Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Niwapongeze kwa speech nzuri, nina mambo matatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja, nililisema na nazidi kulisema ili angalau wenzangu wa
Serikali huko walielewe. Sisi tuna madini mengi sana, lakini nchi hii katika wanaotuzunguka sisi
hatuna soko la madini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, leo Tanzania tukiweka soko la
madini kwamba mtu yoyote anayekuja pale sokoni hatumuulizi madini ameyatoa wapi lakini
yule anayekuja kununua anapoondoka tunaweka export levy, tutapata fedha nyingi sana kama Taifa. Fedha zile zitaingia kama kodi ni nyingi sana na tutapunguza kodi nyingi hizi za kero.
Lakini kila tukisema suala la madini, kwa sababu leo tunawachimbaji wadogo wadogo, hivi
wanauza dhahabu wapi? Nani anajua wanauza wapi? Kwa hiyo, inawezekana wanachimba
kwetu wanaenda kuuza kwingine kwa hiyo faida inaenda kwa wengine, lakini tuna uwezo wa
kuanzisha soko la madini Tanzania na watu wote wakaja wanunuzi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naongea na mtu mmoja hapa anasema, ukienda leo
Telaviv-Israel, moja ya biashara yao kubwa ni diamond na diamond wala haichimbwi Telaviv.
Walichofanya wameweka soko la diamond, so everybody ine the world anakwenda kuuza
diamond pale Telaviv. Kwa hiyo, na sisi kama Tanzania tukiweka soko hapa, tuna hakika
Wakongo wataleta dhahabu, nani ataleta dhahabu halafu watu wanaponunua
wanapoondoka ndiyo tunaweka export levy, tutapata fedha nyingi sana na hawa wanunuzi
watakaa kwenye hoteli zetu, watakula chakula chetu na wale Wauzaji wakishauza dhahabu
watanunua bidhaa so triple down effect kwenye economics itakuwa kubwa sana kama
Tanzania. (Makofi)
Lakini tunalisema hakuna anayetaka kulielewa, naomba sasa Profesa Muhongo, fanya
hili jambo liwe legacy yako. Anzisha soko la madini Tanzania watakukumbuka tu kwa sababu
utakuwa umeanzisha jambo kubwa sana na itakuwa ni source ya fedha nyingi sana kwa nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ni suala la mafuta, tumesema hapa bei za mafuta
duniani zinapanda na kushuka. Kama nchi lazima tuwe na strategic reserve ya mafuta ili
tukishakuwa na strategic reserve ya mafuta tunaweza tuka-survive kwa miezi sita bei ya mafuta
inayo treat haitatu-affect sisi kwa sababu tutakuwa tuna mafuta yetu ambayo tunatumia miezi
sita ama mwaka mmoja. Na hii haihitaji fedha nyingi sana kwa sababu tunayo TIPPER, tunayo
PUMA ambayo tuna asilimia 50, TIPPER tuna asilimia 50, ni suala la kuamua tu na hapa Serikali
itapata faida maeneo matatu:-
(i) Itapata faida kwenye TIPA kwa sababu tuna asilimia 50 kwenye reserve.
(ii) Itapata faida kwenye PUMA kwa sababu tuna asilimia 50.
(iii) Itapata faida ya mafuta tutaweza ku-control inflation, tuta-control bei ya mafuta
ambayo ni kubwa sana kwa maana ya nchi. (Makofi)
La mwisho ni suala la PPP project kwenye barabara, niombe sana, umefika wakati,
tumeongea habari ya PPP project ya barabara. Huu mwaka wa kumi niko Bungeni, tunaifanya
Dodoma kuwa Makao Makuu lazima tuifanye Dodoma iwe accessible. Lazima Dodoma iwe
karibu, hatuwezi kutegemea watu wote wapande ndege. Tutegemee kwamba wanaokuja
Dodoma atakayekuja kwa treni awahi, atakayekuja kwa gari awahi, atakayekuja kwa ndege
awahi, tunafanyaje? Lazima fedha zetu tuweke fedha ya watu binafsi wajenge super high way,
wata-charge...
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru huo ndiyo mchango wangu.