Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kuhusu Mfuko wa Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Kamati ya Bajeti kutambua Mfuko wa Bunge kukabiliwa na changamoto za kutopata fedha za Bajeti kwa wakati na mara nyingine hutolewa zikiwa pungufu jambo ambalo linasababisha shughuli za Bunge kuendeshwa kwa kusuasua ama kubahatisha. Niishauri Serikali iangalie upya utoaji wa fedha za Mfuko wa Bunge kwa wakati na kwa kuzingatia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 (kifungu na 48). Hata hivyo ni vyema hata kama watatoa kwa kila mwezi basi fedha hiyo itolewe yote ili Ofisi ya Bunge iweze kutekeleza majukumu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, afya; yapo majengo yaliyotelekezwa miaka 10 mfululizo hayajatengewa fedha hususani jengo la Chuo cha Uuguzi Korogwe. Niiombe Serikali (Wizara ya Afya) iangalie upya namna itakavyokamilisha jengo hilo hata kwa kutengewa fedha kidogo kidogo
hadi kumalizika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza juhudi zinazofanywa na hii Wizara ya Ujenzi lakini niishauri Serikali fedha zinazotolewa kwa ajili ya barabara za changarawe hususani maeneo ya mjini kama vile Halmashauri ya Mji wa Korogwe Wizara ianze kuona uwezekano wa kutenga Bajeti kila mwaka angalau kilometa 1 - 2 kupitia bajeti ya Road Fund. Aidha, kama haiwezekani basi fedha za barabara za changarawe mijini zitengwe na za kutengeneza mifereji kwa kiwango cha mawe ili kuweka uimara wa barabara hizi.