Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kutoa mchango wangu. Nianze kwa kutoa shukrani zangu nyingi sana kwa Waheshimiwa Wabunge wote walioko katika Bunge hili kwa support kubwa waliyonipa na hatimaye sasa
nimekuwa Mrs. Jamal, ahsanteni sana. Haya makofi naomba yaendelee mpaka mwisho najua kuna sehemu yatagoma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe pongezi za dhati sana Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mheshimiwa Jenista Mhagama na Naibu wake Mheshimiwa Mavunde, wanafanya kazi nzuri sana na kazi kubwa sana. Leo nimesimama hapa, kwanza kwa kweli nina hasira kwa sababu kuna baadhi ya vitu ambavyo havijanifurahisha hata kidogo na kuna baadhi ya vitu ambavyo nikiviangalia unamwangalia mtu halafu unasema; hivi huyu anategemea nini? Unakosa majibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa nafasi ya kipekee nimpe pongezi zangu za dhati sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa sana ambayo anaifanya yeye pamoja na Baraza lake la Mawaziri, wanafanya kazi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi ambayo asilimia 32 ya mapato ya ndani yanakwenda kulipa madeni, katika nchi ambayo malimbikizo ya madeni yapo asilimia sita, katika nchi ambayo Mheshimiwa Rais anapozunguka au Waziri Mkuu au Mawaziri wanapozunguka Rais anaanza kuombwa kuanzia vidonge kwenye hospitali mpaka kwenye ndege watu wanalalamika, Rais huyu kwa kazi hizi anazozifanya kwa kipindi hiki kifupi alichofanya kazi, anastahili pongezi kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaweza tukakaa hapa kukaanza kuongea kirahisi rahisi kwamba Rais huyu amefanya hivi, Rais huyu hafai, Rais huyu sijui amefanya hivi ni rahisi sana kuongea namna hiyo, lakini Wabunge baadhi wamezungumza; hivi sisi Waheshimiwa Wabunge maana nianze hata na mimi mwenyewe kwa sababu nipo humu ndani; katika kipindi hiki cha 2016 mpaka sasa hivi mmefanya nini kwenye Majimbo yenu? Hivi kila mtu akisema akae hapa aanze kuulizwa orodhesha ulichokifanya atasema amefanya nini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema makofi yaendelee najua yatagoma; mimi nimekaa hapa Bungeni kwa kipindi cha miaka 12 kuanzia mwaka 2005 mpaka leo hii niliingia hapa Bungeni nikiwa mdogo sana. Naomba kutoa tahadhari kubwa sana kwa Wabunge ambao ni wapya na hasa Waheshimiwa Wabunge ambao ni vijana. Wako watu ambao ni Genuine kabisa kutoka pande zote mbili; kutoka upinzani na pia na huku. Kuna watu ambao wakiongea unajua kabisa huyu anaongea ni kwa kutoka kwenye dhamira yake lakini kwa experience yangu kuna watu nimeshuhudia tangu nimeingia hapa Bungeni miaka 12 hii kuna watu wananunuliwa na ni Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wana interest zao nyuma, mambo yao yameharibika, wanakuja hapa wanataka kutuvuruga. Kuna mtu anakuja hapa anasimama kwa sababu mume wake alikuwa fisadi ameondolewa kwenye madaraka anasimama hapa anataka kutuvuruga.
Kuna mtu anakuja anasimama hapa kwa sababu alikuwa anapewa pesa na mafisadi, mambo yamekuwa magumu anakuja hapa anataka kutuvuruga, kila saa Serikali mbaya, Rais mbaya, sijui vitu gani vibaya; tunaomba samahanini sana hayo maneno yenu mnyamaze mkaongee huko barabarani. Hapa tunataka tukae tuongee masuala ya maana, masuala ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeishi Rwanda kwa kipindi cha miaka kadhaa siwezi kusema ni miaka mingapi na kule walikuwa wanajua mimi ni Mnyarwanda. Nimeishi uswahilini ya Rwanda na nimeishi Masaki ya Rwanda; watu ambao ni viongozi wanakuwa wazalendo, kuna mambo ambayo ni ya msingi, mtu anakaa nazungumza kwa ajili ya nchi yao. Watu wanakaa wana-discuss issues ambazo ni za maana leo hii tumekuwa viongozi ni mambo ya Twitter, sijui Whatsapp, meseji za kipumbavu pumbavu ni aibu kwetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, inatakiwa tutumie muda ambao huu tunao kukaa, kufanya mambo ambayo ni ya maana. Kwa nini hatukai tukashauriana kwamba jamani hebu tufundishane ujasiriamali tunafanyaje, hebu jamani twende tukamfuate Mheshimiwa Waziri wa Fedha, jamani Mheshimiwa hebu tusaidie, tunataka tujiunge Wabunge 20 tufungue kiwanda, Mheshimiwa Waziri wa viwanda hebu tusaidie Wabunge 50 tunataka tukae tuweke mitaji yetu, tunataka tufanye biashara ya maana, matokeo yake watu mnakaa mnaanza kuchanganyikiwa, mnakuwa hamna hela mkitoka hapa maisha magumu, mmekaa wengine hapa mnapiga makelele, mnapata hizo nguvu kwa sababu mpo
ndani ya vyama vyenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inatakiwa watu muweze kukaa kila mtu amekuja hapa kwa nguvu yake na kila mtu amekuja hapa kwa moyo wake na anajua yeye mwenyewe nini kilichomleta. Sasa msikae hapa mnaanza ku-insight other Members of Parliament to turn against the Government hii ni adabu mbaya, mbaya, mbaya kupita kiasi. Kama mna mambo yenu huko pembeni nendeni mkayamalize, kama mna jambo lenu huko pembeni nendeni mkakae mkaongee huko, lakini siyo mnakuja hapa eti Bunge zima likae liongee mambo ya ajabu ajabu…
Taarifa....
MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokisema nilisema kwamba, katika kipindi ambacho nimekaa hapa Bungeni nimeshuhudia Wabunge wa aina hiyo wapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu afikishe salamu zetu kwa Mheshimiwa Rais aende akamwambie kwamba tuko nyuma yake, tunajua kazi kubwa ambazo anazifanya, tunajua Serikali hii kazi kubwa ambayo inaifanya na tuko nyuma yake kwa njia yoyote ile. Hatuwezi kunyamazishwa lakini ninachoweza kuwaambia, hawa ambao wanaweza kupambana naye, yupo mpaka 2025 ambao wanadhani kwamba 2020 ni mwisho, they are very wrong na wanajidanganya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuwaambia hata baadhi ya Wabunge ambao tuko huku kwenye Chama chetu, kila siku nasema na kuna mtu mmoja nimeshawahi kumwambia; You cannot win the fight with your Boss, you are messing up with the very wrong person katika Awamu hii
ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwepo hapa Bungeni, kipindi cha uchaguzi uliopita, wote tulikuwepo hapa labda hawa wengine wageni ambao hawakuwepo lakini walikuwa wanafuatilia. Baadhi ya Wabunge tulikuwa tunaona tabia za ajabu ajabu walizozifanya ukiwa humu ndani, watu na heshima zao. Mimi nimeingia hapa kwa mara ya kwanza ulikuwa unamwona Mheshimiwa Mbunge unadhani kwa sababu ya umri wake ni mtu mzima, ‘shikamoo Mheshimiwa’ baadaye unakuja kukaa baada ya mwaka mmoja, baada ya miaka miwili, unasema kumbe hata ‘mambo’ hastahili kwa sababu ya jinsi vitu anavyovifanya vya aibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunajua na wala siyo siri, tulikuwa tumekaa hapa, watu wakati wa uchaguzi, makundi yaliyokuwepo, sasa mimi nasema hivi; kama yale makundi yalikuwepo, kama ni masuala ya interest nyingine ambazo tunazo tuachane na hizo biashara sasa hivi tukae tujenge nchi yetu. Tukae tufanye kazi, tukae tuanze kuangalia maendeleo ya nchi yetu yanakwendaje, wengine hapa kwanza hata muda wenyewe wa kuuliza maswali hatuna kwa sababu unawaza biashara tu sasa unamshangaa mtu mwingine kila saa amekaa ‘Serikali hii sijui imefanya hizi’ mimi nasemaga hivi hawa watu wanatoa wapi muda? Mwisho mtakosa Ubunge mrudi nyumbani kule maisha yaanze kuwa magumu, shauri zenu. Ndiyo ukweli wenyewe si nyie mnajijua? Niliwaambieni haya makofi yatafika mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata siku moja Simba Wazungu wana msemo kwamba; “The lion does not turn around when a small Dog barks” Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu wala msihangaike na hawa watu ambao wanapiga makelele ya ajabu ajabu, maneno ya ajabu ajabu, wanasema vitu vya ajabu ajabu, ninyi kaeni, fanyeni kazi mwendelee kuwepo kwenye mstari na tuko pamoja, tunaowaunga mkono ndani ya hili Bunge ni wengi zaidi kuliko hawa wachache ambao wanapiga makelele. Tuwaache waendelee kupiga makelele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka niseme; watakuja siku moja kula matapishi yao, wapo watu ambao tumewashuhudia leo mtu anasema hivi kesho anakuja unamshangaa huyo huyo anasimama Serikali hii nzuri sana. Unashangaa haya maneno ametolea wapi, watakuja kurudi
kula matapishi yao lakini wakati huo tutakuwa tayari tumeshawajua.
Mheshimimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nina hasira sana. Naunga mkono hoja.