Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Mimi ninachangia taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imezungukwa na mataifa kadha wa kadha tunayafahamu wote; Kenya, Burundi na mengine na tunafahamu kwamba pia baada ya Kenya pale mbele kidogo kuna Somalia, Sudan Kusini, kuna Sudan kuna nchi nyingine pale, Eritrea na nyingine ambazo zimekuwa na hali mbaya ya kiusalama. Pale Somalia tunafahamu kuna tatizo la Al-Shabaab kundi la magaidi ambao wanavuruga sana usalama wa nchi hiyo na siyo peke yake hata nchi jirani Kenya imekuwa inashambuliwa mara kwa mara na Al-Shabaab. Mheshimiwa Mwenyekiti, hata sisi Tanzania inaaminika mashambulizi yale ya mwaka jana au mwaka juzi pale Tanga na Mwanza walikuwa ni Al-Shabaab wamekuja ndiyo wakaua watu pale halafu wakaondoka, hatukujua imetokea nini baadaye kama walikamatwa au iliishia wapi. Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hali ya usalama siyo nzuri kwa hiyo hatuwezi kusema kwamba tuko salama, ukanda huu tuko kwenye matatizo hayo ya ulinzi na usalama. Hao Al-Shabaab inasemekana wanafanya kazi pamoja na Boko Haram ambao wako Nigeria na kuna taarifa za uhakika kwamba Al-Shabaab na Boko Haram sasa hivi wanatafuta au wameshapata silaha za maangamizi, silaha za sumu (biological weapons) ambazo kwa kweli kama wakizitumia hizo ni hatari kubwa sana kwa yeyote ambaye zitamfikia. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Mkataba wa Kimataifa wa Kupambana na Silaha za Maangamizi (Convention on Biological Weapons) na umekuwepo muda mrefu, umewekwa pale UN nafikiri mwaka 1972 kwa nchi kusaini na ku-ratify na kufikia mwaka jana mwishoni nchi nyingi zimeshasaini mkataba huo na zime-ratify, nafikiri kama taarifa zangu ziko sahihi nchi karibu 200 zimeusaini mkataba huo na zimeu-ratify na zinautekeleza. Tanzania bado hatujasaini mkataba huo wa Convention on Biological Weapons na Mwenyekiti amesema pale wakati akiwasilisha kwamba mikataba mingi haijawa ratified, haijawa signed, sababu hazijulikani. Huu wa Biological Weapons Convention kwa umuhimu wake kwa nchi hii ilibidi tuwe tumeusaini siku nyingi sana na tumeu-ratify na tunautekeleza ili tuweze kuwa wanachama katika hiyo convention tupate msaada unaotakiwa linapotokea tatizo au tishio la kutumiwa kwa silaha za maangamizi, silaha za sumu. Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua Waziri atakapokuwa anatoa maelezo atuambie kwa nini hatujasaini mkataba huo na kuu-ratify, nini kimetuchelewesha tangu mwaka 1972 mpaka leo wenzetu wamesaini wengi tu nchi 200. Kwa nini, tumeshindwa kuusaini tunajiamini nini, tunasubiri tushambuliwe ndiyo tusaini mkataba huo au una matatizo gani, gharama labda kubwa sana au una masharti mbalimbali tujue nini kinazuia kuusaini mkataba huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliambiwa kwa mfano mkataba wa EPA juzi hapa, mwaka jana, hatukusaini kwa sababu kadha wa kadha za kibiashara, za kisiasa, huu wa kujikinga na silaha za maangamizi ni kitu gani kinatuzuia kusaini mkataba huu ili tujilinde zaidi na hali hiyo ambayo ni tishio kubwa sana kwetu. Tumeonja mashambulizi ya Al-Shabaab pale Tanga na Mwanza na siyo kwamba wameacha, tunasikia kila siku wanashambulia Kenya wako Somalia, kila mahali, Eritrea kule wanakwenda wanaua watu na maeneo mengine na mengine. Kwa hiyo napenda kujua sana hili jambo kwa nini hatukusaini na kama tunausaini hauna madhara tunausaini lini. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa dakika tano hizi.