Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia. Mimi nitachangia katika suala zima la UKIMWI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa zinaonesha kwamba UKIMWI bado maambukizi yapo nami ninaona kama ni janga la Taifa. Watu zaidi ya milioni 1.4 sasa hivi wameambukizwa HIV na watu 54,000 wana maambukizi mapya na watu 36,000 wamekufa na AIDS, asilimia 53 wanatumia dawa za ARV. Takwimu hizi zinatisha, lakini kitu kinachonisikitisha, Mfuko wa UKIMWI bado haujatoa fedha za kutosha. Zamani tuliona kwamba waliweza kutoa matangazo, kuweka vibao kwa ajili ya kutoa elimu kwa ajili ya UKIMWI, lakini sasa hivi matangazo yale hayapo na tumeona mara nyingi nimekuwa nikizungumzia suala zima la maambukizi ya UKIMWI kutokana na wanawake wanavyoenda saluni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake huwa wanakwenda saluni kutengeneza kucha na wakitengeneza kucha wana-share vile vyombo, zile nail cutters kwa ajili ya kusafishia kucha. Ni hatari sana sababu vyombo vile havisafishwi ni chuma na huwa saa nyingine mtu anaweza akajitoboa na kuambukiza yule ambaye alikuwa ameenda saluni kutengeneza kucha. Sijui ni kwa jinsi gani mpaka leo hii Wizara imeweza kuwapelekea wale wenye saluni elimu hii ili waweze kutumia vifaa vya kinga, maana saa nyingine wanafanya hata scrub, anaweza akam-scrub yule mtu lakini yule mtu ukute ana kidonda au yule anayefanya ile scrubing na yeye ana kidonda, kwa namna moja au nyingine anamuambukiza yule ambaye alikuwa anamfanyia hiyo scrubing.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile hizi treatment centre, unakuta watu wenye UKIMWI wanaenda sehemu moja kwenye kitengo ambacho wanakwenda kupata ushauri nasaha pamoja na kupewa dawa, lakini wamekuwa wanapata unyanyapaa na unyanyapaa bado unaendelea. Mimi ningeshauri, ni kwa jinsi gani Serikali inaweza ikajumlisha magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu na hawa wenye magonjwa ya UKIMWI wakakaa pamoja, wakapewa zile treatment, wakapewa dawa na hii itawafanya wale wagonjwa wenye UKIMWI kuwa na ari zaidi ya kuweza kwenda kupimwa na wale ambao wana magonjwa ya kisukari na magonjwa ya shinikizo la damu wataweza kukubali kupimwa kwa urahisi kwa sababu watajisikia kwamba hawanyanyapaliwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo hii inaenda sambamba na dawa za kulevya na viroba. Hivi ni vitu ambavyo vinapunguza sana nguvu kazi katika nchi yetu, vijana wengi sana wameathirika, tunajaribu kujenga shule lakini sijui hawa watoto watakaokwenda kwenye hizo shule ni nani kama hatutalichukulia janga hili kama janga la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha vijana zaidi ya 550,000 wameathirika na dawa za kulevya . Kati ya hao 550,000 ni 50,000 ni kwa ajili ya kujidunga zile sindano na tunajua kabisa wakijidunga sindano wanaweza wakapata maambukizi ya UKIMWI. Mimi nafikiri Serikali ingewachukulia hawa mateja kama wagonjwa badala ya kuwakamata na kwenda kuwafunga lock up. Hawa ni watu ambao wanahitaji kutibiwa kwa sababu ni wagonjwa na mara nyingi hawa mateja badala ya kuwapeleka hospitali za watu wenye magonjwa ya akili, mimi nashauri mtengeneze centres za kuwapeleka hawa vijana kwa sababau vijana hawa siyo vichaa, unakuta tu wamekuwa mazombi fulani wala hawamdhuru mtu lakini ukienda kuwachanganya na wale wagonjwa wenye matatizo ya akili wale wanakuwa hyper wanaweza wakawapiga, wanachukua vyuma wanapiga watu, lakini hawa wanahitaji kwamba wawekwe mahali vizuri, wapewe dawa, wapewe elimu ili waweze kuondokana na dawa za kulevya .
Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na wenzangu wote kabisa hii habari ya kukamata vijana ambao wanatumia dawa za kulevya wale ni innocent, wanatumia tu zile dawa mimi nafikiri ni vizuri mkawakamata wale wanao-supply na hawa vijana wapelekwe waende wakatibiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka naomba nizungumzie suala zima la saratani; Saratani tunajua kutokana na taarifa ni zaidi ya watu 27,000 wanafariki kwa ajili ya magonjwa ya saratani. Kuna baadhi ya saratani kama elimu ikitolewa ya kutosha yanaweza yakatibika, kama tezi dume, saratani ya shingo ya kizazi, saratani ya matiti inayotokana na ulaji mwingi wa mafuta, kuna Saratani nyingine za ngozi ambazo wanawake wanatumia vipodozi vya kujichubua wanapata ugonjwa wa kansa kutokana na vipodozi. Wizara itoe elimu, wanawake waache kutumia hivi vipodozi vya kemikali kali ili...
(Hapa kengele ililia kuashiri kwisha kwa muda wa Mzungumzaji )
MWENYEKITI: Ahsante.