Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii adimu ya kuchangia hizi Kamati mbili muhimu; Kamati ya Ardhi na Kamati ya Kilimo. Kamati zote mbili zimewasilisha ripoti nzuri sana na maoni yao ni mazuri sana na naiomba sana Serikali ichukue haya maoni na mapendekezo kwa uzito kulingana na umuhimu wa ardhi ya nchi yetu pamoja na kilimo kwa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza na suala la mipango miji. Sheria ya Ardhi ya Mipangomiji na Vijiji ni nzuri sana, lakini ukiangalia mipangilio yetu ya miji toka 2007 ilipotoka hiyo sheria kwa kweli inasikitisha sana. Napendekeza; kwa uzito wake wa mipangomiji sasa hivi hakuna miundombinu kwenye miji yetu, hakuna barabara, hakuna sehemu ya kupitisha mabomba; hilo lingezingatiwa na kuhakikisha namna ya kuzishirikisha taasisi binafsi na National Housing wakafanya kazi kwa pamoja kuhakikisha kuwa tunakuwa na mipangomiji mizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri nilionao ni kwenye Mji Mdogo wa Mbalizi. Pale Mji mdogo wa Mbalizi kulikuwa na watu 2,000 miaka 10 iliyopita lakini sasa hivi kuna watu wanaokaribia 150,000; lakini ukienda pale ni squatters tu hakuna mitaa. Kwa watu hao 150,000 hata miundombinu ya maji ni ile iliyokuwepo kwa ajili ya watu 2,000. Sasa hii inatuonesha ni namna gani tuko nyuma katika kupanga miji yetu. Wananchi wetu wanataka hizi huduma na sisi tunaiomba Serikali iangalie jinsi ya kuwasaidia wananchi. Sasa hivi vijiji vingi vinageuga kuwa miji, badala ya watu kujenga kiholela Serikali iwe ya kwanza kuhakikisha kuwa inapanga hayo maeneo na yanapimwa kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Mbalizi kuna ekari zaidi ya 6,000 za iliyokuwa Tanganyika Peckers miaka zaidi ya 50 iliyopita, kile kiwanda hakikuanza kufanya kazi, hizo ekari 6,000 zote hazijafanyiwa chochote na halmashauri na wananchi wote wa Mbeya DC waliamua kuwa waombe hili eneo ili liweze kupimwa liwe makazi ya watu, wautengeneze mji bora ambao utaonesha kioo cha Mbeya kwa sababu hilo eneo ndilo eneo ambalo liko karibu na uwanja wa ndege, ndilo eneo ambalo unatoka katika nchi jirani za Zambia mpaka Afrika Kusini unapoingia Mbeya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wananchi wameomba hilo eneo ili wapewe kuwe na mpangomji na Sheria Namba Nane kama sijakosea inasema uwekezaji wa mashamba kwa mijini usizidi eka tatu. Kwa hiyo hiyo eka 6,000 kwa kuwekwa mjini kwa ajili ya malisho ya ng’ombe nafikiri tutakuwa tunachekesha. Uzuri wake halmashauri imetenga eneo mbadala kwa sababu nao wanahitaji hiki kiwanda cha nyama na vilevile wanahitaji maboresho kuhakikisha kuwa tunafuga mifugo bora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, walichokifanya halmashauri, wamejenga wao machinjio ya kisasa kwa ajili ya soko la ndani na soko la nje. Kwa hiyo, eneo mbadala limepatikana na Serikali itakapopata mwekezaji eneo tunalo tayari. Sisi tunachoomba, hili eneo ambalo liko mjini iachiwe Halmashauri ya Mji wa Mbalizi ili tutengeneze makazi ya kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi shule zetu za msingi na sekondari zina idadi ya wanafunzi kubwa mno na hatuwezi kupanua shule, wanafunzi wakifaulu darasa la saba wanakwenda sekondari za mbali ambazo wanatembea zaidi ya kilometa 10, sidhani katika hali ya sasa hivi kama hayo yanakubalika. Kwa hiyo, tunaomba sana huu ushauri Serikali iuchukue.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumeona kwamba ardhi yetu pamoja na kuwa tajiri wanaofaidi ni wageni. Nilipotembelea National Housing na kamati yangu pale Tanganyika Peckers, Kawe, tuliambiwa kuwa ile ardhi mwekezaji alinunua kwa bilioni sita kwa ajili ya kiwanda, hakujenga, hakuendeleza. National Housing walipokwenda pale kutaka wapate lile eneo mwekezaji akakataa, alipotaka kununua kakataa, akakubali kwamba waingie joint venture, kwa bilioni sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti,Investment iliyoko pale sasa hivi ni mabilioni kama sio trilioni. Sasa jaribu kufikiria mtu mgeni unampa utajiri wa namna hii kwa mali yetu, hajafanya chochote. Sasa hilo lisijirudie katika maeneo mengine ya iliyokuwa Tanganyika Peckers.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo; mimi ni mkulima. Ili umsaidie mkulima unahitaji uwekezaji kwanza, unahitaji umpe mtaji, unahitaji utaalam, unahitaji masoko. Nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wamelichangia hili kwa umakini mkubwa sana, lakini angalia, mtaji utapata wapi? Benki ya wakulima leo hii haina mtaji, bilioni 60 ilizokuwa nazo imewekeza karibu bilioni tatu tu, sasa wakulima nani atawasaidia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kwenye wataalam wataalam wenyewe hatuwaoni wakija kwenye mashamba yetu. Mimi nikiwa kama mkulima sanasana wageni wangu wanaonitembelea kutoka Serikalini ni OSHA na…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.