Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuchangia hoja ambayo ipo hapo mezani na na-declare kwamba mimi pia ni Mjumbe mmojawapo wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa. Naona Mheshimiwa Suzan Kiwanga hajaja mimi nitaendelea tu na dakika zangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo langu kubwa ambalo nalikazia ni eneo la Utawala Bora ambalo Kamati imezungumza na kuainisha maeneo mbalimbali ambayo hayazingatii utawala bora katika Awamu hii ya Tano. Tukiangalia katika ile taarifa ya Kamati tumeona jinsi watu wanavyoswekwa jela kwa kutokuhudhuria tu vikao, ambayo ni kinyume za kanuni na taratibu za uendeshaji Serikalini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona hata kule Singida, Daktari ameswekwa rumande, kwa sababu kuna mgonjwa alikufa. Mimi sitetei uzembe lakini kuna factors nyingi ambazo zinaweza kufanya mgonjwa kufariki dunia. Kwa vile huyu Daktari amewekwa rumande, nasikia ame-resign na sioni ni jinsi gani huyu Daktari angerudi tena akaweza kufanya kazi vizuri katika ile hospitali. Hata wale watumishi wengine ambao wanafanya kazi na yule Daktari watapoteza morali kabisa ya kufanya kazi. Sidhani kama wale wagonjwa watapata tiba stahiki na huduma stahiki kwa jinsi ambavyo mwenzao ametupwa rumande. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hao ndio wanyonge tunaowazungumzia, maana yake hakuna Mbunge atakwenda kutibiwa huko Singida tunakozungumza. Kwa hiyo ni muhimu Serikali ikazingatia kanuni na taratibu za kuchukulia watumishi hatua za kinidhamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona jinsi gani Mtwara kule, Walimu Wakuu wameteremshwa vyeo kwa sababu tu ya matokeo ya form four. Hiyo siyo sahihi, kwa sababu tunamtafuta mchawi. Mchawi ni Serikali yenyewe, haijawekeza kwenye elimu. Kama Mwalimu ana wanafunzi 100 darasani, hana vitendea kazi, marupurupu yake hayajalipwa, utamtegemeaje huyu Mwalimu afanye kazi kwa ufanisi? Kwa hiyo Serikali, ijikite katika kuangalia factors ambazo zinateremsha elimu yetu na inafanya wanafunzi wetu wasiweze kufaulu vizuri madarasani. Hivyo kwa kweli hiyo haipendezi hata kidogo, Serikali isitafute mchawi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nikaangalia pia hii Mihimili miwili ya Bunge na Mahakama. Nakumbuka juzi Spika alisema kwamba Bunge tuko huru kabisa, sikubaliani kama sisi Bunge tuko huru! Juzi hapa tumenyimwa Bunge live na sisi ni Bunge, hakuna mtu amesimama kulisemea mbali ya Wapinzani, halafu tunasema Bunge tuko huru, tuna uhuru gani? Tukitaka kusafiri nje, mpaka tupate kibali Ikulu, tuna uhuru gani? Wakati iko namna ya kudhibiti matumizi ya Serikali, unaifanya katika bajeti tool. Inasema Bunge ninyi kwa mwaka huu mtapata milioni kadhaa kwa ajili ya safari zenu, lakini siyo tuombe ruhusa kwa Executive. Ina maana Bunge limekuwa compromised na hakuna mtu anayelisemea. Kwa hiyo, sisi hapa ni Bunge butu, hatuna meno na huu ndiyo ukweli na lazima tuukubali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia upande wa Mahakama, Mahakama tumenyimwa kufanya mikutano ya kisiasa na hiyo ni kinyume cha Katiba. Mahakama iko kimya, wala haijasema kitu. Jana Mheshimiwa Rais amesema kwamba wale Mawakili wanaowatetea watu ambao wamekosa wawekwe ndani, itakuwaje wawekwe ndani na juzi tumepitisha sheria ya Paralegals ya kutetea wanyonge. Sasa huyo Wakili unamweka ndani atamtetea nani?
watatetewa wale wenye pesa, kwa hiyo wale wanyonge watashindwa kutetewa. Hiyo haiendi sawa na lazima turudi katika misingi ya mihimili mitatu kila mmoja iwe inamwangalia mwenzake lakini kwa sasa hivi ilivyo Mahakama na Bunge tumekuwa compromised na huo ni ukweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakuja suala la decentralization kwa upande wa kimitaa. Ilipitishwa sera miaka kadhaa ya decentralization by devolution lakini kwa jinsi ambavyo Serikali inafanya sasa hivi, inapoka mamlaka ya Serikali za Mitaa. Tanzania ina kilomita za mraba karibu 945,000. Lazima Serikali za Mitaa iwe very strong na kwa mtindo huu, wamenyanganywa property tax na je, huu utawala bora tunaousema ni upi, wakati mkono wa Serikali wa Local Government unanyimwa pesa ambazo zingewasaidia kupeleka huduma kwa wananchi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili haliko sawa na ili neno la good governance tunalizungumza tu lakini kwa kweli hatulizingatii. Nashukuru sana Suzan Kiwanga amerudi sijui kama bado ana dakika. Ahsante.
MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ilikuwa ni hili la TASAF. TASAF tumekwenda kutembelea maeneo mbalimbali na wanafanya vizuri. Mimi naungana na wengine wote waliozungumza, napendekeza kwamba TASAF iendelee na TASAF sasa iwekewe mfumo mzuri kuweza kuwatambua. Kwa sababu inaelekea siyo kila mara Serikali ikishindwa kitu inafikiri kwamba itafanya kitu tofauti badala ya kuangalia imeshindwa wapi na kurekebisha. Kwa hiyo Serikali iangalie kwa nini huu mfumo haufanyi kazi vizuri na ni jinsi gani watu hewa wanaingizwa kuchukua hizo pesa za TASAF ifanyie kazi na siyo kumtafuta mchawi mwingine tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.