Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha na mimi kupata fursa ya kuchangia. Nikushukuru wewe mwenyewe, lakini pia niwashukuru Wenyeviti wa Kamati wa kuwasilisha hizi taarifa zote mbili ambazo ni taarifa muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niseme tu kwamba na mimi naunga mkono hoja za taarifa zote hizi mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, tumepokea ushauri wa Waheshimiwa Wabunge kupitia Kamati yao kuhusu uwepo wa mikataba mibovu na mingine inayodaiwa kuwa mibovu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliambie Bunge lako Tukufu kwamba tayari Serikali imechukua hatua, inaipitia na inaendelea kupitia mikataba hii na inaendelea kuipitia. Ushauri wangu ni kwa Wabunge, popote pale walipo, wanapopata taarifa za uwepo wa mikataba mibovu basi wawasiliane na Wizara za kisekta ili walete kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali tuzipitie wote kwa pamoja ndani ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikataba yote kwa kawaida huwa na vipengele vya marekebisho (amendment clauses) ndiyo inayotoa fursa kwa wahusika wa mikataba hiyo kuirekebisaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ambalo naomba kushauri ni hiki ambacho mmeshauri kuhusu Sheria kama ya EWURA na TCRA kutokuwa na utaratibu wa succession plan. Ukweli ni kwamba ziko succession plan, ukisoma jedwali la kwanza la hizi sheria zote mbili, jedwali la pili limeweka muundo wa ile bodi na namna gani ambavyo hawa Wajumbe wanapatikana. Kwa mfano hii ya EWURA, imeweka kwenye Ibara ndogo ya kwanza Chairman anakaa miaka minne, Director General miaka minne, Mjumbe mmoja anakaa miaka mitatu, Wajumbe wawili wanakaa miaka mitano. Halafu ana fursa ya reappointment, na vivyo hivyo hata ya TCRA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia Sheria zote za bodi zinatoa fursa ya reappointment for one more other term, hii yote imewekwa mahsusi kwa ajili ya kuendeleza ile succession plan na institutional memory ya wale wajumbe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambayo nilikuwa naomba kushauri ni hili suala la Msajili wa Hazina. Ukisoma ile Sheria ya Msajili wa Hazina, kifungu cha 8 na kifungu cha 10 kilifanyiwa marekebisho mwaka 2010 na kupitia Bunge lako Tukufu kupitia Sheria Namba 15 ya mwaka 2015 tumefanya mabadiliko pia kifungu cha 10 tukaongeza 10(a), vifungu vyote hivi vinampa mamlaka Msajili wa Hazina hata kusimamia hii Mifuko ya Hazina kwasababu inataja juu public corporation na statutory corporation havikuiondoa hiyo mifuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunatambua pia kwamba mifuko hii kuna wasimamizi wengine kama SSRA na Benki Kuu. Tutakachofanya ndani ya Serikali ni kukaa namna gani sasa tumuwekee mipaka huyu Msajili wa Hazina kusudi tusije baadae tukaleta mgongano, lakini kwa ukweli ni kwamba anayo mamlaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nikushukuru tena. Naunga mkono hoja.