Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi naomba nipongeze Kamati
zote kwa taarifa walizowasilisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nina machache, kwanza ninapongeza kwa maendeleo
yote ambayo yamepatikana tangu uhuru mpaka sasa, maana kwa kweli tumepiga hatua
kubwa sana kwenye upande wa miundombinu ya barabara, lakini bado hata kwenye matumizi
ya simu za mikononi. Sasa hivi watu wanapata redio, mawasiliano na taarifa kwenye simu za
mkononi, yote ni maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nina mambo yafuatayo:-
Kwanza, nilikuwa naomba sana Wizara ihimize taasisi zinazohusika, kwamba kwenye kasi
ya maendeleo na wenyewe wakimbie. Kwa mfano, mji unapokua, miundombinu ya umeme
ambayo inakuwa imewekwa, TANESCO hawaendani na ile kasi. Utakuta maeneo watu
wameshajenga, hakuna transfoma hakuna nini, kwa hiyo, nilikuwa naomba sana waendane na
kasi ya maendeleo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna suala la hawa wakandarasi wa REA. Pale Mkalama,
kuna vijana 40 ambao wanadai hela zao kwa muda mrefu, miezi mitatu sasa hawapewi.
Mheshimiwa Waziri nilikuwa naomba tusaidie kuhusu mkandarasi yule, wale vijana walipwe
maana anawakimbia mpaka sasa hivi hataki kuwaona.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine nimepata taarifa kutoka kwa wananchi wanaolima
vitunguu kule Mkalama, kwamba kuna mtafiti mmoja amepewa leseni ili akatafiti madini
yanayopatikana pale na awaondoe wale wakulima wanaolima vile vitunguu. Ninaomba suala
hili lisitishwe mara moja, wananchi waachwe, waendelee kulima zao la vitunguu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna jambo lingine, Mheshimiwa Waziri nakushukuru
ulifika Singida ukaenda Tumuli ukakuta kuna wachimbaji wadogo wananyanyaswa na
wanadhulumiwa, ukaagiza tatizo lile litatuliwe, lakini mpaka sasa hivi bado wale wachimbaji
wadogo hawaelewi hatma yao. Kwa hiyo, nilikuwa ninaomba sana ufike pale ili uweze
kuwasaidia wale vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, yangu ni hayo tu. Ahsante.