Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba nichangie hoja ya Kamati inayotusimamia ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Balozi Adadi, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa kuwasilisha kwa ufasaha Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati yake hususan masuala yaliyotekelezwa na Wizara yangu katika kipindi cha Januari 2016 hadi Januari 2017. Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutambua na kushukuru mchango wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wote wa Kamati katika kipindi chote ambapo wamewezesha Wizara yangu kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi na weledi. Wizara yangu kwa kuzingatia ushauri na miongozo ya Kamati yetu katika kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017, imeweza kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake pamoja na malengo yaliyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 – 2020 kwa kiwango kikubwa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, haya yote yamewezekana kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Wizara, Kamati yetu, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Wizara ya Fedha, Wizara za kisekta, taasisi za Serikali na sekta binafsi. Ni dhamira ya Wizara yangu kuendelea kutekeleza dhima ya Hapa Kazi Tu kwa ufanisi na weledi ili kuwezesha nchi yetu kufikia maelengo na matarajio yake ya uchumi wa viwanda. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa shukrani zangu, naomba sasa kuchangia baadhi ya hoja za Waheshimiwa Wabunge na mapendekezo ya Kamati na ambayo yameletwa katika Wizara yangu. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ilikuwa ni mapendekezo ya Kamati ambapo ilikuwa inashauri kwamba Serikali itoe fedha zinazotengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kama ilivyoidhinishwa na Bunge ili kufanikisha azma ya Serikali kuhusiana na miradi. Ushauri huu umepokelewa na Wizara yangu na itaendelea kupeleka fedha katika miradi ya maendeleo iliyopangwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini napenda tu kutoa taarifa kwa Bunge lako Tukufu kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017, Wizara ilitengewe kiasi cha shilingi bilioni nane kwa ajili ya bajeti ya maendeleo na hadi kufikia Februari, 2017 Wizara imepokea kiasi cha shilingi bilioni 3.4 ambayo ni sawa na asilimia 43.62. Kiasi cha shilingi bilioni 2.1 zimepelekwa Ubalozi wa Stockholm (Sweden) na shilingi bilioni 1.3 zimepelekwa Maputo, Msumbiji. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kukosekana kwa Balozi Ndogo na Uwakilishi wa Heshima kwenye baadhi ya miji yenye fursa nyingi za kiuchumi kunaathiri malengo ya Serikali ya kukuza uchumi wa nchi kupitia diplomasia ya uchumi, hilo sisi tunalipokea na tunakubaliana na jinsi Kamati ilivyoelekeza. Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nitoe tu status ya sasa hivi kwamba Mheshimiwa Rais ameweza kuruhusu kufungua balozi sita mpya ambazo ni katika Miji ya Doha (Qatar), Ankara (Uturuki), Tel Aviv (Israel), Seoul (Korea Kusini), Khartoum (Sudan) na Algeria (Algiers). Aidha, Serikali inatemegea kufungua consular zifuatazo ambazo ni za Balozi Ndogo katika Miji ya Lubumbashi - Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Lagos - Nigeria na Guangzhou - China. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la tatu ambalo lilikuwa linahusu APRM Tanzania kutokuwa na hadhi ya kisheria yaani kwa Kiingereza legal entity. Tunaweza kusema tu kwamba Wizara pamoja na taasisi hii ya APRMtulishawasilisha nyaraka katika Ofisi ya AG naye ameipitia na kwa sasa hivi imepelekwa katika Wizara ya Utumishi ili na wao waweze kuichambua na kuangalia upangaji wa muundo wa taasisi hii. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu malimbikizo ya michango ya uanachama wa Tanzania katika Taasisi ya APRM ya Afrika kwamba yanapunguza hadhi ya nchi yetu mbele ya jamii ya kimataifa, Wizara inatambua umuhimu wa kulipa kwa wakati michango katika mashirika mbalimbali ya kikanda na kimataifa ambayo Tanzania ni mwanachama. Wizara imekwishawasilisha orodha ya michango inayotakiwa kulipwa kwa ajili ya kutatua changamoto ambayo imetajwa na Kamati na sisi kama Wizara tutaendelea kufuatilia Hazina kuhusu ulipaji wa michango hii. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine linalohusu APRM kutoa elimu ya kutosha kwa umma kuhusu faida zake. Hili sisi tunapokea mchango wa Kamati na ushauri wake na tutaufanyia kazi na tutahakikisha katika bajeti inayokuja ya mwaka 2017/2018 tuweke hilo ili tuweze kusimamia vizuri jambo hilo. Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni ufinyu wa bajeti ya matumizi ya kawaida, ya maendeleo, kunachangia Chuo cha Diplomasia kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo hali inayoweza kusababisha chuo hicho kufutwa na usajili wa NACTE. Tunachoweza kusema ni kwamba Serikali inaendelea kuongeza bajeti ya Chuo cha Diplomasia ili kukidhi mahitaji ya NACTE. Pamoja na juhudi hizo kwa taarifa napenda kuwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba Wizara kwa kupitia mahusiano yake mazuri na nchi rafiki imeingia makubaliano na nchi ya Kuwait ili kukiwezesha chuo katika nyanja ya kukijengea uwezo hususani…
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu mengine nitawasilisha. Ahsante.