Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja… MWENYEKITI: Dakika tano wote. MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze tu kwa kusema kwamba nawapongeza Wajumbe wa Kamati zote tatu kwa kazi nzuri waliyofanya lakini nitachangia zaidi taarifa ya Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mambo ya Nje. Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema ufike wakati sasa hili Bunge lijione kwamba ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa hiyo zile Wizara za Muungano zipewe kipaumbele, hadhi na uzito na ustahili. Wizara ya Ulinzi na Usalama na Wizara ya Mambo ya Nje ni Wizara za Muungano lakini siku zote huwekwa pembezoni na matokeo yake haijadiliwi ipasavyo. Ukiangalia hivi vijitabu tulivyopewa cha Mambo ya Nje na Ulinzi ndiyo kibaya kuliko vyote, hata pini hazijakaa sawa, maandalizi yake hovyo, wakati ni mambo muhimu sana ya Jamhuri ya Muungano. Naomba hili lizingatiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo basi hata zile taasisi zilizoko kwenye Wizara ya Mambo ya Nje kwa mfano na zenyewe pia hazipewi uzito unaostahili. Chuo cha Diplomasia ni taasisi nyeti sana. Nchi yoyote ile taasisi inayohusika na masuala ya mambo ya nchi za nje inapewa uzito.
Chuo hiki kimekuwa chuo utadhani sijui cha kutengeneza watu gani! Hakina miundombinu mizuri, hakina vifaa vya kufundishia, Walimu wake wako so local! Mtu anafanya first degree mpaka PhD Mlimani pale hatoki mpaka anastaafu – huyu mtu atafundisha vitu gani jamani? Lazima walimu hawa wapewe exposure, wapelekwe nje, wapewe in service training periodically ili waandaliwe na wao waweze kuandaa foreign service officers wetu ipasavyo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, msongamano magerezani. Wamesema waliotangulia kwamba kuna watu wanawekwa mahabusu miaka. Tumeimba kesi chungu nzima, ya Masheikh tumeisema, sasa ni miaka minne ni mahabusu, kesi hazisemwi, watu mnaambiwa kumerundikana! Serikali haiamui, Serikali haiko serious. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati za Bunge haziwezeshwi ipasavyo. Nilitarajia Kamati ya Mambo ya Nje ionane na wadau, miongoni mwao wawepo pia wanafunzi wetu wanaosoma katika nchi mbalimbali basi angalau hao walioko kwenye nchi jirani hapa za Afrika Mashariki. Nimesikia baadhi ya wanafunzi wakilalamika wanavyokuwa mistreated, bahati mbaya ni katika nchi moja jirani mwenzetu Afrika Mashariki kwamba hawa wanalipishwa ada tofauti na vile ambavyo wangelipishwa na vilevile hawapati treatment kama amember country ya East African Community. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hiyo Inter-University Council ya East Africa ambayo inasemekana inashughulikia masuala haya, lakini ni muda mrefu sana hayapati ufumbuzi. Kwa hiyo, naamini kama hizi Kamati zingewezeshwa watu kama hawa wangeweza kufikiwa na Kamati za Bunge na masuala yao yangeweza kushughulikiwa ipasavyo. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nizungumzie kidogo kuhusu…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.