Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. SHUKURU KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya
kuchangia katika hoja ya Kamati hizi mbili, Miundombinu na Nishati.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuipa pongezi sana Serikali ya Awamu ya
Tano kwa kuthubutu kutenga fedha jumla ya shilingi trilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati
kwa standard gauge. Ni jambo kubwa, jambo la uthubutu na hilo ndilo ambalo limewezesha
wahisani kuweza kuunga mkono juhudi hizo na sasa hivi ujenzi karibu utaanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi zote duniani ambazo zina mtandao mzuri wa reli, zenye
uwezo mkubwa wa kuhudumia shehena kubwa na nyingi zimeunganisha usafiri huo wa reli
pamoja na bandari kwa maana ili tunapojenga reli yenye uwezo mkubwa, inayoweza kuhudumia shehena kubwa ya makontena na shehena mchanganyiko maana yake lazima
uwe na bandari kubwa ambayo inaweza kupokea mzigo huo na kuweza kuingiza kwenye reli.
Mwaka 2009 TPA wamefanyastadi na wakaibua mpango wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, niungane mkono na maoni ya Kamati ukurasa wa 41 ambapo
wameitaka Serikali iharakishe ujenzi wa reli hii ya kati, lakini uharakishaji wa ujenzi huu wa reli ya
kati lazima uungane sasa na uharakishaji wa ujenzi wa Bandari kubwa ya Bagamoyo ambayo
itakuwa na uwezo sasa wa kuzalisha shehena hiyo ambayo inahitajika kwa miundombinu
mikubwa hii. Bila kufanya hivyo tutakuwa tumetwanga maji katika kinu. Hatuwezi kupata
mafanikio yale ambayo tulikuwa tunayatarajia kwa uchumi wetu ambao unakua na ambao
tunategemea tufike katika uchumi wa kati mwaka 2020.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi huu wa Bandari ni muhimu tuupe kipaumbele na katika
kuupa Kipaumbele maana yake kwanza tumalize kadhia ile ya fidia kwa wale wananchi
ambao wanapisha ujenzi wa Bandari hii. Hivi sasa nisemapo baadhi ya wananchi wachache
bado hawajalipwa fidia zao. Nadhani ni muhimu zaidi wakati tunaamua kujenga Bandari
tuhakikishe kwamba hakuna mwananchi ambae hajalipwa fidia lakini wapo wananchi wale
ambao walipunjwa na Mkuu wa Wilaya au Kamati ya Mkuu wa Wilaya ilibainisha kwamba
wananchi 687 walipunjwa fidia katika mradi huu wa ujenzi wa bandari.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi wanahakikiwa. Naiomba Serikali iweze kutenga fedha
mapema ili mara uhakiki utakapomalizika hawa ambao walibainishwa kwamba wamepunjwa,
basi waweze kulipwa fedha zao kwa wakati na waweze kupisha ujenzi wa bandari. (Makofi)
Mhehimiwa Naibu Spika, pamoja na suala hili la fidia lakini kuna suala kubwa zaidi ya
kwamba ujenzi wa Bandari hii kubwa, unamaanisha kwamba tutaondosha katika ramani ya
Tanzania kijiji kinachoitwa Pande.
Mheshimiwa Naibu Spika, kijiji chote cha pande na Vitongoji viwili vya kijiji cha Mlingotini
vitaondoka kabisa katika ramani kwa maana vitamezwa na bandari hii, sasa hivi hao ndiyo
wapo katika mchakato wa kulipwa fidia. Sasa hawa wapewe maeneo ya kuhamia, kaya zaidi
ya 2,200 hawawezi wakaambiwa tu tokeni bila ya kuwa na sehemu ya kwenda. Muda
umeniishia naomba kuunga mkono hoja.