Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii adhimu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya uhai na hewa safi ya oxygen ambayo haikati kodi (TRA) wala (ZRB). Pia nikushuku wewe kwa kuniruhusu nichangie Ofisi hii ya Waziri Mkuu. Nataka nianze na suala moja dogo akisimama Waziri Mkuu kujibu hoja za Wabunge anipatie jibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha aliyotoa Msajili ni fedha ya walipa kodi ambayo hukaguliwa na (CAG) Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali. Fedha hii iliyotolewa na Serikali ikaingizwa katika akaunti ya mtu binafsi zitakaguliwaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kujua NMB Bank nani kawapa ruhusa fedha ya Serikali itolewe kiholelea pasipo kufuata miamala ya kibenki na sheria zake.
Inawezekanaje milioni mia tatu na sitini na tisa (369,000,000) zitolewe kwa siku mbili fedha nyingi kama hizi kutoka akaunti ya chama kwenda akaunti ya mtu binafsi au huyu mtu binafsi ana chama chake mwenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano inapigana vita ya ufisadi na rushwa, suala hili limepigiwa kelele takribani miezi minne sasa, lakini hakuna chombo chochote cha Serikali mfano, Polisi, Usalama wa Taifa na TAKUKURU na hizi ni fedha za wananchi; je, kuna nini au ugumu gani katika jambo hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko ya watu wa usafirishaji wa majahazi katika bandari ya Dar es Salaam; wanalalamikia kodi kubwa wanayokatwa kiasi ambacho
wao hawapati kitu na wanashindwa kutoa huduma hiyo.
Wanakatwa kodi kwa kipimo cha (CDM) na CDM moja wanalipa Sh. 7,500/=. Gari moja la fuso linapakia CDM 80 ni sawa na Sh. 600,000/= ambapo wao wakipakia CDM 80 yaani fuso moja mfano wa mbao wanalipwa Sh. 1,000,000/= milioni
moja tu. Kama ni kweli na sahihi katika fuso moja Serikali inachukua 600,000 /= wenye Jahazi wanapata 400,000/= tu.
Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie tatizo hili. Nilimwomba zaidi ya mara tatu Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi akutane na watu wa Majahazi ili awasikilize na awasaidie katika hili lakini bahati mbaya shughuli za hapa kazi zilimzidi
hakuwahi. Naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu anisaidie juu ya hili. Mheshimiwa Mwenyekiti, nizunguzie (MIVARF); mradi huu wa MIVARF Mkoa wa Kaskazini Unguja Wilaya ya Kaskazini ‘A’ tumebahatika kupata mradi wa Soko la Kinyasuni, barabara ya Chaani Donge na barabara ya Lunga Lunga Polisi hadi binti Saidi. Barabara hizi zimesaidia sana wakulima wa maeneo hayo kwa kupata wepesi wa usafiri wa mazao yao. Ushauri wangu barabara hizi zingefanywa endelevu kwa sababu zinajengwa maeneo ya maji hivyo ni rahisi wakati wa mvua kifusi kuondolewa na matatizo kubakia palepale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu soko la Kinyasini, naomba Serikali isimamie kwa karibu sana ili limalizike kwa wakati kuondoa adha wanayopata wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja. Pia kuna watu waliobomolewa kupisha soko hilo na wanalalamika kutolipwa. Nataka kujua nani anawajibika kuwalipa? Naomba nipatiwe majibu; je, wamelipwa, watalipwa au hawalipwi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.