Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi
nichangie kidogo hoja hizi mbili mbele yetu; Taarifa ya Miundombinu na Taarifa ya Nishati na
Madini.
Kwanza napenda kusema kwamba, sekta ya madini kwa kipindi hiki wawekezaji
wamepata shida sana, wengi wanakimbia, wengi wanarudi na sababu kubwa ni kwamba
wawekezaji wengi wana hofu kwamba security of tenure ya leseni zao ziko hatarini wanaweza
kunyang‟anywa leseni wakati wowote, kwa hiyo, nilikuwa naiomba Wizara na Kamati hebu
tujaribu kuishauri Serikali irudishe mazingira mazuri ya kuhamasisha Wawekezaji waje.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ni wachimbaji wadogo ambao kwa sasa hivi
wamekuwa wachimbaji haramu kwa sababu tozo na kodi mbalimbali za uchimbaji mdogo
zilipandishwa sana katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, kwa hiyo, wameshindwa kulipa na
wengi haramu bado wanaendelea kuchimba. Naiomba Wizara hebu fanyeni review ya
wachimbaji wadogo wanavyolipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, ni kuhusu mradi wa magwangala. Mheshimiwa
Musukuma amesema, wameweka mahali ambapo kwanza hata hawajapafanyia
environmental impact assessment na kwa sababu hawajui watatunzaje mazingira ya eneo lile,
Mheshimiwa Waziri labda au mtu mwingine alikwenda akachangua tu akasema wekeni hapa,
sasa hayachukuliwi. Maana yake ni nini? Eneo hilo litachafuka kimazingira. Kwa hiyo, sisi
tulikuwa tunaomba, Kamati inayosimamia mazingira huo mradi muusitishe. Tafuteni maeneo ya
kuwapa hawa Wachimbaji wadogo kama alivyosema Mheshimiwa Musukuma, ni vizuri
kushirikiana na mgodi, kushirikiana na wananchi mpate maeneo mazuri zaidi badala ya kufikiria
kuwapa magwangala ambayo hayana Madini. (Makofi)
Mwisho ni kuhusu bandari, Bandari ya Dar es salaam ilipata matatizo kidogo sasa hivi
tunaishukuru Serikali imeanza ku-pick up kidogo lakini kuna tatizo moja kubwa na tutalisema
sana kesho kwamba Mkuu wa Bandari ameamua kubadilisha watumishi pale, wale wasimamizi
wote kawabadilisha wako saba. Kaleta watu wengine ambao hata taaluma ya mambo ya
maritime hawana. Hii inaleta mdororo zaidi wa huduma katika bandari yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaiomba Kamati pamoja na Wizara mliangalie hili, watu
waliopewa nafasi pale, Wakurugenzi wote wanaomsaidia Bwana Kakoko pale hawana
taaluma wengi ni wahandisi kutoka TANROADS, tutaendeshaje mambo haya kwa urafiki?
Nashukuru kwa kunipa nafasi.