Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi hii nichangie kidogo kwenye taarifa hii, lakini nitajikita zaidi kwenye taarifa ya Kamati ya Viwanda na Biashara. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu na nimpongeze sana Mwenyekiti na Kamati yake hiyo, niseme Kamati zote mbili kwa kazi nzuri walioifanya ya kutuchambulia yale ambayo Kamati hizi zinatakiwa kufanya kwa mujibu wa kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kusema Sera hii ya Viwanda ni jambo zuri sana kinadharia lakini utekelezaji wake ndio changamoto kubwa sana. Nadhani hata Mheshimiwa Rais mwenyewe anapata shida pia kwenye utekelezaji wake kwa sababu kaikuta tu kwenye ilani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ambalo siku zote najiuliza na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda yupo hapa ni vizuri akasikiliza. Tunapozungumza uchumi wa viwanda leo, hivi tulikuwa na viwanda vingapi; tumejiuliza kwa nini viwanda vile vilikufa? Kwa nini viwanda vile vilikufa this is the basic question ambayo lazima tujiulize na tuje na concrete research; kutoka pale tunaweza kuanza kufikiria kujenga viwanda vipya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Lakini tukisema tu nakuletea kiwanda leo, kesho, keshokutwa hatuwezi kwenda hivyo. Sidhani hata nchi zilizoendelea kiviwanda zinaenda katika style hiyo; tulikuwa na viwanda vingi MWATEX, MOTEX, lakini viwanda vimekufa; bila kujua aliyeua viwanda hivi tutaimba wimbo huu wa kuwa na Taifa la viwanda leo, kesho na hata milele. Leo tunazungumza kiwanda cha General Tyre utakifufuaje mpira huna? Uta-import mpira kutoka nje utatengeneza gurudumu utamuuzia nani na kwa bei gani? Haya ni maswali ambayo lazima tufike mahali tukae chini tujiulize, tuje na majibu ya kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo sera yetu tunasema tunajenga viwanda; nani anajenga Serikali au watu binafsi? Mfumo wa uchumi duniani sasa hivi, mimi sio mchumi lakini mfumo wa uchumi duniani sasa hivi unazilazimisha third world countries kupiga makofi kwa yale yanayoamuliwa na wakubwa. Leo tunasema watu wafanye investment Tanzania ya viwanda; tuna viwanda karibu 30 vya pamba lakini raw material zinazoingia kwenye viwanda vile hazitoshi. Tuna-import karibu asilimia 51 ya mafuta ya kula kutoka nje, viwanda vya mbegu za pamba ambavyo vingeweza kutoa mafuta havipati material ya kutosha kwa sababu uzalishaji wa pamba wenyewe umeshuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nenda kwenye mawese na alizeti; viwanda vipo vya kutosha, nadhani tuanze sasa pengine tuimarishe viwanda vilivyopo sasa badala ya kuanza kufikiria kujenga vingine. Kwa sababu wasiwasi wangu tukiendelea kuhamasisha ujenzi wa viwanda kwa kiwango kikubwa hata hivi ambavyo vipo tena navyo vitakufa. Kwa sababu mfumo wa soko duniani sasa hivi ni competitive lakini how can you compete with a giant katika uchumi. Hayo ni mambo ambayo lazima tuyaangalie sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa namsikiliza siku moja rafiki yangu, Mjomba wangu, Waziri wa Viwanda anasema amepata soko la mihogo china; sasa nikasema tunahamasisha kujenga viwanda halafu tena tunataka tuuze raw material nje, hivi viwanda vitafanyaje? Ni jambo la kukaa sisi kama Taifa tufanye maamuzi kwa lengo la kuitoa nchi yetu hapa ilipo iende mahali. Nimetoa angalizo tu kwamba mfumo wa globalization duniani leo kwa third world country kama ya kwetu na tukawaomba hawa hawa wakubwa njooni mjenge viwanda, lazima tuwe very careful. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ushauri wangu njooni na concrete research kwamba kwa nini viwanda hivi vilikufa; mkija nayo mkakaa mezani mka-brainstorm vya kutosha mtakuja na policy nzuri sana ya kuleta viwanda ambavyo kweli tunavihitaji. Leo ukimuuliza Mwijage hata ukikutana nae hapo mlangoni anakwambia nakuletea kiwanda, ukikutana nae canteen pale anakwambia nakuletea kiwanda; sasa hata bajeti yenyewe hivi viwanda anasema anakuletea hana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati hapa imetuambia leo kwamba fedha iliyotengwa kwa ajili ya hili zoezi haijatoka; lakini Waziri wa Viwanda yupo tayari kukuletea kiwanda. Sasa I have been asking kwamba hivi viwanda mnavyo kwenye mifuko ya makoti? Tusipowaambia ukweli tutakuwa tunadanganyana na sisi bila kusema ukweli hatuwezi kusaidia nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine unaweza kulalamikiwa hivi kwamba ukaonekana huyu jamaa mbona anasema sema vibaya, no lazima tuseme ukweli kwa lengo la kusaidia Taifa letu, lakini tukisema tu kwa sababu ya kufurahishana tutakuwa hatuendi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu Ilani ya uchaguzi ya Chama chetu imeweka mambo mengi sana nafikiri, samahani kwa siku zijazo hata vyama vya siasa ni vizuri mgombea Urais akapatikana kabla ilani hazijaandikwa. Kwa sababu matokeo yake hata Rais huyu amekuta ilani ina ahadi 148; hata ule utekelezaji ule wa milioni 50 kila Kijiji mpaka wakati mwingine namuonea huruma Rais; kwa sababu unakuta umeandikiwa vitu walioandika watu wengine wewe unaambiwa nenda katekeleze. Nadhani tufike mahali tuseme ukweli kwa lengo la kulisaidia Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la viwanda tunawashukuru sana Kamati mmefanya kazi nzuri sana lakini pia tuache siasa kwenye viwanda. Ukianza kusema nakuletea kiwanda huna kiwanda mfukoni, don’t do that; mtapiga sound hapa wee 20 years inakaribia kuisha, kesho tutasema jiulizeni tu. Niombe Mheshimiwa Mwijage wewe baba mkwe sijui nani sielewi vizuri lakini tusaidie tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfanye stadi nzuri ya mfumo wa uchumi duniani ulivyo sasa. Mkifanya utafiti wa kutosha kwamba mfumo wa uchumi duniani ukoje then unaweza kuja na hii concrete idea ukafika mahali ukasema tunachofanya hiki, ni hiki na hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa mwisho tu kwa mfano, viwanda vya kuchambua pamba, tuviimarishe vile ili mafuta haya yazalishwe hapa nchini, lakini pia tuwasaidie wakulima bila kuboresha kilimo tutaimba wimbo wa viwanda leo, kesho na kesho kutwa. Kila Kijiji leo tuna extension officers lakini wanasaidia wananchi wetu kwenye kilimo vipi? Bado wananchi wanamwaga mbegu na hawa ni waajiriwa wa Serikali na wanalipwa; kila mwisho wa mwezi kuna extension officer anapata mshahara, ana kazi gani zaidi ya kupima ng‟ombe na anachukua maini, they have nothing to do.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kuboresha kilimo mfumo huu tunaouzungumza wa viwanda utatusumbua sana wazee wangu. Tukae chini tutafakari nchi yetu iweze kwenda mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na nawashukuru kwa mara nyingine tena niwapongeze sana Timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys kwa kufuzu kwa michezo ya under seventeen ya Afrika, hongera sana Mheshimiwa Nape na timu yako yote; sasa tujipange basi kuiandaa timu yetu kwa sababu hiyo nayo pia ni sehemu ya viwanda. Ahsante sana.