Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa ninaomba niunge mkono hoja za ripoti za Kamati zote tatu ambazo zimewasilishwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za Kamati. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijielekeze kwenye nyumba za askari wetu. Askari wetu wanaishi kwenye mazingira magumu sana katika nchi yetu ya Tanzania, unaweza ukasema labda Mkoa wa Katavi wanaishi labda vibaya, hawana nyumba, hawana nini, lakini ukitoka ukienda sehemu nyingine unasema loh, afadhali kwangu kuliko sehemu nyingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali hizi bajeti tunazipanga ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaomba zifike kwa wakati ili askari wetu waweze kujengewa nyumba au hata kuboreshewa nyumba wanazoishi, kwa sababu askari wetu ndiyo wanaotuweka sisi kwenye mazingira ya amani na upendo katika maeneo yetu husika. Tunaomba Serikali ijipange kuangalia hao askari. Tunawapa majukumu mengi makubwa ambayo wanatakiwa watekeleze lakini mazingira yao ambayo wanaishi sio mazingira rafiki. Tunaiomba Serikali hizi bajeti tunazopitisha safari hii Serikali ijipange kujenga nyumba angalau nyumba za askari. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tumeona at least Jeshi la Kujenga Taifa wamejengewa maghorofa sehemu mbalimbali, hapo tunaweza tukawapongeza kwa sababu wamejitahidi kwa upande mwingine, lakini kwa upande wa askari polisi bado hatujawatendea haki, wanaishi kwenye mazingira magumu sana. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende upande wa bodaboda. Bodaboda ni vijana wetu ambao wanajitafutia tuseme maisha yao na maisha haya wanajitafutia kutoka vyombo hivi ambavyo vimekuja kuwarahisishia maisha yao, lakini unakuta sasa ndani ya maeneo yetu kuna baadhi ya maaskari wanawanyanyasa sana bodaboda. Ninaomba basi Serikali, tunajua wale ni watoto wetu tumewapa ajira, wamejitafutia ajira kupitia bodaboda, tupange mikakati ya kuwafundisha usalama barabarani kwa sababu tunaona labda wanafanya vitendo vibaya, wanakwenda vibaya, wanaumia, wanapata ajali usiku na mchana, tufanye mikakati ya kuweza kuwapa semina ili waweze kujua jinsi gani watakavyotumia zile bodaboda. Ninaomba sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi itekeleze hayo.(Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaenda upande wa magereza. Magereza zetu zimejaa sana; sasa mimi najiuliza, kuna wengine wamekaa kule magerezani miaka kumi, kesi zao haziishi, uchunguzi bado unachunguzwa. Tunaomba Serikali sasa hivi ifanye mikakati ya kuwatoa wale watu wenye kesi zao za muda mrefu waweze kutoka mule ndani kwa sabaabu wanakula bure, wamekaa kama vile mahabusu wengine mpaka leo wamekaa miaka sita, saba, nane hawajahukumiwa sasa wanajaza magereza na chakula kila siku tunasema kinapotea, tunaendelea kuwaweka watu ambao wanatakiwa waweze kuondoka ili magereza ile iweze kupungua. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mahakama ndani ya nchi yetu. Mahakama bado, kama sisi kwetu Katavi mahakama hatuna ya Mkoa, hatuna hata Mahakama ya Wilaya huwezi ukasema kama tuna mMahakama. Tunaomba basi Serikali ijitahidi kujenga mahakama ndani ya nchi yetu ili tuweze kupata urahisi katika huduma mbalimbali za kimahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaenda kwenye Balozi zetu. Balozi zetu Wabunge wengi wamesema pesa haziendi kwa wakati. Wako nchi za nje huko wanaishi kwenye mazingira magumu sana. Tazameni Balozi zetu kuzipelekea pesa, unakuta sehemu nyingine balozi nyingine mazingira wanayoishi na lile jumba walilonalo utafikiri ni gofu. Hampeleki pesa za kutengeneza majengo ambayo yako maeneo hayo. Tunaomba Serikali, jitahidini jamani bajeti tunazopitisha, tafuteni pesa za kupeleka maeneo hayo ili mazingira yawe rafiki kwa wale watu tunaowapeleka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.