Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasimama mbele ya Bunge lako Tukufu kwa sauti ya huruma sana na kwa unyenyekevu mkubwa, ninategemea pia ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge mtanisikiliza vilevile kwa unyenyekevu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nazipongeza Kamati zote mbili kwa kazi nzuri. Nitachangia vitu vichache tu. Mheshimiwa Kabwe Zuberi Ruyagwa amesema kitu kizito sana leo hapa kwamba kunajengeka utamaduni mpya hapa nyumbani wa kwamba ukituhumiwa tu, wewe ujue tayari umehukumiwa. Hiyo wamesema; once accused, you are condemned guilty. Ni kitu kizito amekisema ambacho sikubaliani naye, lakini kwa hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Susan Lyimo naye hakuwa mbali, asubuhi leo ameongelea hayo hayo akisema kuwa katika vita hii dhidi ya dawa za kulevya kuna Wakuu wa Mikoa wanataja tu majina ya watu, lakini kwa kweli alikuwa anamzungumzia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Vilevile Mheshimiwa Lucy Owenya naye anaona kwa kweli kuitwa tu polisi ni kama kuhukumiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulithibitishia Bunge lako Tukufu kuwa katika operation hii dhidi ya dawa za kulevya, hakuna mtu aliyekurupuka na katika hili Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye ndio alianzisha hii operation, hajaenda nje kabisa ya sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ninukuu kifungu cha 10 cha Drug Control and Enforcement Act kinachoipa Serikali wajibu wa kuja na mikakati na hatua mbalimbali kupambana na tatizo hili la dawa za kulevya. Alichokifanya Mheshimiwa Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni kutekeleza tu sheria hii, naye ni sehemu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi/Kicheko/)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kidogo hapa Bungeni, sijui tunawaonaje Wakuu wa Mikoa, pengine tunawaona hawana wajibu huo kisheria. Naomba tu jamani, sisi ndio tunaotunga sheria, tukumbushane. Ukienda kifungu cha 5 cha Regional Administration Act, kinatamka kwamba Mkuu wa Mkoa ndiye mwakilishi wa mhimili wa utendaji katika eneo lake (The Regional Commissioner shall be the principal representative of the government within the area of his jurisdiction).
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kulikuwepo neno moja aliliongelea Mheshimiwa Kabwe hapa, akatoa na mfano wa Kigoma kule kwamba kuna kachura kapo juu, pale chini unajua kuna mtu; hili hakuna la kuficha! Mkuu wa Mkoa anateuliwa na Rais wa nchi na hawezi kufanya vitu ambavyo havina baraka ya Rais wa nchi. Ukienda kifungu cha 6 cha Regional Administration Act, it is clear, inasema; “The President may delegate any of his functions and duties under written law to any Regional Commissioner.”
(Hapa kulikuwa na muingiliano wa sauti)
tunaanza mambo ya kitoto haya ya kuzimiana microphone, nimepewa…
(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naeleza tu kwamba Mkuu wa Mkoa ana hayo mamlaka, lakini vile vile ukienda kifungu cha 7 kinamruhusu Mkuu wa Mkoa kuagiza mtu kutiwa ndani. Kasome tu, Regional Administration Act, kimepitishwa na Bunge hili hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kulikuwepo na hoja Mheshimiwa Halima Mdee; naomba nimhakikishie Mwanasheria Mdee kwamba sim-quote out of context, lakini aliongelea hapa kwamba vita dhidi ya dawa za kulevya inataka tuwe na pesa kwanza. Ametoa hata mfano wa Marekani, wametumia matrilioni ya pesa katika pesa hii. Angetaka leo na sisi tutumie matrilioni ya shilingi katika hii vita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu, Wamarekani wameshindwa kwa sababu walitanguliza pesa, siyo dhamira, ndiyo maana hii vita imeshindikana mpaka leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi hatujatanguliza pesa, tumetanguliza dhamira. Shida ya Bunge letu hili, tumejaa mgawanyiko kushindana shindana. Leo tungekuja na pesa, mngesema dhamira iko wapi? Tumekuja na dhamira; eeh, pesa iko wapi? Tuacheni tufanye tunavyoweza na tutafika tutakapofika. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuitwa na polisi sio kuhukumiwa. Unajua kuna tatizo hapa la public perception na legal reasoning, wanasheria mko wengi hapa, sio kwamba ukiitwa na polisi basi umefungwa, hapana, umeitwa pale kuisaidia Serikali kujua kiini cha tatizo na kuweza kujua tatizo lenyewe upana wake ukoje ili tuweze kumfikisha mtu anayehusika mahakamani.
Naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa ujasiri, kwa uthubutu wa kujitoa muhanga kuonesha mfano kwamba tunaweza tukapambana na hili tatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kelele za leo ni kelele za mwanzo tu, tusubiri kesho, keshokutwa kama hii operation itaishia hapo mnapofikiria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nimalizie kitu kidogo kwa sababu imekuwa ni kelele kama ya shule ya msingi, naomba tu nimalizie kitu cha mwisho nisiendelee tena.
Mheshimiwa Hussein Bashe ameongea kitu kizuri sana hapa, kwamba tuna matatizo hapa mengine ya ushoga ambayo alianzisha Mheshimiwa Makonda tukamuachia mwenyewe, nataka kumthibitishia Mheshimiwa Mbunge kwamba hatukumuachia na Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla ameligusia vizuri.
Naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba suala lile tulilibeba na tumeendelea nalo kwa sababu tatizo hilo ni kubwa hatutaki kukurupuka nalo, ni kubwa na tutaliambia Taifa ndani ya mwezi huu tumechukua hatua gani. Kwa sababu tumekuja kubaini, kuna NGOs hapa nchini zinatumwa na nchi ambazo zinaamini kwamba mahusiano ya jinsia moja ni haki za binadamu na hizo nchi zinazoamini hivyo zinafadhili baadhi ya vyama vya siasa hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tunachukua muda tuje na ushahidi wa kutosha ili tuchukue hatua. Wanasema aisifuye mvua imemnyea, unapiga kelele nini kama huusiki!
heshimiwa Mwenyekiti, jamani, nimalizie tu kwa kusema naunga mkono hoja.