Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante kwa nafasi hii nitoe mchango
wangu. Kwanza niwapongeze Kamati ya Miundombinu pamoja na Kamati ya Nishati na Madini.
Baada ya pongezi hizo niende moja kwa moja kwenye point.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu bado liko pale pale kwa REA II ambao ni mradi
ulikuwa umeanza tarehe 25 Novemba, 2013 na ulikuwa uishe tarehe 25 Novemba, 2015. Mpaka
hivi ninavyozungumza hata robo haijafikia mradi ule, mkandarasi yule ni mbabaishaji SPENCON
na nilishasema hapa huyo mtu hatumtaki. Tunaomba tubadilishiwe mkandarasi aletwe
mkandarasi mwingine ili aweze kukamilisha mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu umeme ni fursa, kuna mashine za kukoboa,
saluni vijana wafungue za kiume na za kike, welding, carpentry, tufunge pump za maji za
umeme pia, zahanati zetu, vituo vya afya, shule. Sasa mtu anacheza cheza na maisha ya watu,
hatumtaki huyu mkandarasi tunataka mkandarasi mwingine. Naomba mlisikie hilo Mawaziri
mtusaidie tunataka umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ni REA III; tunaomba ianze. Tuliambiwa Desemba mwaka
uliopita lakini haikuanza, Februari haikuanza, tunaomba hii tarehe 15 Machi ambayo mmeisema
basi tunaomba ianze REA III. Kwangu kule Manyoni, vijiji ambavyo vina umeme ni vile ambavyo
vimepitiwa tu na njia kubwa ambavyo ni REA II, lakini kuingia ndani vijijini huko ambako ni mbali
na njia kuu hakuna umeme. Nikizungumzia Jimbo la Manyoni Mashariki, vijiji ambavyo vimepata
umeme kwa maana ya vile 58 ni karibu robo tu ndiyo vimepata umeme vingine vyote
havijapata umeme. Lakini pia REA III component ile ambayo mnasema kwa kijiji kimoja kwa
mfano, sasa hivi kwenye REA II ambavyo vilipata umeme ni robo tu ya kijiji lakini robo tatu ya kijiji
hakijawashwa umeme. Kwa hiyo, tunaomba ile 100 percent kijiji kiwashwe kwenye REA III.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, Mji wa Manyoni unapanuka, tumepima viwanja zaidi
ya 2000. Tunahitaji miradi ya umeme kwenye mji wa manyoni ili upanuzi wa mji uende pamoja
na huduma ya umeme. Nimeliongea hili, naomba tena nirudie mara ya pili, tafadhali sana
mtusaidie kwa sababu bei ya nguzo zile ni gharama kubwa, hatuwezi kumuuzia mtu kiwanja,
mnawaambia waungane wanunue nguzo wapeleke umeme haiwezekani hatuwezi kupanua
mji kwa namna hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa upande wa
miundombinu tunawashukuru tumepata ileā€¦
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa naunga hoja mkono, ahsante.