Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiaw Mwenyekiti, kwanza niwapongeze wenzetu wa Kamati zote kwa kazi nzuri walizofanya. Najua ukiwa wa mwisho itakuwa point zako nyingi zimechukuliwa lakini nimebaki na chache ili nisirudie rudie zile ambazo wenzetu wamezisema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa tu nataka ni-observe mambo mawili, kwamba katika nchi yetu nafikiri tunatakiwa tuongeze uzalendo zaidi maana naona kwamba kila wakati tunasema tukaangalie wawekezaji kutoka huko nje. Hatuweki misingi ya kusema tujenge uwezo wa watu wetu wa ndani. Kama wenzangu waliotangulia waliosema Wachina, nakumbuka hata kile kisiwa cha Hong Kong wakati wazungu wale wa Uingereza wakitakiwa waondoke, 10 years before, waliwawezesha watu wao wawe na mitaji mikubwa waweze kuwekeza kwenye vie viwanda vikubwa na wawe board members ili waweze kujifunza na kupata uzoefu, ndiyo maana wenzetu mpaka leo China wamekwenda mbele sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwetu tunajua kwamba kuna aliyesema 50 percent ya mafuta yanaingizwa kutoka nje, infact ni 70 percent ya mafuta ya kula wakati alizeti zinalimwa sana na infact tungeongeza pressure au misaada kwa wakulima wetu wa zile alizeti tungehakikisha kwamba hatu-import mafuta ya kula. Wenzetu kutoka Kenya wanakuja kuchukua vitunguu hapo Singida wanavi-re-export, sisi tunabaki tunaangalia wakati vitunguu vinatoka kwetu. Tunadharau vitu vidogo vidogo, lakini tungeangalia bottom up tungejikuta tunasaidia wakulima zaidi as a result tukaboresha na umaskini tukauondoa katika level ile ya chini kwa kuweza kuunganisha viwanda vyetu na malighafi kutoka kwa wakulima wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tunaangalia institutions zetu, tuna TEMDO, CARMATEC, CBE, Dar Tech, Arusha Technical; wote hawa wanafanya kazi ambazo wangewekwa pamoja, wakasaidiwa, wangeweza ku-invent vitu vizuri na ushauri mzuri kwamba tu-invest kwenye nini na waweze kuweka utaalam wao pale. Hivi vyote vimewekwa pembeni tunaangalia watu wa nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabalozi wetu wametumwa nje, wanaambiwa muangaie wawekezaji, samahani sikumbuki labda imesemwa hiyo; lakini ningetegema nchi iwe ime-identify ni mazao gani tunaweza ku-export ili kila Balozi anayekwenda nchi fulani tumwambie atuangalilie soko la kitu hiki na kile na kile. For example, vitu vinavyolimwa Tanzania ambavyo tunaweza kupeleka nje ni vitu kama nini? Tunaweza kusema ni mzaha mzaha lakini tangawizi ambayo tunaweza kuiboresha, ni nchi yetu ina-produce tangawizi the best katika Afrika, lakini hivyo vyote hatuviangalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unaangalia maziwa tuna-import mengi, kwa nini hatuboreshi viwanda vyetu watu wakasaidiwa, wafugaji wakazalisha maziwa kuliko ku-import maziwa, viwanda vile vikakuzwa. Unaona kuna ASAS Iringa, kuna kiwanda cha maziwa cha Tanga hatutaki kuviboresha badala yake tuna-import maziwa ya unga, yanakuwa imported sijui madawa gani kutoka South America yanakuwa packed, tunapata maziwa ya hovyo hovyo. Sasa kuna mambo mengi sana, kwamba bado uzalendo wetu haupo kuangalia kwamba tukuze from the bottom up halafu tuwe na inward looking badala ya kila siku tunasema kalete wawekezaji, wawekezaji ambao wakija wanatunyanyasa. Tunajua kuna viwanda watu wamewaweka huko hawajui hata Kiswahili sasa ndiyo tunayoyataka hayo. Mimi nafikiri ifike high time ambayo tutaweza kuangalia kwamba tunasaidiaje watu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie suala la mitaji, banks zinaweka riba kubwa sana kwa nini tusiwe na strategic plan ya kuona kwamba tuna-identify viwanda gani ambavyo tuwaboreshe watu wetu na tuwape…….
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana.