Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza Waziri wa Fedha , Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara kwa kuwasilisha Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa ili tuweze kuujadili.
Mheshimiwa Naibu Spika, yapo mambo ambayo naomba Serikali iweze kunipatia ufafanuzi wake:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza viwanda; ni imani yangu kuwa kama viwanda vitaimarishwa nchini, Serikali itaongeza pato la Taifa na tutaongeza ajira kwa vijana wetu nchini.
Ningeomba kujua, nchi yetu ilikuwa na viwanda vingi sana, ambavyo vingi vyao vilibinafisishwa na wawekezaji wengine wamebadilisha matumizi ya viwanda hivyo. Je, nini mpango wa Serikali kwa viwanda hivyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, tulikuwa na kiwanda cha kuchonga almas cha Tancut Iringa, ambacho kilikuwa kinatumia malighafi za ndani, lakini leo hii almas yetu inapelekwa nje kuchongwa. Tungependa Serikali iweke Mpango wa wazi unaoeleza jinsi ya kuanzisha viwanda vitakavyotumia kununua bidhaa za ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, miundombinu ya barabara; ningependa kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha barabara zote za kiuchumi zinapitika wakati wote ili kuweza kuchukua mazao na malighafi kama Mgololo kilichopo Iringa, hiyo ingejengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Iringa ni kati ya Mikoa ya kiuchumi. Kwa mfano, tunalima mahindi kwa wingi, vitunguu, nyanya, chai na tuna msitu mkubwa sana wa miti, lakini barabara zake zote zinazokwenda kwenye maeneo hayo zina hali mbaya sana! Ningependa jambo hili, Serikali itoe kipaumbele. Pia zipo barabara kama ile inayokwenda kwenye Mbuga ya Wanyama ya Ruaha National Park iwekewe lami ili tupate Watalii wengi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, umeme; Viwanda vitakapoanzishwa vitahitaji umeme wa uhakika, umeme usio katikakatika kama tulionao hivi sasa na kuwepo umeme, mijini na vijijini ambao ni wa uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nne, kilimo; kwa kuwa nchi yetu, wananchi wake asilimia kubwa sana wanategemea kilimo na tunategemea Serikali yetu iweke mpango mahususi kwa ajili ya kusaidia wakulima. Wakulima wapatiwe elimu ili walime kilimo cha kisasa na chenye tija na kitakachoweza kusaidia malighafi katika viwanda vyetu pamoja na kupatiwa mikopo katika Benki yetu ya Kilimo. Je, ni kwa nini Serikali isifungue Benki ya Kilimo katika Mkoa wa Dodoma ili Benki hii iweze kufikiwa na mikoa yote kuliko ilivyo sasa, Benki hii ipo Dar es Salaam tu?
Mheshimiwa Naibu Spika, tano, uimarishaji wa miradi ya vyanzo vya mapato; Serikali iwe na mpango madhubuti wa kumalizia miradi ambayo imechukua muda mrefu sana, ambayo inaweza kuongeza pato la Taifa kwa sababu tumekuwa tukianzisha miradi mipya wakati miradi ya zamani inasuasua!
Mheshimiwa Naibu Spika, sita, ujenzi wa reli na viwanja vya ndege; bila Serikali kutoa kipaumbele katika ujenzi wa reli bado tutaendelea kusuasua sana katika ukuzaji wa pato letu la Taifa. Reli itaponya hata barabara zetu nchini na kupunguza hata bei ya bidhaa. Pia Serikali ieleze wazi mpango hata kuhakikisha viwanja vyetu vya ndege vinajengwa ili viweze kusaidia kukuza pato la Taifa.