Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru nimepata nafasi hii mara ya kwanza. Namshukuru Mwenyezi Mungu, tumejaliwa sote tuko pamoja na Insha Allah Mungu ataleta neema yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Spika wa Bunge pamoja nawe Naibu Spika kwa kazi yako nzuri. Katika Bunge hili mimi ni Baniani peke yangu. Kama nimekosea, mtanisamehe, lakini nitajitahidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napongeza Kamati yangu ya Miundombinu, imefanya kazi nzuri kabisa, pamoja nami, nimetembelea bandari, uwanja wa ndege, reli na barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Rais wangu wa Muungano, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, yeye amefanya kazi nzuri kabisa katika Tanzania yetu na nchi yetu.
Ameboresha miundombinu, barabara na mambo mengine ya reli na bandari. Nasi Wabunge tunamsaidia kufanya kazi apate sifa, kazi tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nampongeza Mheshimiwa Rais wangu wa Zanzibar, amefanya kazi nzuri na kuiboresha Zanzibar kwa miundombinu ya barabara, taa za solar Michenzani, Amani na sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza vile vile Waziri Mkuu. Waziri Mkuu anafanya kazi nzuri pamoja nasi na anakwenda kila mahali anafanya kazi yake nzuri, nasi tuko pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja katika mada yetu ya Kamati yetu ya Miundombinu.
Kamati yetu tumetembelea barabara zote na hivi juzi tumekwenda kuanzia Dar es Salaam, tumetoka Dodoma kwenda Arusha, tumeona barabara inajengwa na madaraja. Naipongeza Tanzania yetu na Mheshimiwa Rais amefanya kazi nzuri na kuweka uchumi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nataka kuzungumza kuhusu Uwanja wa Ndege.
Nimetembea viwanja vya ndege mbalimbali. Tumetoka kwenda Arusha, tumeona mambo mazuri, lakini yanatakiwa kuboreshwa. Mnara wa uwanja wa ndege ni mdogo sana, unatakiwa ufanywe mkubwa upate kuonekana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kamati yetu na mimi nimefaidika kumsaidia Mheshimiwa Rais, uwanja wa ndege wa Kilimanjaro wa International ni mzuri kabisa; lakini uwanja wa ndege wa Moshi, tunatakiwa tutie mkazo katika Serikali. Yaani uwanja wa ndege wa Moshi ile ndege inatua katika barabara mbovu kabisa. Tokea enzi ya British ipo pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali pamoja na Mheshimiwa Waziri, tuboreshe uwanja wetu ule, kwa sababu katika uwanja wa ndege wanakuja watalii. Watu wanakuja kwa utalii wanashuka Arusha wanateremka Kilimanjaro, lakini pale uwanja wa ndege wa Moshi upo
karibu na mlima wetu wa Kilimanjaro na Mount Meru. Uwanja wa ndege wa Arusha ndege nyingi zinatua pamoja na ATC, kwa hiyo, kwa nini usiboreshwe pale Moshi? Kwa sababu pale Moshi ni centre, wanakuja watalii wapate kwenda moja kwa moja katika mambo ya kutazama
wanyama pamoja na Mlima wetu wa Kilimanjaro.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumetembelea bandari nyingi sana. Bandari hii inahitaji kuboreshwa hasa. Tumekwenda Tanga, Mwanza, tumeona Bandari ya Mwanza ni nzuri, lakini inatakiwa kutiwa nguvu kabisa kuboreshwa ili kukuza uchumi, kusafirisha mizigo nchi za jirani.
Bandari ya Tanga ipo jirani na Zanzibar na Mombasa. Tumeona kuna uzito na ipo haja kubwa sana ya kuboresha, kupanua na kuleta meli kubwa za makontena makubwa kuliko Dar es Salaam ambapo tunateremsha kontena zetu. Ni bora kufika Tanga kwenda kwa nchi za jirani.
Vilevile tuboreshe bandari yetu ya Bagamoyo. Tumetembezwa, tumeridhika na tumesema Tanzania yetu naomba Mheshimiwa Rais aboreshe ile Bandari ya Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye sekta ya reli. Standard gauge ya reli sisi Kamati tulikwenda kutembea, nampongeza Mwenyekiti na Kamati yangu. Mara ya kwanza nimekwenda Tanzania nimeona reli. Standard gauge imekwama sehemu fulani, haikuweza kuboreshwa, lakini nashukuru Mheshimiwa Rais wetu amepata ufadhili mpya, tutaboresha tufanye kazi; reli yetu kwa upande wa Congo tupate kupeleka mali yetu Burundi na Rwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutakuwa tunaongeza uchumi wa nchi na hiyo ndiyo sekta muhimu. Wenzetu wa Kenya kutoka Mombasa wamefika Nairobi, wataunganisha na jirani pale Congo na wapi, sisi tutakosa soko. Naiomba Serikali tufanye kazi na namshukuru Mwenyezi
Mungu na naishukuru Serikali ya Awamu ya Tano, Mungu ampe uzima na afya Mheshimiwa Rais wetu afanye kazi ya ziada…
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa muda
wangu umekwisha, naunga mkono Kamati hii na Bunge letu. Ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme jambo moja, kama nimekosea, ulimi hauna mfupa. Ahsante.