Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa heshima na taadhima napenda kumshukuru Mungu wa mbinguni, aliyeziumba mbingu na ardhi kwa kunipa fursa hii mchana wa leo kuweza kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa miezi michache iliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nitakwenda moja kwa moja kujikita katika hotuba ya Mheshimiwa Rais katika sekta ya kilimo. Wilaya ya Ikungi ni miongoni mwa Wilaya zilizopo katika Mkoa wa Singida. Nikiri kwamba Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa michache inayochangia katika Pato la Taifa hasa katika sekta mafuta ya kupikia. Kilimo cha alizeti ni zao kubwa la kiuchumi na kibiashara kwa wakazi wa Mkoa wa Singida, Wilaya yangu ikiwa ni miongoni mwao. Nikiri kwamba so far Serikali yetu bado haijafanya juhudi za makusudi na za kutosha kuhakikisha kwamba inawatafutia wakulima wetu masoko ya kuuza mafuta na kuhakikisha mazao mbalimbali yanayotoka katika Mkoa wa Singida yanapata masoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mfano katika Wilaya ninayotoka na Jimbo la Singida Magharibi. Wilaya na Jimbo ninalotoka tunakabiliwa na changamoto kubwa ya upatikanaji wa masoko ya mafuta yanayozalishwa katika viwanda vidogo vidogo ambavyo kimsingi vinawasaidia wananchi wetu kupata kipato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nilizungumza hili pia na Waziri wa Kilimo tulipopata muda wa kuteta kidogo, tuna changamoto kubwa ya uharibifu wa ndege kwa lugha ya nyumbani wanawaita selengo. Mazao ya wananchi yamekuwa yakiliwa kwa kiwango kikubwa sana lakini kwa kipindi chote cha karibia miaka kumi Serikali haijaja na majibu ya kuweza kuwasaidia wananchi mazao yao yaache kuliwa na hawa ndege. Nilizungumza na kaka yangu Mwigulu Nchemba, ni rai yangu tena kwa Serikali yangu hii ya Awamu ya Tano, watu hawa wanatumia nguvu zao kuzalisha lakini kilio chao kimekuwa hakisikiki sawasawa Serikalini na hawapati majibu juu ya kutatua tatizo lao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu wamemchagua Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ni Waziri msikivu, Waziri mwenye moyo wa kuwasikiliza Wabunge, muda wote ukimpigia simu anakusikiliza.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwigulu Nchemba nakuomba kaka yangu spirit uliyonayo endelea nayo, Wabunge wengi wanakupenda kwa sababu huna kiburi, unajishusha chini ya miguu ya watu.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Nakuomba na natoa rai, panga ziara twende Jimboni kwangu ukaone uharibifu mkubwa unaofanywa na ndege wanaitwa selengo kwa mazao ya wanyonge hawa. Nakuahidi ukienda kutatua kero hii Mungu wa mbinguni atakukumbuka na thawabu zake zitakuwa juu yako. (Makofi)
Mhesheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze pia katika sekta ya elimu, nitumie fursa hii kwa dhati ya moyo wangu kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Simbachawene kwa agizo alilolitoa kwa Halmashauri zetu zote kuhakikisha kwamba watoto wa Kitanzania, is a shame kwa nchi, watoto wa Kitanzania kukaa chini ya mbao fifty years of independence. Tunaweza tusielewane hapa tukaona kwamba tunaishambulia Serikali lakini ni aibu kwa nchi watoto wa Kitanzania kukaa chini ya mbao miaka 50 ya uhuru. Haya mambo tusipoyasema sisi Wabunge wa CCM tutawapa nguvu watu wa Upinzani watayasema watabomoa Serikali yetu. (Makofi)
Kwa hiyo, mimi nasema, wito uliotolewa na Waziri Simbachawene na kaka yangu Simbachawene nikutie moyo, toa circular ipeleke kwa Wakurugenzi wako wote nchini, wape deadline na mikakati. Mimi kwa mfano kwenye Jimbo langu nimepeleka proposal Halmashauri, nimewaambia tuko tayari sisi kutoa nguvu kwa kutumia fedha zetu na kutafuta fedha za wafadhili, tuna mapori mengi tunayalinda wakati watoto wa Kitanzania wanakaa chini. Watu waruhusiwe wapate vibali, tukakate mbao, tuchonge madawati, nakuhakikishia suala la watoto wa Kitanzania kukaa chini itakuwa na history katika Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sekta ya afya, niiombe Serikali na nimuombe Mheshimiwa Waziri wa Afya, Mheshimiwa Rais alipokuwa akifanya kampeni miongoni mwa ahadi alizozitoa alisema kwamba tutahakikisha tunakwenda kujenga zahanati katika kila kijiji cha Taifa hili. Nimuombe dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, nina imani naye, ana uwezo wa kufanya kazi, Jimboni kwangu tumeshamuanzishia, tumeanza ujenzi wa zahanati katika vijiji 19. Namuomba Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Serikali pale ambapo Wabunge tunakuwa na initiatives zetu wenyewe na ku-solicit kutafuta fund kwa maarifa yetu, Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi isichelewe kutuunga mkono Wabunge kuhakikisha kwamba tuna-fulfil ndoto na njozi za Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongeze jambo lingine, ndugu yangu amezungumza hapa kuhusiana na Madiwani lakini pia niwatetee Wenyeviti wa Serikali za Vijiji. Kama inawezekana, najua vijiji ni vingi lakini kama Serikali inaweza ikajipanga at least katika kipindi chao cha uongozi cha miaka mitano wakaangaliwa. Watu hawa wanaisaidia Serikali na kufanya mambo makubwa, naomba Serikali pia iweze kuwakumbuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala mwisho ni reli ya kati na reli ya Singida. Ikumbukwe kwamba kipindi cha utawala wa Mheshimiwa Benjamini William Mkapa, Serikali ilitumia mamilioni ya shilingi kufanya uwekezaji wa kujenga reli iliyotoka Dodoma kuja mpaka Singida. Leo ninapozungumza reli hii ya Singida imeachwa haifanyi kazi. Ushauri wangu kwa Serikali ya chama changu, najua tupo watu baadhi tuna interest katika sekta ya transport, tujenge reserve ya kutosha ya mafuta pale Singida, reli ifanye kazi ya kusafirisha mafuta kutoka Dar es Salaam mpaka Singida. Magari yanayotoka Mwanza, Bukoba, Kagera, Shinyanga, Tabora wachukulie mafuta pale Singida, hii reli tuliijenga kwa faida gani?
Ndugu zangu kwa nini tunawekeza vitu halafu hatuzingatii suala zima la value for money? Hii reli haina kazi! Najua watu wanaweza wakani-attack maana najua kuna watu wana interest kwenye mambo ya malori na transport, I don’t care, lakini suala la msingi reli ya Singida iliyojengwa inawezaje kutumika hata kusaidia sekta ya barabara ambazo zinaharibika kwa sababu ya malori. Pelekeni mafuta Singida pale tutawapa maeneo ya kuwekeza kama mko tayari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima na taadhima nirudie tena kwa mara ya mwisho kwa dhati ya moyo wangu na bila chembe ya unafiki na kwa unyenyekevu mkubwa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
Aidha, naongeza kumuunga mkono kaka yangu Kitwanga, suala la NIDA mlilolifanya jana, nakupongeza Kitwanga simama, we are behind you, tunakuunga mkono.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mimi nataka nikuhakikishie, nimefanya kazi Serikalini, nilikuwa nikifanya kazi Fair Competition Commission mwaka 2010 kabla sijateuliwa na Rais, nimepigwa picha ya kutengenezewa kitambulisho cha Taifa mpaka leo sijapata. Kitwanga kanyaga, tunakuunga mkono na watu wa Mungu tutafunga na kuomba kwa ajili yako. We will pray for you brother.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, kwa heshima na taadhima, naunga mkono hoja kwa asilimia mia kwa mia, ahsanteni sana. (Makofi)