Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa fursa na mimi niseme kutoka awali kwamba naunga mkono taarifa za Kamati zote mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la viwanda halina mjadala, Bunge lako Tukufu hili limekubali kama Serikali inavyotaka kwamba ili tufike nchi yenye kipato cha kati ni lazima tupitie kwenye viwanda. Lakini nataka niwambie kwamba kama tunataka tufaulu kwenye viwanda lazima tuwe na uwezo wa ushindani kwa sababu bidhaa za viwanda zitashindana na bidhaa za nchi nyingine.
Kwa hiyo, nataka niwaeleze wale waliokuwa wanataka viwanda vya miaka ya 1960 na 1970 vifufuliwe, inaweza ikawa hasara kwetu kwa sababu uwezo wa ushindani utakuwa mdogo, ila tutake viwanda vipya vya korosho na sehemu zingine vianzishwe. Tusipoangalia hilo tutajiingiza na mimi nafurahi sana Serikali hii ya Awamu ya Tano inalijua hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilitaka niseme jambo moja ambalo lilishaanzishwa na sisi tusipolipeleka mbele tunaweza tukajirudisha nyuma. Kupitia SIDO na Wizara ya Viwanda kulikuwa na mradi wa MUVI ambao unajua kila Wilaya inaweza ikawa na viwanda vipi ili tuwe na uwezo wa kubadilishana ndani ya nchi ambamo viwanda vingi ni vya kuchakata mazao ya kilimo katika kuongezea thamani.
Kwa hiyo, naomba mradi huu wa MUVI muuangalie upya kusudi kusiwe na Wilaya ambayo haina viwanda, ama sivyo tutaifanya nchi iwe na sehemu nyingine ina viwanda, sehemu nyingine haina viwanda halafu wengine wakawa nyuma na wengine wakawa wamepiga hatua. Kwa hiyo, naomba sana, hili liangaliwe, tuwe na nchi ambayo ina uwezo wa kuwa na viwanda nchi nzima na kwa kuangalia kwamba kila Wilaya ina-specialize kwanza issue ya division of labour na specialization lazima iangaliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, mimi nataka kusema habari ya mikataba. Mikataba ya nchi hii imetayarishwa na wataalam na wataalam ni binadamu. Inawezekana kwamba kuna maeneo yamekosewa, lakini sidhani kama mikataba yote ni mibaya kiasi hicho. Kwa hiyo tuwe watu wa kuangalia mikataba ipi inaupungufu na mikataba ipi ambayo ni mizuri iendelezwe na ile ambayo ina upungufu iweze kuangaliwa na kuboreshwa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kusema kwamba tuhakikishe kweli viwanda vinafanikiwa. Ili viwanda vifanikiwe kuna kitu kinaitwa basic industries au viwanda mama. Viwanda vya chuma, viwanda vya chemicals, viwanda ambavyo vinaweza vikafanya vingine vikazaliwa na vikaendelea kuzaliwa. Tusipofanya hivi tunaweza tukaanzisha viwanda ambavyo havitasonga mbele. Kwa hiyo haya yote tuyaangalie na suala la uwekezaji lazima tulitilie mkazo. Watu wasipowekeza ndani ya nchi, nchi itatawaliwa na watu wengine wa nje. Tulianzisha forum ya uchumi katika kila mkoa, naomba Waziri uendeleze zile forums ili kila mkoa ujue kwamba wanaweza kuwekeza sehemu gani ili nchi yetu iwe na maendeleo sawia kwa kila mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.