Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi leo nichangie hotuba ya Waziri Mkuu. Awali ya yote itabidi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema ili nichangie hotuba hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja; sababu, hotuba hii imejali maslahi ya wananchi wa vipato vya aina zote. Pili, niweze kumshukuru kwa kazi nzuri anayofanya Mheshimiwa Waziri Mkuu na Baraza lake kwa ujumla. Hii kauli ya Hapa Kazi kwa
kweli inaonekana kwa vitendo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya yangu ya Kibiti takriban Mawaziri watano wamefika ndani ya mwezi mmoja. Hata wananchi wa Rufiji kwa ujumla wamesema kwa kweli Serikali hii ya Awamu ya Tano inakwenda na wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende sasa katika afya. Nashukuru kwamba Idara ya Afya imetugawia kila kituo shilingi milioni 10 ambazo tumekarabati, kila penye mafanikio hapakosi kuwa na changamoto. Tuna upungufu mkubwa wa watumishi katika Idara ya Afya. Kuna baadhi ya zahanati ina watumishi mmoja-mmoja ikiwemo Kiomboni, Kechuru, Msalale…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge, hebu badilisha hiyo microphone nenda sehemu nyingine.
MWENYEKITI: Aah ok, basi endelea.
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ndivyo nilivyo. Nikupe taarifa tu nina kigugumizi, nina kilema ambacho amenipa Mwenyezi Mungu, hata hii mic ukiibadilisha hutaweza kunibadilisha, haya ni maumbile aliyonipa Mwenyezi Mungu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niongelee suala la kilimo. Wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti bado wanalima kilimo cha Nungu abile, yaani ina maana Mungu yupo, watu wanalima ili kusubiria mvua wakati sasa hali ya hewa imebadilika. Ninachoomba Waziri anayehusika atuletee miundombinu ya umwagiliaji Kibiti ili wananchi walime kilimo chenye tija. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unavyozungumzia kilimo chenye tija kwa sisi wananchi wa Kibiti lazima tuzungumzie masuala ya korosho. Korosho bado Chama Kikuu cha Msingi kina matatizo, kwa sababu wananchi wanalima korosho zao, wanapopeleka katika hayo masoko bado makato yao yanachukua muda mrefu katika kulipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika suala zima la elimu. Tunafahamu Serikali yetu imeweka mfumo wa elimu bure, lakini kila penye mafanikio hapakosi kuwa na changamoto, katika Wilaya yangu ya Kibiti kuna upungufu mkubwa hasa wa watumishi, majengo na nyumba za
walimu. Kwa hiyo, naiomba Serikali yangu huu ni upungufu iliangalie Kibiti kwa jicho la huruma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Benki ya Maendeleo ya Akinamama; sote tunafahamu bila ya akinamama hatuwezi tukasonga mbele. Hawa akinamama lazima tuwaboreshee mazingira yao kwa sababu muda mwingi wa nyumbani akinamama ndio wanalea familia. Tuna kila sababu ya kuangalia kwa jicho la huruma ili katika vile vikundi vyao wapewe mikopo ya bei nafuu. Jambo la kushangaza ni kwamba benki hizi zimekaa mijini tu, je, kule vijijini watafika lini ili na kule akinamama wetu wa vijijini nao wakafaidike? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie na suala la miundombinu kwa sababu, barabara yetu ya Bungulu kwenda Nyamisati haipitiki. Tunaomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana aiangalie barabara hii kwa sababu barabara hii inafaidisha wananchi wa Kibiti na wananchi
wa Mafia kwa ujumla. Mbali ya barabara upo ujenzi wa Gati – Nyamisati, ujenzi huo wa Gati Nyamisati likirekebishwa naamini kwamba wananchi wa Mafia na wananchi wa Kibiti watafaidika na gati hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie kwamba, Wilaya ya Kibiti ina Kata 16, lakini ziko baadhi ya Kata ziko Delta. Kwa hiyo, Delta iangaliwe kwa jicho la huruma kwa sababu miundombinu ya Delta siyo rafiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga hoja asilimia mia kwa mia.