Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi nichangie Kamati hii ya Kilimo, Mifugo na Maji na ninaomba ku-declare interest kwamba mimi ni mjumbe wa Kamati hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kusema kwamba kwa bahati mbaya sana tunadhani kwamba tunaweza kuwasaidia Watanzania angalau kuondokana na umaskini kupitia kilimo; jambo ambalo kwa kusema ule ukweli kwa haya yanayofanyika imekuwa ni vigumu sana na sidhani kama kweli tupo serious. Unaona leo kwenye ruzuku ya pembejeo za kilimo wamepeleka bilioni 20 kwenye bajeti, na bilioni 20 yenyewe hii, hizi fedha bado inaonekana hali ni mbaya na hizi fedha bilioni 20 haziwezi kuwatosha wakulima wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti tulishapendekeza siku za nyuma kwamba ikiwezekana huu mfumo wa kuweka ruzuku kwenye pembejeo za kilimo, Serikali iachane nao kabisa kwa sababu hauwasaidii wakulima wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukitaka kumsaidia mkulima ni mara mia ukapunguza kodi kwenye mbolea, kwa sababu kinachopandisha bei ya mbolea tunajua kabisa ni kodi; hii kodi ambayo ipo kwenye mbolea. Bahati nzuri hata Waziri amewahi kuzungumza kwamba kwenye mbolea kule kuna tatizo moja, kuna kitu kinaitwa udalali. Tukitaka kuwasaidia wakulima twendeni tukapunguze kodi kwenye mbolea na kwenye pembejeo nyingine ili wakulima wetu waipate dukani kwa bei ndogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ajabu sana leo nchi kama Malawi inatumia Bandari ya Dar es Salaam na inapofikisha mbolea nchini kwake bei ni ndogo sana mfuko hata shilingi elfu 20 haufiki; unapokwenda Zambia vivyo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wetu tumewachezea vya kutosha na Mheshimiwa Waziri, naomba niwe muwazi kabisa, msema mkweli ni mpenzi wa Mungu, tutakapokuwa tunaenda kwenye Bunge la Bajeti kabisa kama mchezo tunaoenda nao ndio huu, nitashika Shilingi ya Mheshimiwa Waziri na nitaomba huko mbele ikiwezekana uweze kuachia Wizara hiyo kwa sababu naona kama ina changamoto nyingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema ule ukweli kabisa hali jinsi ilivyo hata kwa wafugaji wetu; leo mifugo inakufa. Ukimuuliza Waziri hapa ndugu yangu mifugo iliyokufa; karibu nchi nzima mifugo inakufa kwa sababu ya ukame; hata takwimu hana. Hajui mifugo mingapi, ng’ombe wangapi wamekufa na mbuzi wangapi wamekufa. Sasa kwa hali kama hii, huu ni uzembe na udhaifu mkubwa sana kwa Wizara hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wamekuwa wakijipendekeza wanazungumza na uongo hadi wanadanganya wanasema kwamba njaa hakuna kwa sababu Mtukufu Rais amesema njaa hakuna na wao wanafuata hivyo hivyo. Kwa hiyo, inapofika mahali Rais akisema hii ni nyekundu si nyeupe, Waziri nae anasema hii ni nyekundu kwa sababu Rais kazungumza, huko sio kuwasaidia Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwe muwazi kabisa nchi nyingine, kwa mfano nchi kama Kenya mifugo ikifa Serikali inaamua kwenda kufidia, inawapa wananchi angalau mifugo kidogo kwa ajili ya kufidia kidogo wananchi wasiingie hasara. Sasa nashauri ikiwezekana na sisi Serikali yetu tuweze kuiga kwa majirani wa zetu hapa Kenya na nchi nyingine tuweze kuiga mfumo wanaoutumia. Mifugo inapokufa angalau tuweze kuwafidia kidogo wafugaji wetu, maana leo katika Taifa letu mifugo imekufa hatujui sasa ukame huu ukiendelea itakuwaje, maeneo mengine; hali ni mbaya zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya ziara maeneo mbalimbali, Kamati yetu tumekwenda Simanjiro na Kiteto, hali ni mbaya kweli kweli tunakutana na mifugo mingi, mizoga ng’ombe wamekufa njiani. Leo Serikali yetu kama haitachukua hatua za kuwafidia wale wafugaji hakika hali itakuwa ni mbaya zaidi kuliko wakati mwingine wowote ule katika Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme; kusema ule ukweli kabisa yapo maeneo mengine mengi tu ambayo bado Wizara hii ina matatizo. Alikuwa anaongea Mwigulu Nchemba hapa akiwa Waziri. Kuna matumaini fulani fulani hivi ambayo kidogo alitaka kuonesha. Anasema mbolea itapatikana madukani kama coca cola; Mheshimiwa Waziri amewasiliana na Mwigulu hiyo mbolea kama coca cola madukani ime… (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante