Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii
kuweza kuchangia hoja hii ya Kamati. Kwanza kabisa ningependa kupongeza sana Wizara hii
ya miundombinu, kwa kiwango kikubwa katika miezi sita hii ambayo tumekuwa nayo
imeonyesha dalala kweli kwamba kuna mambo ambayo yanaonekana kabisa na ni dhahiri
kabisa kwamba wamejitahidi kwa kadri ya uwezo wao. Waziri mwenyewe, Mheshimiwa Profesa
ametembea nafikiri nchi nzima hii nilikuwa kila nikiangalia television naangalia anapumzika
wakati gani lakini naamini kabisa amefika mikoa yote kwenye nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, utaona tu ni dhahiri kabisa ametuletea ndege zimeletwa hapa
bombardier mbili na nyingine zinakuja, mkataba wa reli umetiwa saini juzijuzi hapa, barabara
wametengeneza karibu kilometa 400 za lami, kuna flyovers ambazo zimeanza kuonekana pale
TAZARA, madaraja ya Coco Beach yameanza kushughulikiwa na magati mengi kule bandarini.
Kwa hiyo, ninachosema ni kwamba Wizara hii ya Miundombinu kwa kiasi fulani imejitahidi na
imetoa nuru ya Awamu ya Tano ni kitu gani ambayo inataka katika hiki kipindi cha miezi sita.
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengi ambayo imeyafanya especially
mambo ya reli, lakini utaona kwamba reli yetu ya Tanga kidogo imesahaulika na sijui ni kwa nini,
katika taarifa ya Kamati kwa kweli ingebidi na reli hii ya Tanga iangaliwe, hatuwezi kusubiri
mpaka reli ya kati imalizike ndiyo mipango wa kuanza kushughulikia reli ya Tanga ianzishwe.
Kwa hiyo, ningeomba vitu hivi viende kwa pamoja, simultaneously, huku inafanyika na huku
inafanyika kidogo.
Kuna suala la bandari pia, bandari Tanga sijaona kitu chochote ambacho kimefanyika
ukitilia maanani kwamba kuna bomba la mafuta ambalo linafanyika lakini mipango ya
kupanua ile bandari ya Tanga ili kuweza kukidhi mahitaji ya hili bomba ambalo linakuja bado
sijaiona. Kwa hiyo, ningeshauri Kamati iitake Serikali maandalizi hayo yaanze mapema ili n watu
wa Tanga waanze kufaidika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la barabara ambazo Wizara hii imejitahidi sana kwenye
kilometa 400 lakini barabara hasa jimboni kwangu, sijaiona na ninaomba Mheshimiwa Waziri
usisahau kuiingiza kwenye bajeti inayokuja barabara kilometa 40 ya Amani mpaka Muheza, ni
barabara muhimu sana na ambayo sasa hivi ina matatizo sana ya kuipitika. Kwa hiyo,
wananchi wa Muheza wanaamini kwamba safari hii barabara hiyo basi itawekwa kwenye
bajeti hii.
Vilevile kutokana na ukame ambao upo sasa hivi tunategemea kwamba ahadi zile za
Mheshimiwa Rais za kilometa tatu ambazo alituahidi pale Muheza basi zitatekelezwa kwa
sababu vumbi limekuwa kbwa na ukame umeongeza vumbi, basi tunategemea hizo kilometa
tatu tukipata lami kidogo tutapata ahueni ya lami. (Makofi)
Kuhusu mawasiliano, kuna tatizo kubwa, hasa kwenye Mlima wa Amani kule, ambapo
redio hazisikiki, simu hazisikiki na nilikwishamuomba Mheshimiwa Waziri ili aweze kuliangalia
tupate minara maana yake hatupati mawasiliano kabisa maeneo ya Amani, tarafa yote nzima,
vijiji vya Ngomole, vijiji vya Zirai, Vijiji vya Kwezitu, inakuwa mawasiliano ni matatizo makubwa
sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, labda nije kwenye Wizara ya Nishati na Madini; ishu ya bomba
la mafuta kutoka kule Hoima, Uganda mpaka Bandari yetu ya Tanga linasisimua sana pale
Mkoani Tanga na linasisimua sana hata Muheza. Lakini sijaona fukutofukuto lolote ambalo
wananchi wanaweza kusema kwamba sasa hivi hii kitu inafanyika, tunaona mkataba umetiwa
saini, lakini hatuoni…
Mheshimiwa Naibu Spika, REA Awamu ya Tatu…
NAIBU SPIKA: Muda umekwisha Mheshimiwa.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante
sana.