Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea na hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia uhaba wa chakula. Kwanza niwashukuru watoa hoja wote, Kamati ya Ardhi na Kamati ya Kilimo, wamezungumza vizuri kwenye vitabu hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua tu kwa Mawaziri wanaohusika na Wizara hizi au wa Serikali sijawahi kuona kwamba kwa nini kila siku tunazungumza hivi vitu vinavyohusu mifugo, vinavyohusu ardhi kutopimwa na sina hakika kwamba hivi muda huu toka Wabunge wamekuja toka mwaka 1961, haya mambo ya kupima ardhi yalikuwa hayajazungumzwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokiomba kwa Wabunge wenzangu mkitaka Bunge hili tulitendee haki tuondoeni maneno yanayohusu U-CHADEMA na U-CCM. Mkiondoa haya maneno haya mtajenga Bunge ambalo ni imara na litasimamia Serikali. Tukifika humu tumebaki kubishana tu, tunabishana upande huu mara mwingine azushie Magufuli maneno, mara sijui Rais amefanya nini hatutafika hiyo. Tuzungumze mambo yanayohusu wananchi tuwaulize Serikali kwa nini kila siku tunazungumza migogoro ya mifugo na haitatuliki. Kama hakuna majibu tuseme sasa itakuaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kila siku tunakuja hapa maneno tu kama ngonjera tu, tukubaliane kwamba kama sisi ni wasimamizi wa Serikali, tuiulize Serikali kwa nini sasa mipango hii ya ardhi ambayo wakulima na wafugaji wanauana, kwa nini haifiki mwisho? Tutapata majibu siku hiyo. Kama haifiki mwisho hatuendi kwenye bajeti, tutapata majibu haya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze kwenye eneo langu la Bunda. Amekuja Waziri Mhagama, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu yangu hapa Ramo Makani, amekuja Naibu Waziri Kilimo, Mheshimiwa Ole-Nasha wamejionea hali halisi ya uharibufu ya wanyama tembo katika maeneo yangu, kata saba na Bunda Mjini. Wameona hali ilivyo, ikaahidiwa kwamba watapeleka chakula hakijaenda. Sasa nimeona humu wanaandika tupeleke mbegu bora, unaipanda wapi? Unapanda mbegu bora lakini tembo anaishi pale kila siku, wale Wazanzibar wanaita ndovu, anaishi pale pale kwenye shamba, tunapeleka mbegu bora ya nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hao tembo au ndovu hawawezi kutoka kwenye Jimbo lile watu watalima lini? Nawashukuru siku hizi wanajitahidi wapeleke na magari, lakini tembo au ndovu zimewashinda kutoa. Wanaishi pale pale kila siku, wamepeleka tochi imeshindikana. Kwa hiyo, nafikiri kwamba ni vizuri Serikali ituambie kama mpango wa eneo langu, vijiji vya Unyali, Maliwanda, Kihumbu, Nyamang’unta, Tingirima, Mgeta na kule kwa neighbour wangu Mheshimiwa Ester Bulaya, vijiji vya Nyamatoke na Mihale, watuambie kama maeneo haya hayawezi kulimwa basi Serikali ijiandae kwenda kuwapa chakula cha bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tembo sasa hivi wamefika wakati sasa wanavunja maghala, wanachukua chakula wanakula, hawana uwezo sasa wakulima pale, ngombe hawaendi porini wanakamatwa, sasa tunafanyaje? Kwa hiyo, tunaiomba Serikali katika hili kuwa wepesi wa kupeleka chakula cha msaada au chakula cha bei nafuu wapeleke katika Kata Saba za Jimbo langu. Hali ni mbaya na Kata Tatu za Jimbo la Bunda Mjini. Hali ni mbaya sana kwenye maeneo haya, njaa ni shida.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilimpa rafiki yangu, jirani yangu anaitwa Ryoba dakika tano uwe unanichunga kama zikizidi itakuwa mbaya zaidi. Kwa hiyo, niseme tu kitu kimoja…
MWENYEKITI: Mheshimiwa zimekwisha dakika tano zako.