Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nianze kwa kuipongeza Serikali kwa maana ya Rais mwenyewe, Baraza la Mawaziri na watendaji wote wa Serikali kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya ya kuiweka nchi yetu vizuri ili watu wakae sawa na mwisho wa siku wananchi wapate usawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyosema wenzangu, nianze kuipongeza Kamati yangu kwani nami nipo kwenye Kamati ya Katiba na Sheria, kwa kazi kubwa ambazo tumezifanya kwa ushirikiano wa pamoja. Pamoja na pongezi hizo, kama walivyosema wenzangu, changamoto za Kamati zipo na zimetusababishia pengine tusiweze kutekeleza majukumu yetu vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya changamoto kubwa ambayo tumekumbana nayo ni Kamati kutokuwa na fedha za kutosha hasa fedha kwa ajili ya ziara. Kama walivyosema wenzangu, kiasi kilichotengwa ni kidogo mno hivyo kimetusababishia kukwamishwa katika kutekeleza majukumu yetu. Kamati inapopewa fedha ya ziara inaiwezesha kwenda kujifunza juu ya majukumu yake. Kwa hiyo, Kamati inapokuwa haipati fedha za kutosha inashindwa kutekeleza majukumu yake vizuri ya kuisaidia na kuisimamia Serikali.
Mheshimwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika bajeti zinazokuja tuombe Serikali iweze kutoa fedha za kutosha tukizingatia kwamba Kamati ya Katiba na Sheria ni Kamati ambayo inasaidia wananchi wake kupata haki. Kwa hiyo, tusipojifunza kwa nchi nyingine au kwa wengine wanafanyaje shughuli zao inakuwa ni vigumu kutunga sheria ambayo itakuwa inatenda haki. Kwa hiyo, tuombe awamu inayokuja angalau Kamati zipate fedha za kutosha kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake hasa ya kuisimamia Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ziara zinatuwezesha sisi Wabunge kuweza kujua fedha zilizopelekwa kwenye taasisi mbalimbali kama zimefanya kazi ile ambayo imekusudiwa. Kwa hiyo, inatusaidia kujua value for money. Sasa Kamati inaposhindwa kwenda kwenye eneo husika kwa maana ya site na inapewa taarifa kwenye makaratasi tu lakini haiwezi kuona kitu kilichotendeka kwa uhalisia basi ile value for money hatuwezi kuiona vizuri. Kwa hiyo, niiombe Serikali yetu katika bajeti inayokuja ijitahidi kuhakikisha kwamba inatoa fedha za kutosha kwa ajili ya kufanya ziara ili Wabunge waweze kwenda ziara na kukagua miradi mbalimbali ambayo tumeitengea fedha ili kuona ilivyotekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine linahusu OC kwenye Halmashauri zetu. Halmashauri zimekuwa hazipelekewi fedha za kutosha kwa maana ya OC na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yake. Kwa mfano, Kitengo cha Ukaguzi, siku hizi tunasema Udhibiti Ubora wa Elimu. Kitengo hiki kimeshindwa kufanya kazi yake kabisa, shule nyingi zimeshindwa kufikiwa na wameshindwa kwenda kukagua kutokana na kukosa fedha hasa kwa ajili ya mafuta ya kuendea kwenye maeneo hayo. Hii ni hatari kama tunakuwa na shule ambazo hazikaguliwi. Kuna shule nyingine utakuta miaka mitatu au mitano imepita hazijakaguliwa. Labda ukaguzi unaofanyika ni ukaguzi ule wa muda mfupi wa kuangalia mambo machache.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji shule zetu ziweze kukaguliwa, Walimu waweze kupitiwa ili wakaguzi waweze kuwashauri juu ya mbinu za kujifunzia na kufundishia. Tusipofanya hivyo, itakuwa ni vigumu kuwaweka Walimu katika wakati wa kisasa na kuweza kuenenda kadri inavyopaswa kufundisha kulingana na syllabus na mambo ya taaluma yanavyobadilika. Kwa hiyo, ni muhimu hizi Halmashauri zipewe OC za kutosha ili taasisi zote zinazosimamiwa na Halmashauri kwa maana ya Ukaguzi na sekta nyingine ziweze kutekeleza majukumu yake vizuri na hatimaye tutaweza kupata elimu bora na tutaweza kuwa na watendaji wazuri kwa kuwa wana OC ambazo zitawawezesha kwenda kutekeleza majukumu yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nipongeze (kama walivyopongeza wenzangu) juu ya Mfuko wa TASAF, TASAF amekuwa mkombozi wa wanyonge. Huko vijijini sisi Wabunge tunaopita huko tumeona jinsi maisha ya watu yanavyobadilika na kuna maeneo mengine tumeshahamasisha hao wananchi ambao walikuwa wana kipato cha chini waweze kuanzisha miradi midogo midogo ili waweze kujikimu katika maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaiomba Serikali pindi itakapopata hela za kutosha iendelee kuongeza fedha za TASAF ili wananchi wengi maskini waweze kunufaika na fedha hizi kwa ajili ya kujikwamua katika maisha yao na hatimaye kuendelea kuanzisha miradi midogo midogo ambayo hiyo itawaondoa kutoka kwenye umaskini na hatimaye kuwa na hali nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye TASAF pia kuna tatizo limejitokeza kama wenzangu walivyosema, kuna baadhi ya wananchi walifanyiwa tathmini na wakaonekana kwamba wao ni kaya zile za hohe hahe (kaya maskini) na wakaingizwa kwenye mpango wa kupewa fedha lakini baadaye maafisa wetu wamepita na kusema kwamba hizo kaya hazina sifa za kuendelea kunufaika na mfuko wa TASAF. Baadhi ya kaya zilizo nyingi, kuna hizo kaya za wazee ambao hawana uwezo na kuna kaya nyingine wameondolewa kwenye mpango, uwezo wao ni mdogo, wanashindwa kusomesha watoto wao shule na hatimaye kuleta usumbufu na matatizo makubwa. Wengine wametoroka nyumba zao wakihofia kwamba watakamatwa na Serikali kwa kuwa maafisa waliokuwa wanaenda huko wanawatishia kwamba wasiporudisha hizo fedha basi watafungwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyojua Watanzania wanaogopa kufungwa, kwa hiyo wamekuwa wakiacha nyumba wakikimbia kuogopa kushikwa na mkono wa sheria kwa maana ya kurudisha fedha hizi. Tuombe basi Serikali ijaribu kuliangalia jambo hili, kama kweli ni kaya maskini, naomba tujaribu kuwaachia waendelee kunufaika na fedha hizi ili hatimaye waweze kusaidia familia zao kuweza kupata mahitaji muhimu hasa mahitaji ya kujikimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni juu ya uhamisho wa watumishi wa Serikali. Tulikuwa na zoezi la uhakiki, natumaini kwamba Serikali sasa imeshahakiki watumishi, imeshajua nani ni mtumishi hewa, nani ni mtumishi ambaye hana sifa za kuendelea kufanya kazi katika Serikali. Sasa kwa kuwa uhakiki umekwisha basi turuhusu hao watumishi wetu waweze kupata uhamisho. Sasa hivi kuna Walimu wengi wanaomba uhamisho wanakataliwa, kuna watumishi wa sekta ya afya wanakataliwa uhamisho kwa kisingizio kwamba bado tunafanya uhakiki wa watumishi hewa. Tuombe Serikali iweze kufungua milango hasa ya uhamisho ili watumishi wetu waweze kuhama. Kwa sababu ilivyo sasa hivi tukiwaacha hawa watumishi waendelee kuishi huko walipopangiwa kazi wasipate uhamisho ni hatari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vijana wameoa, kuna mabinti wameolewa wanataka kwenda kwa wenzao, lakini wanazuiwa kwa sababu ya kisingizio cha uhakiki wa watumishi. Kwa hiyo, tuombe kwa kuwa Serikali yetu ina mpango na inadhibiti maambukizi ya UKIMWI, tukiwaacha hawa vijana huko ambao wameoa na kuolewa baadaye tutakuta tumewapoteza kwa kujiingiza kwenye vitendo ambavyo vitawapelekea kupata UKIMWI kwa sababu ya kukaa na wenza wao mbali. Kwa hiyo, niombe Serikali yangu iweze kufungua milango ya uhamisho ili vijana wetu waweze kuhama na waweze kwenda waliko wenzi wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka nilizungumzie na wenzangu wamelizungumzia ni juu ya semina za viongozi. Semina hizi ni muhimu hasa kwa hawa wanaoteuliwa, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa. Kwa hiyo, tuombe wapewe semina za kutosha ili waweze kuongoza vizuri. Naamini kwamba wametoka kwenye kazi mbalimbali na kama walivyosema wenzangu kuna wengine hawaifahamu vizuri kazi ya Ukuu wa Wilaya na wengine Wakuu wa Idara, tuwape mafunzo ili waweze kusimamia vizuri majukumu yao na wasiwabughudhi watu. Kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge kwamba kuna baadhi ya maeneo wamekuwa wakiwatishia wananchi na watumishi…