Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo langu la kwanza naomba nitoe shukrani kwa Serikali kwa kunifanyia ukarabati Kituo cha Lupilo na kunijengea theatre. Hii inadhihirisha uchaguzi wao wa kumchagua Rais jembe na Mbunge jembe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nije kwenye suala la elimu. Wizara ya Elimu kila siku inatoa miongozo, juzi hapa wamesema private school wapunguze ada, wawawekee kiasi cha ada yaani wao Serikali ndiyo wawe waamuzi, lakini hao hao Serikali wanaziwekea kodi nyingi hizi shule za private, sasa tunafanya nini? Ninyi Serikali si mna shule zenu na si mna shule nyingi, kwa nini msiwe mnatoa miongozo kwa shule zenu ili zifaulishe? Ada tunalipa sisi wazazi ninyi nini kinawakereketa? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mzazi mwenyewe ataamua, atachagua mwenyewe shule ya kumpeleka motto wake. Hawa wanapandisha ada kwa sababu demand imekuwa kubwa wasingekuwa wanapandisha ada. Wazazi wenyewe wawe waamuzi, waamue wapeleke au wasipeleke watoto wao katika shule hizo. Kwa hiyo, fanyeni maamuzi kwa shule zenu. Mlikuwa na shule Mzumbe, Pugu, ziko wapi sasa hivi, sifuri tupu! Kwa hiyo, fanyeni maamuzi kwa shule zenu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kwenye hizo hizo shule za private, kwa mfano Jimboni kwangu mimi kuna shule inaitwa Kasita Seminary, Regina Mundi zinafaulisha kweli! Shule hizi zinafaulisha kwa sababu wanaweka madaraja kutoka kidato kimoja kwenda kidato kingine. Mwanafunzi asipofikia wastani wanamrudisha darasa. Sasa ona wanafaulisha, ninyi mnawaamuru watu waende tu, mbona wanapata sifuri? Halafu mnakuja mnalalamika oh, wanapata sifuri; wenzenu wana mikakati na nyie pangeni shule zenu, wekeni mikakati vizuri, faulisheni! Wazazi wenyewe ndiyo wataamua, watakubali watoto wao waende mbele au warudi nyuma. Kwa hiyo, fanyeni ya kwenu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi hatujaja kugombana na wazazi. Mama yangu Ndalichako, mwaka juzi wakati wa kampeni hukuwepo. Sisi tuliokuwepo tulitoa ahadi hizi nzuri kwa wananchi wetu. Hatujaja kugombana na wamiliki wa shule za private, tumekuja ku-entertain, tunataka elimu ya Tanzania iwe juu, lakini sio kwa hiyo miongozo mnayotoa kila siku. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ni kwenye mikopo. Serikali ya Chama cha Mapinduzi jamani nyote ni mashahidi, Mheshimiwa Rais alisema kitu chenyewe ni mkopo halafu kinacheleweshwa lakini sasa hivi hakipo kabisa, siyo kinacheleweshwa hakipo kabisa, ndiyo. Hatujaja kugombana na wanafunzi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii wanasema ukisoma shule ya private hupati mkopo. Wengine wamesoma shule za private kwa sponsor na ni wengi. Kwa mfano, shule ya mama yangu Tibaijuka karibu nusu wanakuwa na ma-sponsor sasa leo hii anafauli kwenda chuo kikuu amepata divison one, eti mnamwambia kwa sababu umesoma shule ya private haupati mkopo. Hatuko kwa ajili ya hiyo, hatujaja kugombana na wanafunzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nne ni hili ambalo sasa hivi limekuwa kama linashika headlines la dawa za kulevya. Jamani mimi naomba niwaambie, sisi viongozi na naomba ni-quote Ahadi Namba 8 ya mwana TANU, nitasema ukweli uongo kwangu mwiko. Kwa hiyo, nitakachosema mtu yeyote akitaka anihukumu akihukumu chama changu kwanza na kama wewe mwana CCM utanichukia, rudisha kadi ndiyo unichukie. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara wa dawa za kulevya hamna asiyewajua, tunawajua! Humu ndani wapo, nje ya Bunge wapo, kwa nini hatuwataji tunakaa kimya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwa ridhaa yako unaniruhusu mimi nitawataja hata humu ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa za kulevya ni pamoja na bangi. Kuna Mbunge alisimama humu alisema bangi hazina madhara, alijuaje kama hazina madhara kama hatumii? Tungeanza na huyu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, viongozi wenzangu, naomba niwahakikishie kama tutakuwa wanafiki mbinguni sisi ndiyo tutakaokuwa kuni. Tunawafumbia macho wafanyabiashara wa dawa za kulevya na tunakula nao. Nimpongeze sana ndugu ya Makonda wa Dar es Salaam kwa kuthubutu kutaja neno dawa za kulevya lakini nimhakikishie katika kila marafiki watano wanaomzunguka, watatu ni wafanyabiashara ya dawa za kulevya, aanze na hao! (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais watu wasikuchezee akiliā€¦
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Goodluck.