Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana kwa kunipa nafasi ili
niweze kuchangia kwenye taarifa za Kamati ya Nishati na Madini na ile ya Miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie nafasi hii nipongeze sana kamati zote hizi mbili
kwa kuja na ripoti nzuri; ripoti ambazo ukizisoma zimesheheni mapendekezo mazuri sana na
maazimio mazuri kwenye ripoti hizi na imani yangu kwamba Serikali itafanyia kazi na
kuyatekeleza vema mapendekezo ambayo yapo kwenye ripoti ya Kamati hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya ya miundombinu pamoja na nishati na madini
ni muhimu sana katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi yetu. Stadi zinaonesha asilimia 80
ya uwezeshaji wa uwekezaji inatokana na nishati hizi pamoja na miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mkazo mkubwa ukiwekwa kwenye sekta hizi
utachochea kiasi kikubwa sana cha maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimboni kwangu Ushetu hatuna umeme, tumebahatika kuwa
na vijiji vitatu tu ambavyo vimepata umeme, imekuwa ni vigumu sana kushawishi wawekezaji
kuja kuweka uwekezaji wa aina mbalimbali. Kwa hiyo, ninaamini kabisa katika hii REA III kwa vile
vijiji vyangu vimeonekana kwenye ule mpango basi nafikiri Mheshimiwa Waziri hapa
atanihakikishia kwamba tutapata umeme ili ile kasi ya kuvutia wawekezaji katika maeneo ya
kwetu tuweze na sisi kuweza kusukuma katika maeneo yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta hii ninasema ni muhimu katika ukuaji wa uchumi; hivi
majuzi tulikuwa tunazungumza juu parameter mbalimbali za ukuaji wa uchumi ikiwemo
mfumuko wa bei; nilitaka nijikite hapa kidogo nizungumze na namna ambavyo hata wakati
mwingine bei hii ya nishati ya umeme na mafuta inavyoweza kuathiri; kuna muda wa kutafsiri hili
suala la mfumuko wa bei.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu utakuja kuona mfumuko wa bei umekuwa
mkubwa sana katika hizi nishati za petroli, mafuta ya taa pamoja na vitu vinavyoambatana na
petroli. Kwa mfano kwa ripoti za BOT zinaonyesha kwamba kwa mwezi ule wa Oktoba na
Novemba mfumuko wa bei umepanda sana kwenye nishati hii ya mafuta na umeme kutoka
asilimia 6.2 kwenye asilimia 11.7. Sasa utakuja kuona kwamba hii ndio maana wakati mwingine inaleteleza tukitafsiri mfumuko wa bei inakuwa haieleweki kwa watumiaji hasa kule vijijini kwa
sababu utaona kwamba maeneo mengine kumekuwa na mfumuko katika rate ndogo, lakini hii
ukija kuchanganya kwa ujumla wake utakuja kuona unapata wastani wa nne nukta tano
mpaka nne nukta nane katika mwezi ule tu wa kutoka mwezi wa kumi kwenda mwezi wa kumi
na moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tukizungumza juu ya hali ilivyo vijijini saa nyingine inaweza
isieleweke sasa nataka niseme kwamba upo umuhimu sasa wa Serikali kutazama eneo hili la
nishati ili kuweza kuudhibiti huu mfumuko katika maeneo haya ya nishati ili ule uwiano wa ujumla
ulete maana halisi. Kwa hiyo, nilikuwa naona hii ni sehemu muhimu sana kwamba Serikali iweze
kuiangalia. Kwa sababu ukiona upandaji wa gharama hizi za nishati za mafuta na umeme
zinasababisha ukuaji ambao uko shaghala bagala katika maeneo mbalimbali ya utumiaji kama
kwenye chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu nilikuwa najaribu kuangalia ripoti hii utaona
kabisa kwamba wakati mfumuko wa bei unapanda kwenye nishati hii, bei ya chakula inakuwa
ni shida. Nilikuwa najaribu kuona katika kipindi kirefu kwa mfano, nimeangalia kipindi cha mwezi
Mei mpaka Oktoba, 2016 hii ilikuwa imeshuka inflation katika eneo hili. Lakini kipindi kilichofuata
baada ya Oktoba kume-shoot sana katika nishati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali naishauri ijaribu kuangalia kwa sababu nishati
hii inavyopanda, bei ya chakula inapanda ukizingatia kwamba wananchi wetu sasa
kwasababu ya miundombinu iliyopo mjini sehemu ambayo kuna umeme kumekuwa na
uzalishaji wa vyakula na bidhaa nyingine zimekuwa bora zaidi. Kwa hiyo, wananchi wanauza
mazao yao yanakuja mjini halafu baadae yanarudi kwa ajili ya utumiaji kule; kwa hiyo
kunakuwa kuna athari kubwa ndio maana tunaona kwamba bei ya chakula inakuwa ni shida.
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka nizungumze eneo lingine kwa sababu natoka maeneo
ya uzalishaji wa chakula, umuhimu wa matumizi ya nishati yetu katika kutengeneza mbolea,
niishauri tu Serikali kwamba ilitazame eneo hili ili uzalishaji wa mbolea uwe kwa wingi ndani ya
nchi lakini pia wananchi tuweze kupata mbolea kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nataka pia nijue kwamba ule mradi wa kutengeneza
mbolea ya Urea ambao kulikuwa kuna majadiliano kati ya TPDC na wale Wajerumani umefikia
wapi kwa sababu sisi ndiyo matumaini yetu. Katika msimu huu hatukupata kabisa mbolea,
tulipata mbolea kwa ajili ya kilimo cha tumbaku, wakulima wa mahindi hawajapata mbolea
sasa na wananchi wameitika vizuri sana kutumia hizi pembejeo. Na kwa kweli inatia matumaini
kwa sababu sasa wananchi wanaweza kuzalisha hadi gunia 30 kwa eka kama watawezeshwa.
Kwa hiyo, nilitaka niisemee Serikali itazame uzalishaji wa mbolea kwa kutumia hizi nishati zetu za
gesi asili ili mbolea ipatikane kwa wingi wananchi waweze kupata mbolea na kuweza kufanya
uzalishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie kusaidia wachimbaji wadogo, maeneo
ninayotoka tuna maeneo ambayo wachimbaji wadogo wanachimba. Sasa ni ombi langu tu
kwa Serikali kama alivyoahidi Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni isaidie kuweka mazingira
mazuri kwa wachimbaji wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kwa kusema naunga mkono hoja hizi, Serikali iweze
kutusaidia tuweze kusonga mbele. Ahsante.