Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ni suala la kikatiba, Ofisi hii ina jukumu ya kuvisajili Vyama vya Siasa na kuvishauri. Kutokana na majukumu hayo Ofisi ya Msajili haina mamlaka ya kuingilia maamuzi yaliyofanywa na vyama vya siasa na katiba zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Msajili wa Vyama vya Siasa kuwapa viongozi wa siasa ambao tayari wameshajiuzulu katika vyama vyao ni kinyume na Katiba ya Vyama na hata Serikali zote mbili. Kwa maana hiyo, tunamwomba Msajili wa Vyama kutekeleza majukumu yake na kuwaachia vyama kutekeleza majukumu katika vyama vyao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa mambo ya kisiasa kama yalivyoelezwa kwenye hotuba ya Waziri Mkuu naomba niseme kwamba, suala hili si shwari ndani ya nchi yetu. Kauli ya Mheshimiwa Rais kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hali hii inaashiria kutokuwepo na uhuru wa kisiasa wa viongozi mbalimbali wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chama cha CCM kina mamlaka pekee ya kufanya siasa katika nchi hii. Kwa mujibu wa Msajili vyama vyote ni sawa, leo iweje Msajili wa Vyama kuviona vyama vingine vina haki na vyama vingine vikawa havina haki; je, hii ni sawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, madawa ya kulevya, kwanza naipongeza Serikali kwa kudhibiti madawa ya kulevya katika nchi hii. Madawa ya kulevya yanaathiri nguvu kazi ya vijana wetu ndani ya nchi yetu. Ndani ya nchi yetu vijana wengi wamejishughulisha na biashara ya madawa
ya kulevya kama vile cocaine, bangi, mirungi, viroba na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tayari imeunda Tume ya Kupambana na Madawa ya Kulevya, lakini fedha zilizotengwa ni kidogo kutokana na tatizo hili kuwa kubwa. Hata hivyo, hizi zilizotengwa zitumike vizuri ili lengo lililokusudiwa lifanikiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usafiri wa anga, Kiwanja cha ndege kilichoko Pemba ni kidogo mno kinahitaji kupanuliwa kwa sababu ndege zitakazowasili ni nyingi kutokana na abiria wanaingia na kutoka ni wengi hasa watalii wanaokuja kujionea vivutio kama vile nyumba iliyojengwa ndani ya bahari iliyoko, Panga Watoro, katika Kijiji cha Makangale, pamoja na vivutio vilivyoko Meseli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango wangu huo, naomba nijibiwe.