Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nipongeze Kamati zote. Hata hivyo, kabla sijaanza kuchangia, naomba nieleze jambo hili. Suala la vita ya madawa ya kulevya ni janga la Kitaifa. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwamba mtu yeyote anayesimama kuanza kupambana na vita ya madawa ya kulevya aidha awe ni mwizi au vyovyote atakavyokuwa kwa pamoja tuungane mkono na tumuunge mkono mtu huyo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo ambalo mimi nimekuwa nikijiuliza, hivi huyu Makonda mali wanazosema alikuwa nazo kabla hajaanza kupambana na vita ya madawa ya kulevya mbona hamkumleta Bungeni? Waheshimiwa Wabunge tuwe makini kuna mchezo unaendelea na huu mchezo tuugundue, tuukatae, tuungane na Makonda kwa nguvu zetu zote kupambana na vita ya madawa ya kulevya. Mlikuwa wapi? Kwa nini hamkumleta Bungeni kusema ni mwizi, kusema ana mali kibao? Huo mchezo tumeugundua na hatukubali tunaungana na Makonda kama ana upungufu, atawajibika kwa upungufu wake, lakini vita ya madawa ya kulevya tutaendelea naye. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niongelee suala la ulinzi na usalama. Niombe Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani tuangalie mazingira wanayofanyia kazi ya jeshi letu la polisi kwa kweli sio mazuri. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine sisi ambao tuko pembezoni tunaomba kwa kweli ulinzi uimarishwe kwenye mipaka yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru.