Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata ufafanuzi wa lini uwanja wa ndege wa Lindi utakarabatiwa na kutoa huduma za ndege kama ilivyokuwa kwa hapo awali? Uwanja huu ni miongoni mwa viwanja vya ndege vya zamani hapa nchini lakini pia ni uwanja mkubwa wenye barabara nyingi za kurushia ndege. Uwanja huu umechakaa sana kiasi cha kufanya ndege kuacha kutua jambo ambalo linasababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa Lindi ikizingatiwa kuwa hivi sasa Lindi iko mbioni kuanza mradi wa LNG hivyo kuna haja ya kuboresha uwanja huu ili kurahisisha usafirishaji kwa njia ya anga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu ombi la Mfuko wa Maafa ulio chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuweza kusaidia katika maeneo mbalimbali ya jimboni kwangu ambapo miundombinu ya madaraja yamebomolewa na mafuriko yaliyotokea mwezi wa tatu mwaka huu wa 2017. Madaraja na barabara zilizoharibiwa na mafuriko ni barabara ya Mkwajuni - Namkongo; barabara ya Milola - Nangaru; pamoja na barabara ya Kitomanga - Mvuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiukweli kabisa barabara hizo zimeharibika sana na fedha kidogo zinazotolewa na mfuko wa barabara haziwezi kujenga madaraja hayo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba sana mfuko wako wa maafa usaidie kujenga walau madaraja yaliyopo katika barabara tajwa hapo juu.