Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwenye Kamati
ya Miundombinu naunga mkono hoja, taarifa yao ilikuwa nzuri sana. Nakubaliana nao hoja
kwamba kuzorota kwa huduma za reli kumesababisha utegemezi kwenye barabara kwa
usafirishaji wa abiria na mizigo. Na hiyo ina matokeo mabaya sana kwa upande wa uchumi
wetu, kwa sababu barabara zetu zinaharibika kwa haraka, tunaongeza gharama za ukarabati,
uhimilivu wa barabara unapungua kutoka miaka 20 hadi miaka mitano na gharama za usafiri
na usafirishaji kwa ujumla zinaadhiri uchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano lita moja ya petroli au dizeli kwa wastani inauzwa
kama shilingi 2,000; lakini kama mafuta yale yangekuwa yanasafirishwa kwa njia ya reli isingefika
bei hiyo ingekuwa labda shilingi 1000, shilingi 800 au shilingi 1200; na hiyo ingekuwa na matokeo
mazuri kwa uchumi. Kwa hiyo naomba kutoa wito Serikali isilale, ifanye mbinu zozote zile hata
kama gharama ni kubwa ijengwe reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa. Hiyo itakuwa ni
ukombozi mkubwa sana kwa Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, wakati mbinu hizo za kujenga reli zinafanyika, wasiache
kuendelea kujenga barabara za lami na barabara za changarawe hasa vijijini ili kusudi
kuwezesha gharama zetu za usafiri na usafirishaji kupungua. Kwetu kule Sikonge kuna barabara
muhimu ambazo nataka nizitaje hapa, barabara ya changarawe ya Tutuo - Izimbili - Usoke,
barabara ya changarawe ya Sikonge - Mibono - Kipili naomba ziangaliwe kwa macho mawili.
Barabara hizi tunadhani huwa kuna mchezo unafanyika. Kwa mfano barabara ya Sikonge -
Mibono - Kipili kila mwaka hupangiwa fedha kwamba itatengenezwa kutoka Sikonge mpaka
Kipili, lakini wakifika Mibono wanaacha, kila mwaka. Naomba mwaka huu imepangiwa milioni
862 ifike Kipili.
Naomba Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi aifikirie sana hiyo Wizara, na akubaliane na mimi
kwamba barabara ile itobolewe mwaka huu ifike Kipili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu ambalo napenda kulizungumzia, suala la kusema
Bandari ya Tanga na Mtwara zinajiendesha kwa hasara huo ni uongo uliopitiliza. Serikali ifanye
uchunguzi kubaini sababu kwa nini bandari hizi zijiendeshe kwa hasara wakati potential ni
kubwa? Kwa mfano wafanyabiashara wa pale Tanga Mjini kwa nini wapitishie mizigo
Mombasa? Ina maana kuna matatizo hapo kwenye bandari ya Tanga. Kwa hiyo, naomba sana
uchunguzi ufanyike ili watakaobainika hatua zichukuliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la nne suala la mawasiliano. Zinatumika fedha nyingi za mfuko
wa mawasiliano vijijini, lakini kunakuwa na wababaishaji upande wa mitambo ambayo
inawekwa. Inakuwa wananchi hawapati coverage ambayo tunaitaka kwenye mawasiliano,
mtambo unawekwa lakini coverage inakuwa ndogo sana. Sasa mimi naomba Wizara
inayohusika; kule kwetu kuna kata za Kipili, Kirumbi, Kilori, Kitunda, Ngoywa, Ipole, Kiloleli, Igigwa,
Nyahuwa na Mole, hakuna mawasiliano ya uhakika licha ya kwamba kuna minara. Mimi
naomba sana Wizara inayohusika ifuatilie matumizi ya fedha za mfuko wa mawasiliano vijijini, je,
zilitumika kihalali au kulikuwa na ubabaishaji, ili kusudi hatua zichukuliwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa kwenye umemeā€¦
NAIBU SPIKA: Muda umekwisha Mheshimiwa.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante naunga mkono hoja.