Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa mchango wangu katika bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu na hususani kuhusu maendeleo ya vijana nchini ofisi ya Waziri Mkuu imepewa jukumu la kusimamia maendeleo na ustawi wa vijana lakini kundi hili la vijana
halipewi kipaumbele na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa randama ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 20017/2018 Serikali imefanya shughuli tatu tu ambazo inadai kuwa ndizo shughuli za kusimamia na kuratibu maendeleo ya vijana, hizo ni za mbio za mwenge, mafunzo na kutoa mikopo katika mifuko ya vijana na wanawake katika Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika randama hiyo, Serikali imekiri kuwa kwa upande wa mfuko wa maendeleo ya vijana hakuna fedha yoyote iliyotolewa hadi kufikia 31 Februari, 2017. Hii inadhihirisha kuwa Serikali haina mpango wala mkakati wa maendeleo ya vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Taifa ambalo kiwango cha ukosefu wa ajira ni asilimia 11.7 lakini leo hii Ofisi ya Waziri Mkuu inakuja kusema maendeleo ya vijana ni kusimamia mbio za mwenge na uzinduzi wa miradi 1,387 yenye thamani ya shilingi 498,892,879,808 bila kutoa
mchanganuo wa fedha hizo na kuonyesha ni vijana wa ngapi kutoka mikoa ipi walifanikiwa na miradi ya mbio za mwenge. Aidha, Serikali imesema kuwa inaratibu mafunzo ya vijana hao wametoka mkoa gani na wamepatiwa mafunzo gani na mafunzo hayo yamewasaidiaje kupata
ajira na kujikwamua na umaskini.
Mheshimu Mwenyekiti, ni aibu kubwa kwa Taifa letu kukosa kabisa dira mahsusi ya maendeleo ya vijana na kudhani kuwa miradi ya mbio za mwenge ndio maendeleo ya vijana, kitendo hiki ni kuwahadaa vijana na kuwapa matumaini hewa juu ya uwezeshwaji wa kimitaji kwa ajili ya
shughuli zao za kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashauri Serikali kuacha mara moja kuwahadaa vijana kuwa inawajali wakati vijana wa nchi hii wako hoi hawana ajira na ndio wahanga wakubwa wa dawa za kulevya, UKIMWI na kila aina ya jambo baya. Serikali ichukue suala la vijana kwa uzito
unaostaahili kwa kubuni mpango mahsusi wa kushughulikia utekelezaji wa sera ya maendeleo ya vijana na kuweka mkakati wa kuongeza ajira miongoni mwa kundi hili kwani kuendelea kuwabagua vijana kunawezaa kuliingiza Taifa katika machafuko kutokana na vijana kukata tama ya
maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba kuwasilisha.