Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Ombi kwa Serikali kuzuia mbegu feki mipakani. Iangalie mipaka yote ya Tanzania kuna mbegu feki zinapita na hivyo kuathiri kilimo kwenye mpaka wa Tunduma na Namanga wananchi wanaingiliana katika shughuli na hivyo kuleta upenyo wa kupitisha mbegu feki kutoka nchi za jirani
kama Zambia, Malawi na Kenya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Mapato TRA. Serikali iangalie kwa jicho la tofauti kwa wafanyabiashara wanapokadiriwa na TRA katika maeneo yao ili kulipa kodi, kuna malalamiko biashara zao ndogo na wanakadiriwa kulipa kodi kubwa hivyo kuwafanya washindwe kulipa kodi
na kufunga biashara zao na ukizingatia jiografia ya kupata bidhaa kutoka nje ya Katavi na mikoa ambayo iko pembezoni iangaliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Afya, Serikali iboreshe huduma za Wizara Afya na Elimu bure kuhusu VVU katika maeneo yenye watu wengi hususani migodini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Kilimo na Mifugo naomba Serikali iendelee kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa tatizo na hii inaendelea kuleta upungufu wa chakula kutokana na migogoro hii. Wakulima kuchomewa mashamba, mifugo kuuawa au kupigwa risasi.