Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mimi naomba moja
kwa moja nijikite kwenye Wizara ya Miundombinu. Ikumbukwe kuwa Wilaya yetu ya Ludewa,
eneo kubwa liko mpakani mwa Malawi. Tanzania imepakana na Malawi, lakini eneo kubwa la
mpaka ni eneo la Wilaya ya Ludewa, ukilinganisha na Wilaya za Kyela na Nyasa. Lakini mpaka
sasa ninavyozungumza, eneo lile halina mawasiliano ya barabara, katika eneo la tarafa ile ya
mwambao ambayo ina kata tano na vijiji 15 vilivyoongozana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe kuna kipindi palitokea mgogoro, sasa mimi nikawa
najiuliza maswali, hivi mgogoro ule ungeendelea wakati hatuna barabara ya uhakika hali
ingekuwaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tu kukwambia na niiambie na Wizara wananchi wale
kwa sababu ya kuchoshwa kwa kutokuwa na barabara wameamua kuanza kulima wenyewe
kwa kutumia jembe la mkono. Wanalima kwa sururu, wanalima kwa jembe, wanalima kwa
chepe na mitarimbo. Ile ni dhamira ya dhati kabisa kuionesha Serikali kwamba wale watu wana
uhitaji wa hicho kitu. Vile vijiji vyote tumepangana, tunalima kwa jembe la mkono. Sasa niiombe
Serikali iwa-support wale watu na bahati nzuri Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri niliwaonesha
hata clips za watu wakiwa wanalima kwa jembe la mkono. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, usafiri mkubwa tunaoutegemea ni usafiri wa maboti, kwa
sababu meli inaweza ikapita mara moja kwa mwezi na isitoshe lile Ziwa huwa linachafuka sana,
kwa hiyo, inafikia kipindi usafiri unakosekana kabisa. Kwa hiyo, niiombe Serikali kwamba sasa
ichukue hatua kwa sababu wenzetu wa Nyasa wanayo barabara inayopita kando kando ya
Ziwa; wenzetu wa Kyela, wanayo barabara inayopita kando kando ya Ziwa. Kwa hiyo,
tuwaombe sasa na sisi upande wa Ludewa tuwe na barabara ambayo inaunganisha, kwanza
itakuza utalii, halafu pili italeta maendeleo kwa sababu kuna mazao kule ya uvuvi ambayo
yanapatikana kwa wingi.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia eneo lile halina mawasiliano ya simu kabisa. Mimi
ninaamini katika nchi nane tulizopakana nazo, eneo ambalo halina mtandao wa mawasiliano
ya simu inawezekana ikawa ni mwambao wa Ziwa Nyasa. Tuna kata tano, tuna vijiji 15 halafu
viko mpakani. Sasa cha kushangaza tumekuwa tukifatilia hii kitu sijajua tatizo liko wapi lakini
ningependa tu niseme watu wa Ludewa nao wangependa kuwa na maendeleo, wangependa
kuwa na mawasiliano ya simu maeneo yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu bandari. Pamoja na kuwa wakati mwingine
meli ile inatembea mara moja kwa mwezi, lakini bado bandari zake ziko kwenye umbali mrefu
sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante