Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuweza kuchangia, na kama itakupendeza ntaomba dakika zangu mbili nimpatie Mheshimiwa Zitto Kabwe aweze kuendelea nazo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa uwasilishaji wa taarifa nzuri ambayo imesheheni mambo makubwa ya msingi. Nitajielekeza moja kwa moja katika suala la Mji mpya wa Kigamboni. Katika ukurasa wa sita wa taarifa hii Kamati hii ya Bunge ilitembelea Wakala wa Uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni na naomba ninukuu walichokisema:-
“Kamati ilifanya ziara katika Ofisi ya Wakala wa Uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni tarehe 18 Machi, 2016 na kupokea taarifa kuhusu maendeleo ya mradi. Kamati haikuridhishwa na hatua ya Serikali katika utekelezaji wa mradi huu na hadi wakati Kamati inapokea taarifa za utekelezaji wa miradi hakukuwa na fedha zozote zilizotengwa kwa ajili ya uendelezaji wa mradi ikiwa ni pamoja na kulipa fidia katika maeneo yatakayojengwa miundombinu.
Kutokana na hali hii hakukuwa na mradi wowote ulioonekana kuanzishwa na hivyo kupoteza maana halisi ya kuwa na mradi na uanzishwaji wa Wakala. Hali hii imesababisha Serikali kupoteza fedha za kulipia pango za wakala na kuwa na watendaji ambao hawana majukumu ya kutekeleza. Kamati inashauri Serikali iachane na mradi huu kwa kuwa umechukua muda mrefu bila kuwa na utekelezaji wowote.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naunga mkono hoja hii, ni mwaka wa tisa tangu Serikali itoe azimio la kujenga Mji wa Kigamboni. Hadi hivi sasa wananchi wa Kigamboni hawawezi wakajenga wala wakauza ardhi yao wala kuiendeleza, inawaletea umaskini mkubwa sana. Nami naunga mkono ripoti ya Kamati. Katika mwaka wa jana wa fedha Serikali haikutoa hata senti tano na wala hivi tunavyoongea hakuna hata senti tano ya fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka wa jana niliitisha mikutano ya wadau wa Kigamboni, Wenyeviti wangu wote wa Serikali za Mtaa, Madiwani na Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Temeke kabla halijavunjwa na tukatoka na azimio kwamba moja, KDA ivunjwe na mamlaka yake yakabidhiwe katika Halmashauri mpya ya Kigamboni.
Pili, suala zima la uendelezaji wa Kigamboni sasa kwa kuwa Kigamboni sasa hivi ni wilaya inayojitegemea, ni halmashauri inayojitegemea, ina Idara ya Mipango Miji ambayo ina sifa na vigezo vya kusimamia uendelezaji wa Kigamboni; muda wa miaka tisa umetosha sasa tunaomba sisi kama Wanakigamboni tuivunje KDA na shughuli zote zikabidhiwe katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaliomba sasa Waheshimiwa Wabunge hili nalo, pamoja na kwamba mmelitoa kwenye preamble, naomba liingie kama azimio ili sasa Serikali itoe msukumo zaidi, pamoja na mapendekezo ambayo tumeyaleta sisi kama Wanakigamboni hili sasa liwe ni azimio la Bunge ili sasa baada ya hapo Serikali iweze kutekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sina mengi ya kusema, naomba niishie hapo. Nashukuru sana.