Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kazi kubwa inazofanya dhidi ya kukwamua kiuchumi wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea suala zima la afya hasa katika Mkoa wangu wa Arusha katika Wilaya ya Longido, wananchi walio mpakani mwa nchi jirani ya Kenya maeneo ya Namanga wamekuwa wakivuka mpaka na kwenda kutibiwa nchi jirani ya Kenya. Jambo hili limekuwa kero sana kwa wananchi wa Wilaya ya Longido. Tunaomba Serikali iwasaidie wananchi wa Longido kuwajengea hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Arumeru Magharibi ni jimbo kubwa sana hali inayopelekea wananchi wengi kutofikiwa na huduma muhimu. Naomba Serikali iangalie upya jinsi ya kugawa jimbo hili ili wananchi wengi waweze kufikiwa na huduma muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jimbo hili kumekuwa na migogoro ya ardhi mara kwa mara na migogoro hii inapelekea wananchi kuishi bila amani. Kuna baadhi ya wawekezaji wamejilimbikizia ardhi kubwa na wanatumia tofauti na ilivyokusudiwa. Wananchi wana shida ya ardhi
huku wawekezaji wamejilimbikizia ardhi kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo hili la Arumeru Magharibi kuna tatizo kubwa la akinamama ambao wamekuwa wakitembea mwendo mrefu kutafuta maji. Naiomba Serikali iangalie kwa ukaribu changamoto nyingi zilizomo katika jimbo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jimbo hili lina changamoto kubwa ya barabara, barabara zake ni mbovu. Naiomba Serikali iliangalie hili ilki wananchi wake wafaidike na Serikali yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.