Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru nitatoa maoni yangu na mapendekezo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge. Kabla ya kutoa mapendekezo yangu nataka turejee katika Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara 63(2) kujikumbushia tu Waheshimiwa Wabunge. Sehemu hii inasema kwamba:- “Bunge litakuwa chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii”. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nimeamua kusema haya au kujikumbushia nini kinatuongoza katika nchi yetu kama Wabunge? Nina muda wa mwaka mmoja na zaidi hapa Bungeni, nikizingatia haya tuliyoambiwa, lakini ukiangalia mwenendo wetu nimeona kuna upungufu kwa jinsi ambavyo tunaishauri na kuifuatilia Serikali. Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasimama hapa Mbunge mmoja mmoja tunatoa mapendekezo yetu kwa Wizara husika, tunatoa mapendekezo yetu kama Kamati husika lakini sisi tunaotoa hayo mapendekezo hatufuatilii utendaji, hakuna accountability upande wa pili. Waziri atakuja kujibu atasema sawa nimepokea au sawa hili sikubaliani nalo au hili nitalifanyia kazi lakini ukija mwaka unaofuata au Bunge linalofuata hatujui nini kimetekeleza au kama kweli kimetekelezeka. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano dhahiri, mwaka 2013 au 2014, kuliundwa Kamati Maalum ambayo ilikuwa inachunguza na kuleta mapendekezo juu ya hii migongano baina ya wakulima, wafugaji, wawekezaji na mambo ya ardhi. Kamati ile ilitoa mapendekezo mazuri sana kwa Serikali lakini huu ni mwaka 2016 bado tunaongelea lugha hiyo hiyo. Kamati zinatoa mapendekezo hayo hayo hatuoni accountability kutoka upande wa pili. Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mwingine pia sisi ambao tulikuwa mtaani by then tulikuwa tunasikia kuhusu ESCROW, RICHMOND, Kamati zilitoa mapendekezo yake lakini sisi tuliotoka mtaani na sasa tumeingia Bungeni hatujui haya mapendekezo yaliishia wapi. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachotaka kushauri, Kamati kama itaona inafaa waongeze katika mapendekezo yao kwamba Bunge linatakiwa liwe na special monitary and evaluation plan, mikakati ya kutathmini tunachokipendekeza kwa Serikali au tunachokishauri kwa Serikali je kinatekelezeka na kinatekelezeka kwa wakati gani. Hii itatusaidia kama Serikali yetu kuzipambanua hizi changamoto na ku-move forward.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliuliza hapa na pale nikaambiwa wakati uliopita Bunge lilikuwa na kitengo cha kufuatilia ahadi za Serikali Bungeni, the government assurance unit. Sasa nataka kujua hiki kitengo kilikufa au kwa nini hakifanyi kazi kikatuambia ili tusiwe tunajirudiarudia kama Kamati au kwa Mbunge mmoja mmoja kushauri au kupendekeza mambo yale yale kila wakati. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa pili napenda kugusia kwenye mambo ya maadili kwa Kamati hii husika. Nimesoma booklet nikaona muundo wa Kamati, ina wajumbe 10 kutoka Chama Tawala na wajumbe sita (6) kutoka upande wa Upinzani. Sasa maadam hii Kamati ni special siyo kama Kamati nyingine inayoshughulikia maadili ya Wabunge, napendekeza ingekuwa ina 50-50 chance ili kuwe na uwazi au kusiwe na upendeleo wa aina yoyote hata na hao wajumbe wahusika wawe na mawazo mbadala. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nilichokiona kwa Wabunge wenzetu waliopewa adhabu mbalimbali, evidence gani zilitumika? Hata vyombo vya habari, waandishi wetu wa habari wako hapa ndani, kukitokea tafrani humu ndani utaona upande wa Upinzani ndiyo unaoshutiwa kwamba wamefanya fujo. Hata hivyo, in every action there is a reaction yaani kwenye kila tukio lazima kuna sababu nyuma yake, lazima kuna mmoja…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.