Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kukushukuru wewe kwa jinsi unavyoongoza Bunge vizuri, lakini pia kwa jinsi unavyotoa matumaini ya kuendelea kulinda nyumba yako hii kwa adabu na heshima kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2014 nilipata nafasi ya kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze. Katika kampeni zangu, katika matembezi yangu ya ndani ya jimbo kwa maana ya ziara, wanachi wa Jimbo la Chalinze walikuwa wanalalamika sana juu ya uwepo wa ajira. Kwa maana walikuwa wanahitaji sana ziweze kupatikana fursa ambazo zinaweza zikawaajiri. Katika Jimbo la Chalinze kwa kuwa wewe mtani wangu unasimama simama sana Kiwangwa unajua tunazo raw material za kutosha, lakini viwanda hakuna.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii miaka miwili baadaye, ninaposimama hapa, furaha kubwa niliyonayo ni kwamba baada ya miezi isiyopungua mitatu kuanzia leo tutawaalikeni Wabunge ninyi wote akiwepo Mheshimiwa Rais wetu kuja kufungua kiwanda kikubwa cha kuchakata matunda katika Halmashauri ya Chalinze.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nimeanza kusema hivyo? Kwa sababu tunatambua kwamba sera yetu ya kuwa na Tanzania ya viwanda, ndugu zangu Wabunge wenzangu haiwezi kufanikiwa kwa kumwangalia Bwana Mwijage anavyofanya kazi. Nataka niwaambieni ukweli kabisa, Bwana Mwijage, Mheshimiwa Waziri yeye ni sehemu ya kusukuma mambo hayo; kama ninyi Wabunge hamtokuwa wajanja kutumia mazingira yenu, kutumia mazingira ya maeneo tuliyonayo na kuyageuza yawe fursa, ili Serikali ije kutusaidia kuhakikisha kwamba mambo yake tunayoyataka sisi na wananchi wetu yanafanikiwa; hii sera ya viwanda itakuwa ni sera ambayo hatuiishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Chalinze kwetu sisi tuna fursa kubwa sana, mojawapo ni kuwa na logistic center, lakini logistic center ambayo siyo tu kwamba itakuwa inakuja ni kama sehemu ya kufanyia biashara ya kubadilishana vitu, pia sehemu ambayo watu watakuwa wanapitishia mizigo, na fursa mbalimbali. Wanachalinze wametenga maeneo, Mheshimiwa Waziri Mwijage akishirikiana na watalaam wake katika Wizara yake nimshukuru sana, ametupa ushirikaino mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba yale mawazo ambayo siku zote tumekuwa tunayalilia wanachalinze yanafanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ninaposimama hapa logistic center ya Chalinze inawezekana. Kiwanda kikubwa cha tiles kimeshafunguliwa na sasa ujenzi unaendelea vizuri, lakini sio hilo tu kama nilivyosema kwamba sehemu kubwa ya kufanya biashara kwa kingereza sijui wanaitaje maana yake kwa Kikwere tunasema makutano ya biashara. Logistic center ndio mnavyoita?
Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake mama Nagu ameongea logistic center kwa Kimbulu wanavyoita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya yote yanaweza kufanikiwa kwa sababu Serikali yetu inatuunga mkono katika hilo na mimi binafsi bila hata ya aibu niishukuru sana Serikali, kwa sababu kilio cha Wanachalinze kinaweza kupatiwa jibu. Mheshimiwa Lukuvi nimshukuru pia maana kulikuwa na figisu pia pale la upatikanaji wa ardhi, lakini pia kodi kubwa za ardhi. lakini ule utaratibu wa kurasimisha ardhi, toka kwenye mamlaka ya kijiji ili sasa itoke iende kuwa sehemu tengefu kwa ajili ya viwanda nalo pia linawezekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya kwa sababu ninao ushuhuda huo. Pamoja na hayo pia ziko changamoto ambazo Serikali yetu ni lazima iziangalie tunapokwenda kutimiza yale malengo ambayo tumejipangia ya kuwa na Serikali ya viwanda au kuwa na Tanzania ya viwanda. Kwa mfano moja ya tatizo kubwa ambalo Wabunge wengi wamelalamikia hapa ni jambo zima la upatikanaji wa nguvu ya nishati, kwa maana ya umeme. Tumeshuhudia kwa mfano wenzetu hasa kule kwa wajomba zangu Lindi na Mtwara wanalalamika kwamba umeme unatoka kwa siku masaa manne manne, wanasema kila baada ya dakika 20 kama sio dakika 80 umeme unakatika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Tanzania tunayoitaka ya viwanda, moja ya jambo kubwa ambalo lazima tujihakikishie hapa na kama hili hatutakuwa na hakika nalo hii sera ya viwanda itakuwa ni hadithi isiyokuwa na mwisho, au hadithi isiyokuwa na majibu kama umeme wa kutosha wa uhakika hautopatikana katika Tanzania. Mheshimiwa Waziri Muhongo alitueleza kwamba katika upande wa gesi, bado michakato ya kuendelea kusambaza gesi inaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia wametuambia kwamba gesi itakuja hadi huku Dodoma, lakini pamoja na hayo yale maeneo ambayo yamekwishaanza shughuli za viwanda, ni lazima yapewe kipaumbele ili kuhakikisha kwamba sera ile inatimia kwa vitendo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Mheshimiwa Hawa Ghasia Mbunge wa kule Mtwara ameeleza hapa, juu ya jinsi ambavyo mahitaji ya gesi na umeme yanatakiwa kule Mtwara. Pia Mheshimiwa Mwijage wewe mwenyewe umekuja umeona, kiwanda kile mzee, cha kilometa moja, kiwanda ambacho kitakuwa na line of processing mbili, kama hakuna umeme pale itakuwa ni kazi bure na ndoto zako ambazo kila siku umekaa unapiga kelele mpaka wengine ndugu zako akina Nkamia hapa hawaamini, kwa sababu wanaona ni kama hadithi hivi hazitofanikiwa. Kaa vizuri na Mheshimiwa Waziri Muhongo, zungumzeni jambo la sera ya umeme, zungumzeni tuone mambo siyo kwamba yanasemwasemwa tu lakini tuone mambo ambayo yanakwenda sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii mnazungumzia kuweka treni ya umeme, Mheshimiwa Waziri nataka nikwambie mimi mwenyewe ni mshabiki sana wa kupanda vitu hivyo lakini nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Waziri, treni ya umeme hiyo mnayoizungumza na consumption ya umeme ambayo inatakiwa kwa ajili ya kuendesha chombo hicho na kukatikakatika kwa umeme kunakotokea kila siku sina hakika sana kama tunaweza tukafanikiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote Serikali imedhamiria kuhakikisha kwamba ajira zinapatikana katika maeneo hayo. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri kipaumbele cha kwanza katika ajira hizo, mnapokaa na hao wawekezaji waambieni wawape kipaumbele cha kwanza wale wakazi wa maeneo yale. Kwa sababu haiwezekani ikajengwa kiwanda kikubwa kama kile pale Chalinze halafu ajira tukasikia wanatoka vijana Dar es Salaam sijui wapi hili jambo haliwezekani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo nitumie nafasi nyingine pia kumwomba sana Mheshimiwa Waziri hebu hii sera ya viwanda isimamie vizuri brother, kwa sababu kama mambo yakienda vizuri katika viwanda, nina uhakika kuna nyanja nyingi sana ambazo zitakuwa zimekaa vizuri. Kwa mfano viwanda vinahitaji maji, sijajua kwa maji haya yanayosuasua ambayo mpaka leo wana Chalinze bado hawajaelewa tutafikia lini ule mtandao wa maji ukaweza kusaidia watu wote sina uhakika sana Mheshimiwa Waziri kama tutafanikiwa pia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo mashirikiano baina yako wewe, baina ya Wizara nyingine ambazo ni wadau katika lile ni lazima tuyaimarishe ili tuweze kwenda sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja.