa kutekwa pamoja na wenzake watatu siku chache zilizopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati na mimi namsikiliza Mheshimiwa Nkamia Dar es Salaam nilikuwa na kundi kubwa la waandishi wa habari nao walikuwa wanamshangaa kwa nini anashangaa kwa sababu amekuwa kiongozi kwenye Wizara hii anaelewa kabisa Idara ya Habari Maelezo ni Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kwa hiyo, ni ofisi yangu ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni tumehamia Dodoma na Makao Makuu ya Wizara yako hapa LAPF, nikiwa Dar es Salaam ofisi yangu iko Maelezo. Sasa mtu akinikuta Maelezo nimemfuata yeye au yeye amenifuata? Ni vitu ambavyo nataka vieleweke. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijana huyo alipokuwa amepotea mimi ndiye nilikuwa napigiwa simu na ndugu zake na waandishi wa habari, hakupigiwa Mheshimiwa Nkamia au mtu mwingine, napigiwa mimi. Mimi ndiye mlezi wa hii sekta. Mimi nilikuwa nahangaika na polisi huyu kijana kaenda wapi maana ni vitu ambavyo katika Taifa hili hatujavizoea.
Sasa huyu kijana anakuja kuniona ofisini kwangu, kimekuwa kioja tena! Nimekuwa na mkutano naye for one hour ofisini kwangu lakini yule kijana ana picha tofauti kabisa kuliko ramli ambazo zinapigwa huko nje na humu ndani ya Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, amekuja ananiambia aliyeniteka Mheshimiwa naomba tu upelelezi ufanyike in detail kuwa na bastola haina maana mtu lazima atoke Serikalini maana bastola kila mtu anazo. Alichoomba tu alisema tafadhali naomba upelelezi wa kina ufanyike. Kwa hiyo, niliona lazima nimsindikize, ni suala ambalo ni topic nchini, I am the Minister responsible ili kuhakikisha kwamba Watanzania wanaacha kupiga ramli tunapata ushahidi wa kutosha, ndiyo upelelezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu niseme kwamba sasa hivi Sera ya Wizara ni constructive engagement na vijana hawa wasanii. Ndiyo maana hata wiki iliyopita alikuja huyu kijana mwingine anaitwa Ney wa Mitego, akaja ofisini kwangu, sasa mlitaka sijui nimkimbie nikae naye kwenye mgahawa, namkaribisha ofisini kwangu ndio hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki ijayo nakaa na Diamond, ni kijana ambaye nimeona wana mfumo mzuri sana wa haki miliki wanauendesha pale katika mfumo wao, it can be used hata katika nchi nzima kwa wasanii wengine. Sasa ukinizuia nisikutane nao, ukutane nao wewe ili ufanye
nao nini? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, umenipa muda mfupi sana. Kuna suala limejitokeza la lugha za alama, ni Mheshimiwa Ikupa na Mheshimiwa Mollel wameliongelea hili. Ni kweli kabisa, TV zetu bado hazijaanza kutoa huo msaada. Kwa kweli siyo kitu kizuri sana kwa sababu hata Mheshimiwa Waziri Mkuu amelikazania suala hilo. Tuna TV kama tisa hivi nchini hapa ukiachia zile za cable na zote hazijaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hapa ni gharama tu kwamba ukianza kutumia ukalimani lazima kwa siku uwe na wakalimani sio chini ya wanne lakini tumeshaanza majadiliano. Naomba kukuhakikishia kwamba angalau kwa taarifa za habari tu na sitaki nishinikize TV binafsi kabla
sijaanza kuhakikisha kwamba TBC inaonesha mfano yenyewe katika suala hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine Mheshimiwa Kapufi ameongea suala la muhimu sana hapa kwamba hebu tuachane na mipango ya zimamoto katika michezo tuwe na mipango endelevu. Nakubaliana kabisa na Mheshimiwa Kapufi. Kwa muda mrefu sana nchi hii, kwa miongo zaidi ya
mitatu tumekuwa tunalegalega kwenye michezo. Kwa kweli Mzee wetu, baba yetu Ali Hassan Mwinyi hakukosea kusema tulikuwa kama kichwa cha mwendawazimu, kila mtu alikuwa anakuja kujifunzia kunyoa hapa, lakini yote ni kwa sababu tulikuwa hatuamini katika maandalizi ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tumebadilika, naomba niliseme hili na ndiyo maana sasa hivi tunaweza kujivunia hata katimu kama Serengeti kwamba possibility ni kubwa kakarudi na kombe la dunia hapa nyumbani kwa sababu ya malezi. Vijana wale wamelelewa toka wakiwa na umri wa miaka 12, 13, 14, 15 sasa hivi ni under seventeen na hao ndiyo under nineteen watakaotuchezea baada ya miaka kadhaa lakini timu nyingine imeandaliwa sasa hivi kuziba nafasi yao. Tumejifunza hilo kwamba tunahitaji kwa kweli kuandaa hizi talents. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wanatumia academies lakini sisi kwa uchumi wetu kutokana na sera zetu kwamba tunahitaji kila kijana apate opportunity, sisi tumeamua, tena naishukuru sana TAMISEMI, upo hapa Mheshimiwa Waziri kwamba tutumie peoples academies
ambazo ni shule zetu za msingi na sekondari hizi hizi. Ndiyo maana mwaka huu Mheshimiwa Waziri Mkuu amesisitiza lazima tuwe na michezo ya UMISETA na UMITASHUMTA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nimekwenda kupokea kifimbo cha Malkia kuelezea tu kwamba kuna michezo next year ya commonwealth ambayo tulikuwa tunafanya vibaya. Can you believe toka Filbert Bayi avunje rekodi ya dunia miaka 43 bado tuko tu chini sisi. This time tutakuja na medali Watanzania kwa sababu tumeanza maandalizi sasa tena ya nguvu kweli kweli kwa ajili ya michezo hiyo inayokuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uliniomba nikuachie dakika chache, naunga mkono hoja.