Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nikushukuru wewe lakini pia nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2017/2018. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mmoja kati ya Wabunge waliobahatika kuwa katika Kamati ya Katiba na Sheria, Kamati ambayo inafanya kazi kwa karibu sana na Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zote zilizopo chini yake. Tumebahatika kujua mambo mengi na kujifunza mengi na nikuthibitishie kabisa kwamba Ofisi hii na Wizara zake zote wapo vizuri sana katika kuwatumikia Watanzania. Nikuombe wewe na Bunge zima kuunga mkono jitihada za Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kwa kuzingatia muda naomba nijikite kwenye eneo moja muhimu sana ambalo linagusa asilimia 90 ya Watanzania ambalo liko katika ukurasa wa 21 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kuhusu kulimo. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya 2012 asilimia 85 - 90 ya Watanzania tunaishi kwa kutegemea kilimo au moja kwa moja, kibiashara au kwa namna nyingine lakini asilimia 90 ya Watanzania tunategemea kilimo. Kwa mujibu wa sensa ya kilimo na mifugo ya hivi karibuni inatupa takwimu hizo za asilimia 85 - 90 lakini sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 inatueleza idadi ya Watanzania ambao tupo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa wa 21 kwa taarifa tulizonazo, uzalishaji wa mazao ya chakula kwa msimu wa mwaka 2015/2016 ukijumuisha mazao ya nafaka na yasiyo ya nafaka tumezalisha jumla ya tani milioni 16. Tani hizi milioni 16 maana yake zimezalishwa na asilimia 85 ya Watanzania kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012. Kama hivyo ndivyo maana yake kila Mtanzania anayetegemea kilimo amezalisha tani 0.34 au sawa na gunia nne tu za mahindi kwa mwaka mzima wa 2015/2016. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tunaambiwa ziada ya mazao ya nafaka na yasiyo ya nafaka ni tani milioni tatu. Tukizigawa kwa idadi ya Watanzania wanaotegemea kilimo ambao ni asilimia 85 tunapata ziada ya tani 0.07 ambayo sawa na gunia moja tu la ziada. Kwa hiyo, ukiangalia kwa takwimu hizi maana yake Watanzania tunaotegemea kilimo asilimia 85 - 90 kila kaya au kila mtu amezalisha gunia nne za
mahindi na ametumia gunia tatu kwa chakula na amebaki na ziada ya gunia moja. Tanzania ya viwanda hatutaweza kuifikia kwa kasi hiyo ndogo kwenye sekta ya kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naelewa kwa nini asilimia kubwa ya Watanzania hatuna pesa mifukoni ni kwa sababu ziada yetu ni ndogo sana tani 0.07 kwa maana ya gunia moja tu la mahindi kwa mwaka mzima sawa na Sh.35,000 – Sh.50,000. Ziada hii ni ndogo maana yake kilimo katika Taifa letu kinakua taratibu mno.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tumefika hapo? Kwa nini uzalishaji wetu uwe mdogo kiasi hicho? Tani milioni 16 za chakula siyo jambo la kujivunia. Tumefika hapo kwa sababu kubwa mbili. Moja, kilimo chetu hakina dira. Watanzania na taifa hatujui kwenye sekta ya kilimo tunatafuta nini. Tuna maneno ya jumla ya kusema kwamba tunataka ku-address food security, very good. Kwenye food security tumefaulu, Tanzania hakuna njaa mgawanyo wa chakula ukiwa vizuri kila kaya ina uwezo wa kujilisha, kwa hiyo, kwenye hilo tumefaulu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini malengo yetu kwenye sekta ya kilimo siyo ku-address food security pekee. Sekta ya kilimo pamoja na kuwa inakwenda ku-address food security kwa maana ya uhakika wa chakula, sekta hii ya kilimo inawaajiri Watanzania asilimia 90. Kwa hiyo, lazima tutoke hapo kwenye food security twende sasa kukifanya kilimo chetu kiwe biashara na kiwe chanzo cha mapato kwa Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama Serikali tumefanya vizuri kwenye suala zima la uhakika wa chakula lakini bado tuna kazi sasa ya kuwafanya asilimia 85 - 90 ya Watanzania wanaotegemea kilimo waweze kujiajiri katika sekta hiyo. Kwa hiyo, ni vizuri sasa Wizara ya Kilimo itoe dira ni nini kama Taifa tunataka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili ni kwamba kilimo chetu siyo demand driven, hatulimi kwa kuzingatia mahitaji ya soko. Kama tunataka kujitosheleza kwa chakula tulime mazao gani na kwa kiwango gani, uwezo wetu wa ndani wa ku-consume kile ambacho tunazalisha ni upi na
ziada tunaipeleka wapi. Tumeona sekta ya kilimo inayumba sana kwenye eneo la masoko. Mara tunafunga mipaka tusipeleke mazao nje, mara tunafungua mipaka, hatuna uwezo wa ku-forecast production zetu katika sekta hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo ni tatizo na napenda sana Wizara inayohusika ichukue muda wa kutosha kufanya consultation na wataalam mbalimbali lakini hasa na Wabunge wa Bunge hili kwa sababu Wabunge hawa ndiyo wanaoishi na wananchi, ndiyo wanaojua matatizo ya wananchi na sisi ndiyo tunaolima mahindi, maharage, mpunga, soya na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la pili kwenye sekta ya kilimo ni uwezeshaji katika sekta hii umekuwa mdogo sana na uwezeshaji huu wakati mwingine umekuwa holela usiozingatia mahitaji halisi. Serikali imebeba mzigo mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba Watanzania tunapata pembejeo zenye ubora ikiwemo mbolea na kadhalika na zinakwenda kusaidia kuzalisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.