Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kunipatia nafasi hii. Napenda sana kujadili taarifa hizi mbili ya Nishati na Madini pamoja na taarifa ya Miundombinu. Nitaanza kwa kujadili…
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na ninaishukuru Serikali kwa kazi nzuri inayoifanya kwa upande wa Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru naomba kuwapa pongezi Wizara ya Nishati na Madini na hasa kwa upande wa umeme. Kwa umeme
wa REA wamefanya mambo mazuri sana, wamesambaza umeme vijijini na nawapongeza sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba vile vijiji ambavyo bado hawajasambaza waweze kuvisambaza, Wizara inasema kuwa kuwa Awamu ya Tatu watasambaza vijiji vyote. Kwa hiyo, naomba kweli waweze kusamba vijiji vyote kwa Awamu hiyo ya Tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu umeme wa TANESCO, na wenyewe wanafanya vizuri ila kuna sehemu ambazo bado umeme haujafikiwa vizuri. Kwa hiyo, sehemu ambazo bado hazijafikiwa vizuri kwa mfano Mkoa wangu wa Morogoro, kuna kata pale Manispaa hazijafikiwa
na umeme. Kwa mfano Mindu, pamoja na Kihonda na kata zingine, Kiyegeya naomba sana waangalie waweze kuipatia umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, umeme wa TANESCO, kwa upande wa TANESCO imeonekana kuwa wanadai, na kweli wanadai mashirika mbalimbali kwa mfano magereza, mashule na vitu vingine, kudai sio vizuri. Nilikuwa naomba sana Serikali yetu angalau iweze kupunguza hayo
madeni kwa wakati na ifikie kuwa hayo madeni yamekwisha kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa wachimbaji wadogo wale wa madini, uwekezaji tunaupenda na tunaupenda sana kusudi tuweze kuendelea nchi yetu. Ila nilikuwa naomba kwa wale wachimbaji wadogo wadogo waweze kupewa mahali na wenyewe wawekezaji waweze kuwekeza, waweze kupata mahali pa kuchimba na waweze kupewa ruzuku na hiyo ruzuka iweze kupewa kwa wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa bajeti, bajeti inatolewa, bajeti ya Wizara zote tunapanga vizuri, bajeti ya Wizara hii ya Nishati na Madini tumeelezwa kuwa imeandaliwa vizuri, lakini inapokuja kutolewa haitolewi kwa wakati. Kwa hiyo, naomba kuwa mtiririko wa wa fedha
wa Wizara hii uweze kutoka kwa mpangilio kusudi wananchi waweze kupata umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema kuwa Tanzania ya viwanda ndio tunayokwenda nayo. Bila ya nishati ya umeme hatuwezi kuwa na viwanda, kwa hiyo, naomba sana hasa huko vijijini umeme uweze kuwepo hata mjini tuwe na umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa miundombinu na yenyewe natoa pongezi sana kwa Wizara hii kwa sababu wameweza kutengeneza barabara nyingi za lami, nawapa pongezi, wameweza kuunganisha mikoa mbalimbali kwa barabara za lami, nawapa pongezi.
Ila nawaomba sana kwenye barabara zile ambazo miji ya mikoa haijaunganishwa kwa mfano Kigoma na Kagera na mikoa mingine, naomba sana lami iweze kutumika kusudi watu tuweze kupata usafiri kwa urahisi pamoja na kusafirisha mizigo kwa urahisi na hayo ndio maendeleo.
Serikali yetu inafanya vizuri lakini naomba iweze kufikia na mikoa hiyo ambayo bado haijafikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa bajeti pia na yenyewe iweze kutolewa kwa wakati. Kwa upande wa makandarasi nafikiri wakiweza kulipwa kwa wakati wataweza kufanya mambo mazuri sana. Kwa hiyo, na wenyewe tuwaangalie kudai madeni ambayo hawalipwi
huwezi kuwa na moyo wa kuendelea na kazi kama hujalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kuongelea reli ya kati. Wananchi wengi wanasafiri na reli ya kati, wananchi wengi wanasafirisha mizigo yao na reli ya kati. Kutoharibu barabara inapendekeza hasa kusafiri na reli ya kati, kwa hiyo kujenga reli ya kati kwa standardsgauge Serikali naipa pongezi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naipa pongezi sana kwa kusaini mkataba ambao umesainiwa juzi juzi kusudi Uturuki waanze kujenga ile reli ya kati kwa standardgauge kwa kuanzia Dar es Salaam kuja mpaka Morogoro ikiwa wamu ya kwanza. Na naamini wananchi wengi watasafiri
kwa reli kwa sababu itatumia muda mfupi kama mlivyosikia kutoka Dar es Salaam mpaka Dodoma ni masaa mawili tutamia. Waheshimiwa Wabunge ikiisha naomba wote mtumie hii reli tuweze kuunga mkono Serikali yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mawasiliano, minara ya simu ni muhimu sana. Kuna vijiji vingi hasa Mkoa wangu wa Morogoro ambao bado hawajapata matumizi ya simu kwa sababu hakuna mawasiliano. Kwa hiyo, huo ni mfano tu, ni mikoa mingi, vijiji vingi ambayo minara
hakuna kwa hiyo mawasiliano yanakuwa hafifu. Kwa hiyo, nilikuwa naiomba Serikali, iweze kutimiza ahadi hiyo ya kupeleka mawasiliano hasa vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Chuo cha Ujenzi Morogoro. Chuo cha Ujenzi Morogoro ni kizuri sana na kinatoa wanafunzi wengi lakini hakijasajiliwa. Naomba kisajiliwe kusudi wahitimu waweze kujulikana vizuri sana naungana na Kamati na waweze kuajiriwa kwa sababu bado
tunawahitaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, bandari ya Tanga, Bagamoyo na bandari zinginezo kusudi tuende na maendeleo naomba sana tuweze kutimiza na bajeti iweze kutoka ya kumaliza hizi bandari ambazo nimezitaja kwa mfano bandari ya Tanga itasaidia kusafirisha mizigo ya Mikoa ya Kaskazini pamoja na nchi jirani za huko Kenya, Uganda na nchi zinginezo.(Makofi)
Mheshimiwa Niabu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia hii nafasi ya kutoa machache na kuchangia kwenye Kamati hizi nawapa pongezi sana mmefanya kazi nzuri sana, nashukuru na naunga mkono hoja. Ahsante sana.