Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kutoa pongezi kwa Waziri Mkuu na Serikali kwa ujumla kwa kazi kubwa inayofanyika katika Taifa letu. Wananchi wa Tanzania wanayo imani na matumaini
makubwa sana kwa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii napenda kuchangia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwezeshaji wananchi kiuchumi katika eneo hili napenda kuishauri na kutoa msisitizo mkubwa juu ya ahadi ya Rais ya kupeleka milioni hamsini kwa kila kijiji. Serikali katika bajeti ya mwaka 2017/2018 ihakikishe inatenga fedha hizo ili utekelezaji wa ahadi hii uanze kwani wananchi wanategemea fedha hizi katika kuinua uchumi wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sekta ya Madini kazi inayofanyika ni njema hasa utoaji wa ruzuku kwa ajili ya kuimarisha shughuli za ugani. Kwenye hotuba maeneo
yaliyotengwa Mkoani Geita ni Msasa na Matabe tu. Maeneo haya hayatoshi ukilinganisha na mahitaji makubwa yaliyopo hasa kwa wachimbaji wadogo. Kilio kikubwa ni maeneo ya uchimbaji hasa eneo la STAMICO ambalo ni kero ya muda
mrefu. Uwekezaji unaofanyika STAMICO hauna tija kwa Taifa, hivyo, naomba Serikali itazame upya mikataba hii.
Ikiwezekana wananchi (wachimbaji wadogo) wapewe eneo hili la STAMICO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa ahadi ya Rais ya kujenga kilomita 10 za lami katika Mji Mdogo wa Katoro; naomba ahadi hizi za Rais ziangaliwe na zifanyiwe mkakati wa utekelezaji ikiwemo barabara ya Kahama – Bukoli – Geita ahadi ya Rais Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Hivyo ili wananchi waiamini Serikali yao naomba ahadi hizi zifanyiwe kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.