Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Watendaji wake kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kutengeneza Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia Mpango huu kwenye maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina azma nzuri katika kuelekea katika uchumi wa viwanda. Hili ni jambo jema sana litakaloivusha nchi yetu katika kuelekea kwenye uchumi mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika miaka ya 1970 tuliweka viwanda vingi sana ambavyo kwa sasa vimepoteza uwezo wake na vingine vimekufa kabisa. Hivyo, kwanza naishauri Serikali iangalie sababu za kuanguka kwa viwanda hivyo. Sababu hizo ndizo zitakazotuongoza kuelekea kwenye azma hii baada ya kuzifufua.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ni vyema Serikali ianze kujiandaa kwa kutayarisha rasilimali ambazo zitaweza kukabiliana na suala hili. Miongoni mwa rasilimali hizi ni rasilimali watu (HR). Serikali ianze kuwasomesha watu wetu badala ya kuja kutegemea wataalam kutoka nje ya nchi kama ilivyo katika sekta nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante.